Matangazo
◼ Toleo la vitabu la Mei: Toleeni watu magazeti mkikazia mojawapo, Mnara wa Mlinzi au Amkeni!. Mnaporudilia watu waliopendezwa, kutia ndani wale wanaohuzuria Ukumbusho na/au matukio mengine ya kitheokrasi, lakini ambao hawashirikiani kwa bidii na kutaniko, fanyeni jitihada ya kuwaachia kitabu kipya Biblia Inafundisha Nini Hasa? Mradi unapaswa kuwa kuanzisha funzo la Biblia katika kitabu hicho. Juni: Toleeni watu kitabu Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu. Ikiwa watu wanasema kwamba hawana watoto, watoleeni kitabu Furaha ya Familia. Julai na Agosti: Tumia broshua yoyote ya kurasa 32 kati ya zifuatazo: Endeleeni Kukesha!; Jambo Gani Hutufikia Tunapokufa?; Je! Kweli Mungu Anatujali?; Je! Uamini Utatu?; Jina la Mungu Litakaloendelea Milele; Kuishi Milele Duniani Katika Furaha!; Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa; Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai?—Wewe Waweza Kulipataje?; Roho za Wafu—Je! Zaweza Kukusaidia au Kukuumiza? Je! Ziko Kweli?; Serikali Itakayoleta Paradiso; na “Tazama! Mimi Ninafanya Vitu Vyote Kuwa Vipya.”
◼ Kwa kuwa mwezi wa Julai una miisho-juma mitano, itakuwa mwezi bora wa kutumika kama painia msaidizi.
◼ Mwangalizi-msimamizi, au mtu mwingine atakayechaguliwa naye, anapaswa kufanya uchunguzi wa akaunti za kutaniko mnamo Juni 1 au mapema zaidi iwezekanavyo baada ya tarehe hiyo. Ikiwa kuna feza zinazolindwa, kama vile feza kwa ajili ya utengenezaji wa kawaida wa jumba au ujenzi, mipango itachukuliwa pia ili kufanya uchunguzi wa akaunti hiyo. Jambo hilo litakapokuwa limefanywa, tangazieni kutaniko baada ya kusoma ripoti ya akaunti ya kawaida.
◼ Waandishi wa makutaniko wanapaswa kuwa na kiasi cha kutosha cha fomu Demande d’admission au service de pionnier permanent (S-205) na Demande d’admission au service de pionnier auxiliaire (S-205b). Hizo zinaweza kuombwa kwenye fomu Demande de publications (S-14). Iweni na fomu za kutosha ambazo mnaweza kutumia kwa mwaka mmoja. Mbele ya kutuma fomu za mapainia wa kawaida kwenye ofisi ya tawi, chunguzeni vizuri ili kuhakikisha kwamba maulizo yote yanayopatikana kwenye fomu yamejibiwa.