Matangazo
◼ Toleo la vichapo la Januari: Kitabu chochote kilichochapishwa kabla ya 1988 ambacho kutaniko linaweza kuwa nacho katika stoki. Ikiwa hamna chochote cha vitabu hivyo katika stoki, tafadhali chunguzeni ikiwa makutaniko ya kando-kando yana vichapo vya zamani vya ziada ambavyo mnaweza kutumia. Makutaniko ambayo hayana vitabu vya zamani yanaweza kutolea watu kitabu Jitihada ya Ainabinadamu ya Kutafuta Mungu. Februari: Mkaribie Yehova. Ikiwa kichapo hiki hakipatikani, kama toleo lingine, mnaweza kutumia kitabu Création (chapa ya aina kubwa au ndogo) au kitabu Upeo wa Ufunuo. Machi: Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele. Jitihada ya pekee itafanywa ili kuanzisha mafunzo ya Biblia ya nyumbani. Ikiwa watu wamekwisha kuwa na kichapo hicho, kitabu Sikiliza Unabii wa Danieli! kinaweza kutolewa.
◼ Kuanzia juma la machi 15, 2004, makutaniko yanayozungumza lugha ya Kifaransa na Kiswahili, yatajifunza kitabu Mkaribie Yehova katika Funzo la Kitabu la Kutaniko.
◼ Kuanzia Februari au nyuma zaidi kuanzia Machi 7, hotuba mpya ya watu wote itakayotolewa na waangalizi wa mzunguko itakuwa “Ni Maadili ya Nani Unayothamini?”
◼ Makutaniko yanapaswa kuchukua mipango yenye kufaa ili kuadhimisha Ukumbusho mwaka huu, Siku ya Yenga, Aprili 4, baada ya jua kutua. Ingawa hotuba inaweza kuanza mapema, kupitishwa kwa mifano hakupaswi kuanza mpaka jua linapokuwa limetua. Ifuatayo ni wakati mbalimbali ambapo jua litatua katika miji fulani mikubwa ya eneo letu: Pointe Noire, saa 12:16 ya jioni; Matadi, saa 12:09 ya jioni; Kinshasa na Brazzaville, saa 12:03 ya jioni; Bandundu-ville, saa 11:54 ya jioni; Kikwit, saa 11:48 ya jioni; Bumba, saa 11:37 ya jioni; Gemena, saa 12:47 ya jioni; Kananga, saa 12:37 ya jioni; Mbuji-Mayi, saa 12:29 ya jioni; Kisangani, saa 12:26 ya jioni; Kolwezi, saa 12:20 ya jioni; Likasi, saa 12:15 ya jioni; Lubumbashi, saa 12:11 ya jioni; Bukavu saa 12:10 ya jioni; Bunia, saa 12:05 ya jioni. Katika sehemu nyingine ya eneo letu, saa ya kutua kwa jua inaweza kuhesabiwa kwa kuongeza dakika 5 kwenye saa inayojulikana ya kutua kwa jua katika mji mkuu, ikiwa mnapatikana kwenye kilometa 140 kuelekea mangaribi kutoka mji huo. Kwa kuwa hakuna mikutano mingine itakayofanywa isipokuwa ile ya utumishi wa shambani siku hiyo, marekebisho yanayofaa yanapaswa kufanywa ili Funzo la Mnara wa Mlinzi liendeshwe wakati mwingine. Waangalizi wa mzunguko watahitaji kurekebisha programu yao ya mikutano ya juma hilo kulingana na hali za mahali. Ingawa ni vizuri kila kutaniko lifanye mwadhimisho walo lenyewe wa Ukumbusho, huenda hilo lisiwezekane sikuzote. Mahali ambapo makutaniko mengi hutumia kwa kawaida Jumba la Ufalme lilelile, labda kutaniko moja au zaidi yanaweza kupata kibali cha kutumia jengo lingine jioni hiyo. Mahali ambapo inawezekana, tungependekeza afadhali kuwe na dakika 40 kati ya programu mbalimbali kusudi wote wafaidike kikamili na tukio hilo. Baraza la wazee linapaswa kuamua ni mipango gani inayoweza kuwa bora zaidi mahali pao.