Matangazo
◼ Toleo la vitabu la mwezi wa 5: Toleeni watu magazeti Mnara wa Mlinzi na Amkeni!. Mnaporudilia watu waliopendezwa, kutia ndani wale wanaohuzuria Ukumbusho na/au matukio mengine ya kitheokrasi, lakini hawajiungi sana na kutaniko, mjikaze kuwatolea kitabu Biblia Inafundisha. Mwezi wa 6: Toleeni watu kitabu Muumba au Furaha ya Familia. Mwezi wa 7 na wa 8: Toleeni watu broshua yoyote ya kurasa 32 kati ya zifuatazo: Endeleeni Kukesha!; Jambo Gani Hutufikia Tunapokufa?; Je, Kweli Mungu Anatujali?; Je, Uamini Utatu?; Je, Ulimwengu Usio na Vita Utakuwako Wakati Wowote?; Je, Umeipata Barabara Inayoongoza Kwenye Uhai? Jina la Mungu Litakaloendelea Milele; Jinsi ya Kupata Maisha Yenye Kuridhisha; Kitabu kwa Ajili ya Watu Wote; Kuishi Milele Duniani Katika Furaha!; Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa; Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai?—Wewe Waweza Kulipataje?; Nos Problèmes — Qui nous aidera à les résoudre ?; Roho za Wafu—Je, Zaweza Kukusaidia au Kukuumiza? Je! Ziko Kweli?; Serikali Itakayoleta Paradiso; na “Tazama! Mimi Ninafanya Vitu Vyote Kuwa Vipya.”
◼ Kadi mpya ya kiganga DPA (Instructions médicales/Désignation d’une personne de confiance) ilipotokea katika mwaka wa 2006, tulipata hivyo chombo kipya ambacho kinajulisha mambo tunayotaka kuhusu matunzo. Huduma Yetu ya Ufalme ya mwezi wa 11, 2006 ina nyongeza inayosaidia wengi kati ya ndugu zetu wajue jinsi ya kujaza kadi zao za kiganga DPA. Mkijua hivyo, tunawaomba viongozi wote wa funzo la kitabu wawe tayari kusaidia kila mhubiri mwenye kubatizwa katika kikundi chao.
◼ Ikiwa mzee fulani atahuzuria mkusanyiko wa mahali pengine na wala si ule wa mahali ambapo kutaniko lao linaalikwa, tafazali, anaweza kutujulisha mbele ya wakati kupitia barua. Inawezekana kwamba aombwe kutoa hotuba katika programu, zaidi sana ikiwa kuna wasemaji wachache kwenye mkusanyiko huo. Hata hivyo, yeye mwenyewe atalipa feza za usafirishaji na garama zingine zozote.
◼ Katika juma la Mkusanyiko wa Pekee wa Siku Moja, mwangalizi wa mzunguko atachagua kutaniko moja ambalo atatembelea. Siku ambazo si za mkusanyiko, mkutano kwa ajili ya mahubiri utapangwa kufanywa kila siku. Kutaniko linalotembelewa litapanga dakika 45 kwa ajili ya funzo la kitabu Siku ya Pili magaribi, na kisha funzo hilo mwangalizi wa mzunguko au mwangalizi wa wilaya, ikiwa ni yeye aliye msemaji mgeni, atatoa hotuba ya utumishi ya dakika 45. Kutaniko litafanya mkutano wa Shule ya Huduma ya Kitheokrasi na Mkutano wa Utumishi kama kawaida, magaribi ya siku ingine katika juma hilo. Waangalizi wasafiri wanaweza kupewa vipindi katika mikutano hiyo.