Kujikumbusha Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
Maulizo yanayofuata yatatumiwa kwenye Shule ya Huduma ya Kitheokrasi katika juma tokea tarehe 25, mwezi wa 10, 2010. Kwa muda wa dakika 20 mwangalizi wa shule ataongoza kujikumbusha kunakotegemea habari zilizozungumziwa tokea tarehe 6 mwezi wa 9 mpaka tarehe 25 mwezi wa 10, 2010.
1. Tunaweza kujifunza nini kwa kuchunguza maisha ya Mfalme Azaria (Uzia)? (2 Fal. 15:1-6) [w91 7/15 uku. 29-30]
2. Kwa kuwa inasemwa kwamba Yothamu alitawala tu miaka 16, kwa nini andiko la 2 Wafalme 15:30 linazungumzia “mwaka wa 20” wa utawala wake? (2 Nya. 27:7, 8) [it-2-F uku. 1226 fu. 6]
3. “Wasamaria” wanaozungumziwa kwenye andiko la 2 Wafalme 17:29, walikuwa nani? [it-2-F uku. 878 fu. 8]
4. Kwa nini inasemwa kwamba Yehova ‘analifanya’ kusudi lake? (2 Fal. 19:25) [w99 8/15 uku. 14 fu. 3]
5. Namna gani andiko la 2 Wafalme 25:8, 25, 26 linaeleza kwa usahihi mwanzo wa utimizo wa miaka 70; miaka ambayo Yerusalemu ingebaki ukiwa? [it-1-F uku. 403 fu. 5–uku. 404 fu. 1; uku. 471 fu. 1]
6. Kwa nini andiko la 1 Samweli 16:10, 11 linamtaja Daudi kuwa mwana wa nane wa Yese, wakati ambapo andiko la Ezra linamtaja kuwa mwana wa saba? (1 Nya. 2:15) [w02 9/15 uku. 31]
7. Namna gani tunaweza kufuata mfano wa Wagileadi wa zamani? (1 Nya. 5:10, 18-22) [w05 10/1 uku. 9 fu. 7]
8. Tunaweza kujifunza nini kutokana na watunza-milango Walawi? (1 Nya. 9:26, 27) [w05 10/1 uku. 9 fu. 8]
9. Katika Israeli la zamani, kuimba kulipewa nafasi gani? (1 Nya. 9:33) [it-2-F uku. 359 fu. 8]
10. Ni jambo gani lisilofaa ambalo Daudi alitenda kulingana na andiko la 1 Mambo ya Nyakati 13:11? [w05 10/1 uku. 11]