Matangazo
◼ Vichapo vya kutolea watu katika mwezi wa 12: Tutatolea watu kitabu Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi. Ikiwa musikilizaji ana watoto, mumutolee kitabu Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu ao Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia. Mwezi wa 1: Kitabu Biblia Inafundisha Nini Hasa? Mujikaze sana ili kuanzisha mafunzo ya Biblia munapohubiria mutu. Ikiwa mutu huyo amekwisha kupata kitabu hicho na anakataa kujifunza Biblia, muhubiri anaweza kumutolea gazeti fulani la zamani ao broshua yoyote inayozungumuzia mambo yenye kumupendeza.
◼ Katika mwaka wa 2013, Ukumbusho utafanywa Siku ya Pili, tarehe 26 mwezi wa 3.
◼ Ikiwa mwandishi wa kutaniko anapokea fomu Tafadhali Fuatia Upendezi (S-43) kutoka kutaniko lingine lililo katika muji wao ao kijiji, anapaswa kujikaza sana ili kujua jina la kutaniko linalohubiri eneo ambamo mutu mwenye kupendezwa anaishi. Ataandika jina la kutaniko linalohusika kwenye fomu S-43 mbele ya kuitumia kutaniko hilo. Akifanya yote awezayo ili kujua jina la kutaniko linalohusika lakini haiwezekani, ndipo anaweza kuituma kwenye ofisi ya tawi.