Namna Tunaweza Kugusa Mioyo ya Watu Wenye Tunafundisha
1. Mafundisho ya Yesu yalikuwa na matokeo gani juu ya wasikilizaji wake?
1 Yesu Kristo aligusa mioyo ya wasikilizaji wake. Siku moja, mioyo ya wanafunzi wake ‘iliwaka’ kisha yeye kuwafasiria waziwazi Maandiko. (Lu. 24:32) Kwa kuwa utii wa kweli unatoka moyoni, namna gani tunaweza kugusa mioyo ya watu wenye tunafundisha ili wafanye haraka mabadiliko katika maisha yao?—Rom. 6:17.
2. Namna gani utambuzi unaweza kutusaidia kugusa mioyo ya wasikilizaji?
2 Tutumie Utambuzi: Mara nyingi, kuwafundisha watu mambo mazuri na mabaya hakutoshe ili kuwachochea kutenda. Kwa kweli, kusomea mutu maandiko mengi yenye kuhukumu mambo yenye anaamini kunaweza kufanya asipendezwe na ujumbe wetu. Ili kugusa moyo wa mutu, tunapaswa kwanza kutambua sababu gani anaamini na kutenda mambo fulani. Kwa ufundi, tumia maulizo yenye kufaa ili akufunulie moyo wake. (Met. 20:5) Jambo hilo linaweza kukusaidia kuchagua habari fulani katika Neno la Mungu yenye inaweza kugusa moyo wake. Tena, tunapaswa kumuhangaikia na kuwa wavumilivu. (Met. 25:15) Usisahau kwamba watu wanafanya maendeleo ya kiroho kulingana na hali yao. Endelea kuwa muvumilivu mupaka roho takatifu ya Yehova ibadilishe mawazo na matendo yao.—Mk. 4:26-29.
3. Namna gani tunaweza kusaidia wanafunzi wetu wa Biblia wakomalishe sifa nzuri?
3 Tuwasaidie Kukomalisha Sifa Nzuri: Biblia inaonyesha kwamba wema na upendo wa Yehova vinaweza kusaidia wanafunzi wetu wa Biblia wakomalishe sifa nzuri. Tunaweza kutumia maandiko kama vile Zaburi 139:1-4 ao Luka 12:6, 7 ili kuonyesha kadiri gani Mungu anahangaikia kabisa kila mutu. Wakati wataanza kufurahia fazili za bure za Yehova, upendo na ushikamanifu wao kwa Mungu utaanza kukomaa. (Rom. 5:6-8; 1 Yoh. 4:19) Tena, wakati watatambua kwamba mwenendo wao unaweza kumufurahisha ao kumuchukiza Yehova, pengine watachochewa kutenda mambo yenye kumufurahisha na yenye kumuletea sifa.—Zab. 78:40, 41; Met. 23:15.
4. Namna gani tunaweza kuheshimia uhuru wa kukamata maamuzi wa wanafunzi wetu wa Biblia?
4 Yehova halazimishe mutu kutii amri zake. Lakini anaonyesha watu faida ya kutumikisha mashauri yake. (Isa. 48:17, 18) Tunamuiga Yehova wakati tunafundisha watu ili kuwasaidia wafikie kukamata wenyewe maamuzi. Wakati watu wanatambua wenyewe kwamba ni lazima wafanye mabadiliko katika maisha yao, wanaendelea kuwa waaminifu kwa muda murefu. (Rom. 12:2) Maamuzi hayo, yatawasaidia wamukaribie zaidi ‘muchunguzaji wa mioyo,’ nikusema, Yehova.—Met. 17:3.