Tuseme Nini Kuhusu Magazeti
MNARA WA MLINZI Sept. 15
“Katika ulimwengu wa leo watu fulani wanafikiri kwamba wananaswa katika ndoa isiyo na upendo. Watu kama hao wanaweza kwenda wapi ili kupata msaada? [Acha mtu ajibu.] Biblia inatuhakikishia kwamba kanuni za Mungu zinaweza kutusaidia. [Soma Isaya 48:17, 18.] Toleo hili la Mnara wa Mlinzi linazungumzia kanuni za Biblia zinazoweza kuimarisha ndoa.”
Amkeni! Sept. 22
“Tunashangazwa na uwezo ambao wanyama walio nao wa kupashana habari. Lakini je, ulijua kwamba kwa njia fulani wanadamu ni wa namna ya pekee? [Acha mtu ajibu. Kisha soma Zaburi 65:2.] Tofauti na wanyama, tunatamani kupashana habari na Mungu. Gazeti hili linazungumzia jinsi tunavyoweza kupashana habari vizuri na watu na Mungu.”
MNARA WA MLINZI Okt. 1
“Je, umekwisha kujiuliza, ‘Ikiwa Mungu ni mwenye upendo na mwenye uwezo wote, kwa nini haingilii mambo kwa ajili ya wale wanaoteseka?’ [Acha mtu ajibu.] Karibuni atamaliza matatizo yote. [Soma Isaya 65:17.] Wakati huohuo, tunapoteseka Mungu hatazami tu kwa kutojali, kama gazeti hili linavyoonyesha.”
Amkeni! Okt. 8
“Je, umesikia kwamba wakulima wengi wanaona kuwa vigumu kuendelea kufanya ukulima ili kuishi? [Acha mtu ajibu.] Toleo hili la Amkeni! linazungumzia tatizo hilo na pia ahadi ya Biblia ya nyakati bora zilizo mbele. [Soma Zaburi 72:16.] Nitakaporudi, nitapenda nikueleze jinsi Mungu atakavyotimiza hilo.”