Matangazo
◼ Toleo la vichapo la Machi: Endeleeni Kukesha! Aprili na Mei: Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele. Juni: Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu. Ikiwa watu wanasema kwamba hawana watoto, uwatolee kitabu Furaha ya Familia au kitabu Ujuzi. Fanya jitihada ya kuanzisha mafunzo ya Biblia.
◼ Makutaniko yanapaswa kutolea wahubiri magazeti Mnara wa Mlinzi na Amkeni! mara tu yanapopokewa. Hilo litaruhusu wahubiri kufahamiana na mambo yaliyomo kabla ya kutolea watu magazeti katika utumishi wa shambani. Huduma Yetu ya Ufalme pia inapaswa kutolewa wahubiri mara tu inapofika. Inaweza kugawanywa kwenye Funzo la Kitabu la Kutaniko.
◼ Waandishi wa makutaniko wanapaswa kuendelea kuwa na kiasi cha kutosha cha fomu Demande d’admission au service de pionnier permanent (S-205) na Demande d’admission au service de pionnier auxiliaire (S-205b). Hizo zinaweza kuombwa kwenye fomu Demande de publications (S-14). Iweni na kiasi cha kutosha kwa ajili ya mwaka mmoja.
◼ Ukumbusho utaadhimishwa Siku ya Nne, Machi 24, 2005. Ikiwa kutaniko lenu lina mikutano Siku ya Nne, mikutano hiyo inapaswa kufanywa siku nyingine ya juma ikiwa jumba la Ufalme liko huru. Ikiwa hilo haliwezekani na ikiwa Mkutano wa Utumishi wenu unahusika, sehemu ambazo zinahusu kutaniko lenu zinaweza kuingizwa katika Mkutano mwingine wa Utumishi.
◼ Hesabu fulani ya wahubiri wamepigia simu ofisi ya tawi kuhusu rekodi fulani za nyimbo ya Ufalme zinazoimbwa katika mtindo wa muziki wa kawaida ambazo zinasambazwa kati ya Mashahidi wa Yehova. Wanauliza ikiwa rekodi hizo zinakubaliwa na tengenezo. Tunatambua rekodi hizo na tunapenda kuwajulisha kwamba hatuzikubali. Tafadhali msisambaze au kutumiana rekodi hizo kupitia Internet. Tunatumaini kuwa habari hii itafanya mambo yawe wazi.
◼ Mnara wa Mlinzi wa Aprili 1, 2005 utakuwa na kichwa ‘Sayansi na Biblia—Je, Hupingana?’ Kwa sababu ya umaana wa ulizo hilo, kila kutaniko litapokea asilimia 15 ya ziada kuhusu toleo hili.