Programu Ya Mikutano Ya Utumishi
Juma Toka Julai 8
Wimbo 201
Dak. 15:Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyochaguliwa kutoka katika Huduma Yetu ya Ufalme. Kwa kutumia mapendekezo kwenye ukurasa wa 4, fanyeni maonyesho mawili tofauti kuhusu jinsi ya kutoa Mnara wa Mlinzi wa Julai 15 na Amkeni! ya Julai 22. Katika kila tamasha, onyesheni njia tofauti ya kushughulikia kizuia-mazungumzo “Tayari sisi ni Wakristo huku.”—Ona kitabu Kutoa Sababu, ukurasa wa 19.
Dak. 10:Kisanduku cha Maulizo. Hotuba itakayotolewa na mzee ambaye atafanya matumizi ya habari kulingana na hali za mahali. Ikiwa habari hiyo haifai, chunguzeni makala “Tuonyeshe Heshima kwa Mahali pa Ibada ya Yehova,” kutoka katika Huduma Yetu ya Ufalme ya Februari 1998, ukurasa wa 1.
Dak. 20:Kupanga Mambo ili Kutoa Ushahidi wa Vivi Hivi. Mazungumzo pamoja na wasikilizaji kuhusu kitabu Huduma Yetu, ukurasa wa 93-4. Kwa kutumia ukurasa wa kwanza wa nyongeza ya Huduma Yetu ya Ufalme ya Januari 2002, fanyeni maonyesho mawili au matatu mafupi kuhusu jinsi ya kutoa ushahidi wa vivi hivi kwa mtu tusiyemjua, jirani, mshiriki wa familia, au mtu tunayejuana naye.
Wimbo 139 na sala ya kumalizia.
Juma Toka Julai 15
Wimbo 144
Dak. 10:Matangazo ya kwenu. Ripoti ya akaunti.
Dak. 15:Mahitaji ya kutaniko.
Dak. 20:Sababu Nzuri za Kutumia Biblia Katika Huduma Yetu. Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji. Yesu alijua Maandiko, naye aliyataja mara nyingi alipokuwa akifundisha. (Luka 24:27, 44-47) Yale aliyofundisha hayakutokana na yeye mwenyewe. (Yn. 7:16-18) Ni jambo la maana sisi pia tutumie Neno la Mungu. Hilo lina nguvu nyingi zaidi kuliko jambo lolote ambalo sisi tunaweza kusema kibinafsi. (Yn. 12:49, 50; Ebr. 4:12) Watu wanyofu wanavutwa na faraja na tumaini linalotolewa na Maandiko. Jiwekee mradi wa kusoma hata andiko moja la Biblia katika utoaji wako. Onyesha kwamba maandiko yametiwa ndani ya utoaji mbalimbali uliopendekezwa kwa ajili ya kutolea watu magazeti mwezi huu. Omba wasikilizaji watoe maelezo fulani kuhusu jinsi wamekuwa wakitumia Biblia katika huduma na matokeo ambayo jambo hilo limekuwa nayo juu yao wenyewe na juu ya wale wanaohubiria.
Wimbo 215 na sala ya kumalizia.
Juma Toka Julai 22
Wimbo 47
Dak. 10:Matangazo ya kwenu. Mzazi mmoja na mtoto wake wanaofanya kazi pamoja katika utumishi wanafanya onyesho kuhusu jinsi ya kutumia mapendekezo kwenye ukurasa wa 4 ili kutolea watu magazeti ya Agosti 1 na Agosti 8. Mmoja anafanya onyesho kuhusu Mnara wa Mlinzi, na mwengine kuhusu Amkeni! Tia wazazi moyo wazoeze watoto wao hatua kwa hatua katika huduma.
Dak. 17:Utasema Nini kwa Mtu Anayeuliza Kuhusu Uislamu? Hotuba na maonyesho. Kwa kutumia kitabu Jitihada ya Ainabinadamu ya Kutafuta Mungu, sura ya 12, eleza kwa kifupi ulinganifu ulioko kati ya Biblia na Kurani. (Ona kisanduku kwenye ukurasa wa 285.) Onyesha tofauti kati ya mafundisho ya Kiislamu kuhusu nafsi (ukurasa wa 297-300) na maelezo ya Biblia. (Ona kielezi-chini kwenye ukurasa wa 299.) Kwa kutumia kitabu Kutoa Sababu, ukurasa wa 232-6, fanyeni onyesho kuhusu jinsi ya kusaidia mtu aliyependezwa karibuni aelewe yale ambayo Biblia inasema kuhusu nafsi.
Dak. 18:Ninawezaje Kuepuka Hatari Zilizo Kwenye Internet? Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji, yenye kutegemea Amkeni! ya Januari 22, 2000, ukurasa wa 19-21. Onyesha mitego inayotokana na kutumia Internet bila kujizuiza, na ueleze jinsi ya kuepuka kuanguka katika mitego hiyo. Omba wasikilizaji watoe maelezo kuhusu jinsi walivyofaidika kwa kutumikisha shauri hilo. Ikiwa Internet haipatikani katika eneo lenu, tafadhali tumikisheni kanuni zinazopatikana katika makala hii kulingana na hali za kwenu.
Wimbo 61 na sala ya kumalizia.
Juma Toka Julai 29
Wimbo 54
Dak. 10:Matangazo ya kwenu. Kumbusha wahubiri watoe ripoti za utumishi wa shambani za Julai.
Dak. 10:“Programu Mpya ya Kusanyiko la Mzunguko.” Hotuba. Tangaza tarehe ya kusanyiko la mzunguko linalokuja. Himiza wote wahudhurie na kusikiliza programu kwa uangalifu. Tia moyo wahubiri wasiobatizwa wafikirie kutimiza sifa kwa ajili ya ubatizo. Fanyeni jitihada ya pekee ili kualika wanafunzi wa Biblia.
Dak. 25:“Iweni Wenye Kuunganishwa Pamoja kwa Upatano.”* Mnapozungumzia fungu la 3, tieni ndani maelezo kutoka katika Amkeni! ya Aprili 22, 2000, ukurasa wa 9-10. Kwenye fungu la 4, tieni ndani maelezo kutoka katika Mnara wa Mlinzi wa Aprili 1, 1995, ukurasa wa 16-17, fungu la 4-6.
Wimbo 81 na sala ya kumalizia.
Juma Toka Agosti 5
Wimbo 38
Dak. 10:Matangazo ya kwenu.
Dak. 20:“Kukusanya Watu wa Lugha Zote.”* Tieni ndani maelezo kutoka katika Mnara wa Mlinzi wa Aprili 1, 2002, ukurasa wa 24. Ikiwa inafaa, eleza kwa kifupi yale yanayofanywa ili kusaidia wale wanaozungumza lugha za kigeni katika eneo lenu; fanyeni onyesho la utoaji unaopatikana katika fungu la 4.
Dak. 15:Mambo yaliyoonwa katika kutaniko lenu. Omba wasikilizaji wasimulie mambo yenye kujenga yaliyoonwa mpaka sasa kuhusiana na kuhudhuria kusanyiko la wilaya, kufanya utumishi wa painia msaidizi, au kushiriki katika utendaji mwingine mbalimbali wa kiroho wakati wa mapumziko.
Wimbo 184 na sala ya kumalizia.
* Fanya maneno ya utangulizi yasifikie dakika moja, kisha uendelee na mazungumzo ya maulizo na majibu.