Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 9/07 uku. 3
  • Kisanduku Cha Maulizo

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Kisanduku Cha Maulizo
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2007
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Unapata Chakula “kwa Wakati Unaofaa”?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Video na Habari Zingine za Sehemu ya 2
    Furahia Maisha Milele!—Ujifunze Biblia kwa Njia ya Mazungumuzo
  • Ditaba Tsa Sekopa sa 1
    Furahia Maisha Milele!—Ujifunze Biblia kwa Njia ya Mazungumuzo
  • Matumizi ya Internet—Fanyeni angalisho kwa hatari!
    Huduma Yetu ya Ufalme—1999
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2007
km 9/07 uku. 3

Kisanduku Cha Maulizo

◼ Je, “mtumwa mwaminifu na mwenye busara” anakubali kuwe vikundi vya Mashahidi wanaofanya mipango yao wenyewe ya kukutana ili kufanya utafiti (recherches) katika Maandiko au kubishanabishana kuhusu Maandiko?—Mt. 24:45, 47.

Hapana, haruhusu hivyo. Lakini, katika sehemu mbalimbali za ulimwengu, washiriki wachache wa tengenezo letu wamefanya vikundi ili kutafuta mambo yanayohusiana na habari za Biblia. Wengine wamefanya kikundi cha kujifunza luga ya Kiebrania na ya Kigiriki iliyotumiwa katika Biblia ili kuchunguza ikiwa Tafsiri ya Ulimwengu Mpya haina makosa. Wengine wanatafuta-tafuta habari kuhusu mambo ya sayansi yanayohusiana na Biblia. Wameunda vituo fulani kwenye Internet ili kupashana habari na kuzungumzia mawazo yao. Wamepanga pia mikutano na kuchapisha vitabu ili kujulisha habari walizopata na kuongezea kwa zile tunazotolewa kwenye mikutano yetu ya Kikristo na kupitia vitabu vyetu.

Duniani pote, watu wa Yehova wanapata mafundisho mengi ya kiroho na vitia-moyo kwenye mikutano ya kutaniko, kwenye mikusanyiko, na pia kupitia vitabu vya tengenezo la Yehova. Kupitia roho yake takatifu na Neno lake la kweli, Yehova anatoa yale yanayohitajiwa ili watu wake wote ‘waunganishwe vema katika akili ileile na katika njia ileile’ na waendelee “kuimarishwa katika imani.” (1 Kor. 1:10; Kol. 2:6, 7) Kwa kweli, tunamshukuru sana Yehova kwa ajili ya mipango ya kiroho katika siku hizi za mwisho. Kwa hiyo, “mtumwa mwaminifu na mwenye busara” haruhusu kitabu chochote, mikutano yoyote, ao vituo vya Internet ambavyo havitolewe ao kupangwa naye—Mt. 24:45-47.

Tunashukuru watu wanaotumia uwezo wao wa kufikiri ili kutegemeza habari njema. Lakini, jambo lolote ambalo mtu anafanya halipaswi kutukengeusha tuache yale ambayo Yesu anatimiza kupitia kutaniko lake la duniani leo. Katika karne ya kwanza, mtume Paulo alionya kuhusu kujihusisha katika mambo yenye kuchokesha na yenye kupoteza wakati, kama vile “mambo ya kutafuta-tafuta ukoo, ambayo mwisho wake si kitu, lakini ambayo hutokeza maswali ya utafiti badala ya kugawa kitu chochote kutoka kwa Mungu kuhusiana na imani.” (1 Tim. 1:3-7) Wakristo wote wanapaswa kujikaza ili ‘kuepuka maswali ya upumbavu na kutafuta-tafuta ukoo na mizozo na mapigano juu ya sheria, kwa maana hayo hayana faida na ni ya ubatili.’—Tito 3:9.

Tunaomba wale wanaotaka kujifunza Biblia zaidi na kutafuta habari katika vitabu, wachunguze vitabu Étude perspicace des Écritures, “Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa,” na vitabu vyetu vingine kama vile vitabu vinavyozungumzia unabii ulio katika kitabu cha Biblia cha Danieli, Isaya na Ufunuo. Vitabu hivyo vinatoa habari nyingi zinazotusaidia kujifunza Biblia na kufikiri sana juu ya habari tunayojifunza, ili kwamba tuweze ‘kujazwa ujuzi sahihi wa mapenzi ya Mungu katika hekima yote ya utambuzi wa kiroho, ili kutembea kwa kumstahili Yehova kwa kusudi la kumpendeza Yeye kikamili tunapoendelea kuzaa matunda katika kila kazi njema na kuongezeka katika ujuzi sahihi wa Mungu.’—Kol. 1:9, 10.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine