Upendo—Siri ya Kupata Matokeo Mazuri Katika Mahubiri
1 “Njooni kwangu, . . . nami nitawaburudisha ninyi.” (Mt. 11:28) Maneno hayo yenye kupendeza yanaonyesha upendo mwingi wa Yesu kwa watu. Tukiwa watumishi Wakristo, tunapenda kumwiga Yesu kwa kuonyesha upendo wetu kwa watu wenye kuchoshwa na ulimwengu usio na upendo. Namna gani tunaweza kuonyesha upendo huo kwa watu tunapowahubiria habari njema?
2 Katika Maneno: Kwa kuwa Yesu alipenda watu, yeye alichochewa kutumia kila nafasi iliyopatikana ili kuhubiri habari njema. (Yoh. 4:7-14) Upendo utatusaidia tusisite kuhubiria watu hata ikiwa hatukupanga kufanya hivyo. Binti mmoja wa miaka sita alihubiria mwanamke mmoja aliyekaa pembeni yake kwenye hospitali wakiwa wenye kungojea kuonana na mganga. Ni jambo gani lililomchochea kufanya hivyo? Alieleza hivi: “Mwanamke huyo alionekana kuwa mtu aliyekuwa na lazima ya kujua mambo yanayomhusu Yehova.”
3 Kwa uso wenye furaha ya kweli na sauti ya kirafiki, tunaweza kuonyesha watu kwamba tunapendezwa nao. Kusikiliza kwa uangalifu maelezo yao, kujua mambo yenye kuwahangaisha, na kupendezwa nao kwelikweli, kunaonyesha vilevile upendo wetu kwao. (Met. 15:23) Ili kumwiga Yesu, tutakazia ujumbe wa Ufalme wenye kutia moyo na pia huruma na upendo wa Yehova kwa watu.—Mt. 24:14; Luka 4:18.
4 Katika Matendo: Yesu alitenda bila kukawia ili kusaidia wale waliokuwa katika uhitaji wa kimwili. (Mt. 15:32) Sisi pia tunaweza kufanyia watu mambo yenye kuonyesha upendo na fazili tunapokuwa katika kazi ya kuhubiri. Dada mmoja aliona mwanamke fulani akijikaza kuelewa maneno ya lazima sana yaliyosemwa na mtu aliyemwita kwenye telefone. Dada akamsaidia kwa kumufasiria maneno hayo. Tendo hilo la upendo lilifungua njia ya mazungumzo ya Biblia na kusaidia mwanamke huyo akubali funzo la Biblia. Katika hali nyingine, ndugu mmoja aliyerudilia mtu katika mahubiri alimkuta akiwa mwenye kuuzika, akijaribu kuondoa kiti kizito kilichokwama mlangoni. Ndugu huyo, alipokwisha kumsaidia kukiondoa, alikaa sasa kwenye kiti hicho, akaanzisha funzo la Biblia na mtu huyo aliyeonyesha shukrani.
5 Tunapohubiri, tunaonyesha upendo wetu kwa Mungu na kwa jirani zetu. (Mt. 22:36-40) Kuonyesha hivyo upendo kwa maneno na matendo kutasaidia wale wenye mioyo minyofu kuelewa kwamba tuna ukweli.