Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 10/15 uku. 3
  • Kujikumbusha Masomo ya Huduma ya Kiteokrasi

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Kujikumbusha Masomo ya Huduma ya Kiteokrasi
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2015
Huduma Yetu ya Ufalme—2015
km 10/15 uku. 3

Kujikumbusha Masomo ya Huduma ya Kiteokrasi

Maulizo yanayofuata yatatumiwa kwenye Masomo ya Huduma ya Kiteokrasi katika juma la tarehe 26 Mwezi wa 10, 2015.

  1. Namna gani habari yenye kupatikana katika 2 Wafalme 13:​18, 19 inaonyesha faida ya kuwa na bidii katika kumutumikia Mungu kwa moyo wote? [Juma la tarehe 7, Mwezi wa 9, w10 15/4 uku. 26 fu. 11]

  2. Ni nani alikuwa Mufalme katika Israeli wakati Yona alikuwa nabii, na tunaweza kufurahia jambo gani juu ya kazi ya Yona kama vile andiko la 2 Wafalme 14:23-25 linaonyesha? [Juma la tarehe 7, Mwezi wa 9, w09 1/1 uku. 25 fu. 4]

  3. Namna gani Ahazi alionyesha kwamba hakuamini maneno yenye Mungu alimuambia kupitia nabii Isaya, na tunapaswa kujiuliza ulizo gani wakati tunafanya maamuzi makubwa? (2 Fal. 16:7) [Juma la tarehe 14, Mwezi wa 9, w13 15/11 uku. 17 fu. 5]

  4. Wapinzani wa watu wa Mungu wa leo wanatumia njia gani yenye Rabshake alitumia pia, na ni sifa gani inaweza kutusaidia kupinga mawazo mabaya ya wapinzani? (2 Fal. 18:22, 25) [Juma la tarehe 14, Mwezi wa 9, w10 15/7 uku. 13 fu. 3-4]

  5. Yosia alikuwa munyenyevu. Mufano wake unatusaidia namna gani kufurahia usomaji wetu wa Biblia na funzo letu la pekee? (2 Fal. 22:19, 20) [Juma la tarehe 21, Mwezi wa 9, w00 1/3 uku. 30 fu. 2]

  6. Namna gani mambo yenye yalivumbuliwa na wachunguzi wa vitu vya zamani yanahakikisha kwamba wafalme wawili wenye kutajwa katika andiko la 2 Wafalme 25:27-30 waliishi kabisa? [Juma la tarehe 28, Mwezi wa 9, w12 1/6 uku. 5 fu. 2-3]

  7. Yabesi alimuomba Yehova mambo gani matatu, na jambo hilo linatufundisha nini juu ya sala? (1 Nya. 4:9, 10) [Juma la tarehe 5, Mwezi wa 10, w10 1/10 uku. 23]

  8. Namna gani matokeo ya vita yenye kutajwa katika andiko la 1 Mambo ya Nyakati 5:18-22 inatutia nguvu ili tuendelee kupigana vita ya kiroho pasipo woga? [Juma la tarehe 12, Mwezi wa 10, w05 1/10 uku. 9 fu. 7]

  9. Sababu gani Daudi alielewa na kuheshimia kanuni ya Sheria ya Yehova juu ya kuona damu kuwa kitu kitakatifu, na mufano wa Daudi unatuchochea kufanya nini? (1 Nya. 11:17-19) [Juma la tarehe 19, Mwezi wa 10, w12 15/11 uku. 6-7 fu. 12-14]

  10. Daudi alizarau kufanya jambo gani wakati alijaribu kuleta sanduku la agano katika muji wa Yerusalemu, na jambo hilo linatufundisha nini? (1 Nya. 15:13) [Juma la tarehe 26, Mwezi wa 10, w03 1/5 uku. 10-11 fu. 11-13]

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2026)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine