Programu Ya Mikutano Ya Utumishi
Juma Toka Novemba 10
Wimbo 212
Dak. 10:Matangazo ya kwenu na Matangazo yaliyochaguliwa kutoka katika Huduma Yetu ya Ufalme. Fanyeni maonyesho mawili halisi kuhusu jinsi ya kutumia mapendekezo kwenye ukurasa wa 4 ili kutoa Mnara wa Mlinzi wa Novemba 15 na Amkeni! ya Novemba 22 katika eneo lenu.# Katika kila tamasha, magazeti hayo mawili yanapaswa kutolewa yakiwa pamoja, hata ingawa ni moja tu ndilo linalozungumziwa. Omba onyesho moja litie ndani maelezo kuhusu jinsi gharama ya kazi yetu ya ulimwenguni pote inavyolipiwa.—Ona Mnara wa Mlinzi, uku. 2, au Amkeni! uku. 5.
Dak. 15:“Iweni Tayari.”* Omba wasikilizaji watoe maelezo kuhusu kile kinachowasaidia wasiache mahangaiko na vikengeusha-fikira vya mfumo huu wa mambo vichukue wakati ambao ungetumiwa kwa matokeo zaidi katika mambo ya kiroho.
Dak. 20:Unachaguaje Marafiki Zako? Mazungumzo pamoja na wasikilizaji yanayotegemea kitabu Mwabudu Mungu, ukurasa wa 47-9. Ukitumia maulizo na maandiko yanayotajwa katika fungu la 13, omba wasikilizaji watoe maelezo kuhusu kanuni za Biblia ambazo zinapaswa kutuongoza katika kuchagua marafiki zetu.
Wimbo 127 na sala ya kumalizia.
Juma Toka Novemba 17
Wimbo 96
Dak. 12:Matangazo ya kwenu. Hoji wahubiri wawili au watatu ambao wamejionea mambo yanayopendeza katika utumishi wa shambani walipotumia toleo la vichapo la mwezi. Labda wengine waliweza kuanzisha mafunzo ya Biblia.
Dak. 15:Mahitaji ya kutaniko.
Dak. 18:“Pongezi Linaburudisha.”* Tia ndani maelezo kuhusu kitabu Furaha ya Familia, ukurasa wa 49-50, fungu la 21. Omba maelezo mafupi yatolewe na watu waliotiwa moyo na maneno ya pongezi kutoka kwa wengine.
Wimbo 58 na sala ya kumalizia.
Juma Toka Novemba 24
Wimbo 213
Dak. 12:Matangazo ya kwenu. Ripoti ya akaunti. Fanyeni maonyesho mawili tofauti kuhusu jinsi ya kutumia mapendekezo kwenye ukurasa wa 4 ili kutoa Mnara wa Mlinzi wa Desemba 1 na Amkeni! ya Desemba 8.# Andiko tofauti na lile linalopendekezwa kwenye ukurasa wa 4 linaweza kutumiwa. Katika kila tamasha, magazeti hayo mawili yanapaswa kutolewa yakiwa pamoja, hata ingawa ni moja tu ndilo linalozungumziwa. Katika utoaji mmoja, onyesheni jinsi ya kutolea watu magazeti kwa namna ya vivi hivi katika vyombo vya kusafirishia watu wote, au katika kikao kingine kinachofaa katika eneo lenu.
Dak. 10:Kisanduku cha Maulizo. Hotuba itakayotolewa na mzee.
Dak. 23:“Tusitawishe Urafiki wa Karibu Pamoja na Yehova.”* Tumia maulizo yanayoandaliwa. Fanya wasikilizaji watoe maelezo juu ya jinsi maandiko yanavyohusiana na habari. Chukueni mipango kimbele ili mtu mmoja au wawili watoe maelezo kuhusu kile kilichowasaidia waboreshe funzo lao la Biblia la kibinafsi.
Wimbo 202 na sala ya kumalizia.
Juma Toka Desemba 1
Wimbo 138
Dak. 10:Matangazo ya kwenu. Kumbusha wahubiri watoe ripoti za utumishi wa shambani za Novemba. Sema kuhusu toleo la vichapo la Desemba. Rudilia kwa kifupi utoaji uliopendekezwa, mmoja au mbili. Eleza jinsi wahubiri wanavyoweza kutumia Index des publications de la Société Watch Tower ili kupata utoaji zaidi.—Ona Huduma Yetu ya Ufalme ya Septemba 2001, uku. 2.
Dak. 15:Tusitawishe Roho ya Ukarimu. Hotuba itakayotolewa na mzee, inayotegemea Mnara wa Mlinzi wa Novemba 1, 2003, ukurasa wa 27-30. (Ikiwa toleo hilo halijapatikana, tafadhali tumia makala yenye kichwa “Ukarimu Mwingi Huleta Shangwe,” katika Mnara wa Mlinzi wa Novemba 1, 2000, ukurasa wa 28-31).
Dak. 20:Wenye Sifa za Ustahili wa Kutosha Kufundisha Wengine. Mazungumzo pamoja na wasikilizaji yanayotegemea Mnara wa Mlinzi wa Juni 1, 2000, ukurasa wa 16-17, fungu la 9-13. Kuwa na uwezo wa kufundisha kwa matokeo ni mradi wa msingi katika huduma yetu. Kufanikiwa kwetu katika kusaidia wale walio mfano wa kondoo kunategemea uwezo wetu wa kutoa ujumbe wa Ufalme kwa namna inayowaelimisha na kuwachochea. Zungumzieni maulizo yafuatayo: (1) Kuna tofauti gani kati ya kuhubiri na kufundisha? (it-2-F uku. 632 fu. 4) (2) Kwa nini wengine wana wasiwasi kuhusu kujaribu kuongoza funzo la Biblia? (3) Tunawezaje kuboresha uwezo wetu wa kufundisha? (4) Tunawezaje kuwa hakika kwamba mwanafunzi wetu anaelewa yale anayojifunza? (5) Ni mradi gani tunaopaswa kujaribu kusaidia mwanafunzi autimize?
Wimbo 70 na sala ya kumalizia.
* Fanya maneno ya utangulizi yasifikie dakika moja, kisha uendelee na mazungumzo ya maulizo na majibu.
# Tafadhali tumieni mapendekezo yaliyotolewa kuhusu magazeti ya karibuni zaidi yanayopatikana.