Matangazo
◼ Vichapo vya kutolea watu katika mwezi wa 1: Tutatolea watu kitabu Biblia Inafundisha Nini Hasa? Mujikaze sana kuanzisha mafunzo ya Biblia munapohubiria mutu. Ikiwa mutu amekwisha kupata kitabu hicho na anakataa kujifunza Biblia, muhubiri anaweza kumutolea gazeti fulani la zamani ao broshua yoyote inayozungumuzia mambo yenye kumupendeza.
◼ Mwangalizi wa eneo la dunia atatembelea tawi letu tarehe 8-19/04/2012.
◼ Programu ya kumutolea Yehova majengo ya Beteli itakuwa tarehe 26-27/05/2012. Kwa kuwa hakuna nafasi za kutosha kwenye Beteli yetu, itaomba kuwa na mwaliko wa pekee ili kuhuzuria. Wale watakaoalikwa watajulishwa mbele ya wakati.
◼ Kuanzia mwezi wa 2, mwangalizi wa muzunguko atatoa hotuba mupya yenye kichwa “Je, Unamutumainia Kabisa Yehova?”
◼ Kuanzia tarehe 1/02/2012, toleo la watu wote la Mnara wa Mlinzi litakuwa na habari yenye kichwa “Masomo Yangu ya Biblia.” Habari hiyo imetayarishwa ili wazazi waitumie wanapofundisha watoto wenye miaka mitatu ao chini ya miaka hiyo. Mara kwa mara habari hiyo itatolewa mahali pa habari zenye kichwa “Wafundishe Watoto Wako” na “Kwa Ajili ya Vijana Wetu.”