Habari Nzuri Sana Kwa Usomaji!
Je, haukubali kwamba vichwa vifuatavyo vya makala ya zamani ya Mnara wa Mlinzi vinasikika kuwa habari nzuri sana kwa usomaji?
‘Mungu Hujua na Hulinda Watu Wake’
‘Kufanya Maendeleo Katika Kuufuga Ulimi’
‘Ukristo Ulipofanywa Kichinichini’
‘Kuhubiri Kwa Matokeo Milangoni’
‘Kujibu Swali, Je, Umeokoka?’
Makala haya na mengine mengi yalitolewa katika Mnara wa Mlinzi mnamo miaka ya 1951 na 1952. Je, ni yenye kuzeeka hivi kwamba hatuwezi kufaidika kutokana nayo? Bila shaka hapana! Bado unaweza kupata mabuku ya Mnara wa Mlinzi katika Kifaransa ya miaka ya 1951 na 1952. (Mabuku fulani ya Kifaransa ya miaka ya 1953 mpaka 1959 yanapatikana pia) Mhubiri yeyote anayehitaji mabuku ya Mnara wa Mlinzi anaweza sasa kuyaomba kupitia mtumishi wa kutaniko anayeshughulika na vichapo.
Mwangalizi wa Shule ya Huduma ya Kitheokrasi anapaswa kuchunguza ikiwa buku lolote linakosa katika maktaba ya Jumba la Ufalme na kufanya ombi linalolingana.