Kujikumbusha Masomo ya Huduma ya Kiteokrasi
Maulizo yanayofuata yatatumiwa kwenye Masomo ya Huduma ya Kiteokrasi katika juma la tarehe 26 Mwezi wa 10, 2015.
Namna gani habari yenye kupatikana katika 2 Wafalme 13:18, 19 inaonyesha faida ya kuwa na bidii katika kumutumikia Mungu kwa moyo wote? [Juma la tarehe 7, Mwezi wa 9, w10 15/4 uku. 26 fu. 11]
Ni nani alikuwa Mufalme katika Israeli wakati Yona alikuwa nabii, na tunaweza kufurahia jambo gani juu ya kazi ya Yona kama vile andiko la 2 Wafalme 14:23-25 linaonyesha? [Juma la tarehe 7, Mwezi wa 9, w09 1/1 uku. 25 fu. 4]
Namna gani Ahazi alionyesha kwamba hakuamini maneno yenye Mungu alimuambia kupitia nabii Isaya, na tunapaswa kujiuliza ulizo gani wakati tunafanya maamuzi makubwa? (2 Fal. 16:7) [Juma la tarehe 14, Mwezi wa 9, w13 15/11 uku. 17 fu. 5]
Wapinzani wa watu wa Mungu wa leo wanatumia njia gani yenye Rabshake alitumia pia, na ni sifa gani inaweza kutusaidia kupinga mawazo mabaya ya wapinzani? (2 Fal. 18:22, 25) [Juma la tarehe 14, Mwezi wa 9, w10 15/7 uku. 13 fu. 3-4]
Yosia alikuwa munyenyevu. Mufano wake unatusaidia namna gani kufurahia usomaji wetu wa Biblia na funzo letu la pekee? (2 Fal. 22:19, 20) [Juma la tarehe 21, Mwezi wa 9, w00 1/3 uku. 30 fu. 2]
Namna gani mambo yenye yalivumbuliwa na wachunguzi wa vitu vya zamani yanahakikisha kwamba wafalme wawili wenye kutajwa katika andiko la 2 Wafalme 25:27-30 waliishi kabisa? [Juma la tarehe 28, Mwezi wa 9, w12 1/6 uku. 5 fu. 2-3]
Yabesi alimuomba Yehova mambo gani matatu, na jambo hilo linatufundisha nini juu ya sala? (1 Nya. 4:9, 10) [Juma la tarehe 5, Mwezi wa 10, w10 1/10 uku. 23]
Namna gani matokeo ya vita yenye kutajwa katika andiko la 1 Mambo ya Nyakati 5:18-22 inatutia nguvu ili tuendelee kupigana vita ya kiroho pasipo woga? [Juma la tarehe 12, Mwezi wa 10, w05 1/10 uku. 9 fu. 7]
Sababu gani Daudi alielewa na kuheshimia kanuni ya Sheria ya Yehova juu ya kuona damu kuwa kitu kitakatifu, na mufano wa Daudi unatuchochea kufanya nini? (1 Nya. 11:17-19) [Juma la tarehe 19, Mwezi wa 10, w12 15/11 uku. 6-7 fu. 12-14]
Daudi alizarau kufanya jambo gani wakati alijaribu kuleta sanduku la agano katika muji wa Yerusalemu, na jambo hilo linatufundisha nini? (1 Nya. 15:13) [Juma la tarehe 26, Mwezi wa 10, w03 1/5 uku. 10-11 fu. 11-13]