Tumia Kitabu Mwabudu Mungu Ili Kuongoza Mafunzo ya Biblia
Kitabu Mwabudu Mungu wa Pekee wa Kweli kimekusudiwa ili kusaidia wapya wafanye maendeleo katika kweli na kuongeza kwa kina kirefu uthamini wao kwa Yehova na tengenezo lake. Kinaweza kutumiwa kuwa kitabu cha pili cha kujifunza na wanafunzi wa Biblia. Huduma Yetu ya Ufalme ya Juni 2000, ukurasa wa 4, inaeleza: “Ikiwa ni wazi kwamba mtu anafanya maendeleo, ingawa ni ya polepole, na kwamba ni mwenye kukomaza uthamini kwa yale anayojifunza, basi endelea na funzo la Biblia katika kitabu cha pili baada ya kumaliza broshua Anataka na kitabu Ujuzi. . . . Kwa vyovyote, funzo linapaswa kufanywa kwanza katika broshua Anataka na kitabu Ujuzi. Funzo la Biblia, ziara za kurudia, na wakati unaopitishwa ili kuendeleza funzo vingepaswa kuhesabiwa na kuripotiwa, hata ikiwa mwanafunzi anabatizwa mbele ya kumaliza kitabu cha pili.”
Ni nani mwingine anayeweza kufaidika na funzo la Biblia katika kitabu Mwabudu Mungu? Makala hiyohiyo inaendelea: “Ikiwa mnajua watu fulani ambao walijifunza [broshua Anataka na] kitabu Ujuzi wakati uliopita lakini hawakufanya maendeleo kufikia wakfu na ubatizo, mnaweza kutaka kufanya hatua ya kwanza ili kuona ikiwa wanaweza kurudilia tena funzo lao la Biblia.” Acheni tufanye jitihada ya pekee ili kuanzisha mafunzo katika kitabu Mwabudu Mungu pamoja nao mnamo Machi na Aprili.