Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 1/04 uku. 1
  • Tunawezaje Kusaidia Wenzi wa Ndoa Wasio Mashahidi?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Tunawezaje Kusaidia Wenzi wa Ndoa Wasio Mashahidi?
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2004
Huduma Yetu ya Ufalme—2004
km 1/04 uku. 1

Tunawezaje Kusaidia Wenzi wa Ndoa Wasio Mashahidi?

1 Watumishi wengi wa Yehova ni wenye kuishi na wenzi wa ndoa wanaofurahia ndugu na wanaopendezwa na kutaniko, lakini bado wanajizuia kuwa watumishi wa Mungu. Mume wa dada mmoja alikubali: “Wazo la kwenda nyumba kwa nyumba lilikuwa kizuizi kikubwa kwangu.” Wengine huenda wana mazoea yasiyopatana na maandiko ambayo wanapaswa kushinda, au huenda wanajisikia kwamba ni vigumu kabisa kuheshimu programu ya kitheokrasi yenye mambo mengi kama wafanyavyo wake zao. Tunawezaje kuwasaidia?

2 Tuonyeshe Upendezi wa Pekee: Kuonyesha kwamba tunapendezwa kibinafsi na wengine na kujua mambo yanayowatia wasiwasi kunaweza kuwafungulia njia ili waitikie kweli ya Biblia. (Flp. 2:4) Wale ambao hapo zamani hawakuwa waamini pamoja na wenzi wao wa ndoa, mara nyingi wanasema kuhusu kupendezwa kwenye upendo ambako Mashahidi wengine waliwaonyesha. “José, mzee katika kutaniko, alionyesha upendezi wa pekee kwangu,” alieleza mume aliyetajwa hapo juu. “Nafikiri ni kitia moyo chake kilichonifanya mwishowe nianze kujifunza kwa bidii.” Mume mwingine anakumbuka kwamba akina ndugu waliomtembelea walifanya jitihada ili kuzungumza mambo yenye kumpendeza. “Nilianza kuona imani ya [mke wangu] kwa njia tofauti kabisa,” yeye alisema. “Marafiki wake walikuwa watu wenye akili sana walioweza kusema juu ya mambo tofauti-tofauti.”—1 Kor. 9:20-23.

3 Tutoe Msaada Unaofaa: Wenzi wa ndoa wasio Mashahidi wanaweza pia kuguswa na msaada wenye fadhili wanaotolewa. (Met. 3:27; Gal. 6:10) Gari la mume mmoja asiyeamini lilipoharibika, Shahidi mmoja kijana alikuja kumsaidia. “Hilo lilinivutia sana,” yeye anasema. Ndugu mwingine alipitisha siku nzima akimsaidia mume asiyeamini wa dada mmoja kujenga ua wa uwanja wake. Walipokuwa wakitumika na kuzungumza pamoja, walisitawisha urafiki. Juma mbili baadaye, mtu huyo alimfikia ndugu na kusema: “Wakati umefika wa mimi kufanya mabadiliko fulani katika maisha yangu. Je, ungejifunza Biblia pamoja na mimi?” Yeye alifanya maendeleo ya haraka na sasa ni Shahidi aliyebatizwa.

4 Tunapoendelea kutafuta katika eneo letu wale wanaostahili, acheni tuendelee kusaidia wale walio wenzi wa ndoa wasioamini wanaoishi na waamini wenzetu.—1 Tim. 2:1-4.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine