Kujikumbusha Masomo ya Huduma ya Kiteokrasi
Maulizo yenye kufuata yatatumiwa kwenye Masomo ya Huduma ya Kiteokrasi katika juma la tarehe 28 Mwezi wa 12, 2015. Tarehe yenye kila ulizo litazungumuziwa inaonyeshwa pia ili kusaidia watu kutafuta majibu katika vichapo wakati wanatayarisha masomo ya huduma ya kila juma.
Je, Daudi aliwatendea kama nyama watu wenye alikamata katika vita, kama vile watu fulani wanawaza andiko la 1 Mambo ya Nyakati 20:3 linasema? [Juma la tarehe 2 Mwezi wa 11, w05 15/2 uku. 27]]
Ni nini ilimuchochea Daudi atoe vitu vingi, na ni nini itatusaidia kufanya hivyo? (1 Nya. 22:5) [Juma la tarehe 9 Mwezi wa 11, w05 1/10 uku. 11 fu. 7]
Daudi alimaanisha nini wakati alimuambia Sulemani: ‘umujue Mungu wa baba yako’? (1 Nya. 28:9) [Juma la tarehe 16 Mwezi wa 11, w10 1/11 uku. 30 fu. 3, 7]
Jambo lenye Mufalme Sulemani aliomba kwenye andiko la 2 Mambo ya Nyakati 1:10 lilionyesha kama alikuwa mutu wa namna gani, na inatufundisha nini juu ya mambo yenye tunatia katika sala zetu kwa Yehova? (2 Nya. 1:11, 12) [Juma la tarehe 23 Mwezi wa 11, w05 1/12 uku. 19 fu. 6]]
Kulingana na andiko la 2 Mambo ya Nyakati 6:29, 30, Yehova ana uwezo gani wa pekee, na sababu gani tunapaswa kumufunulia moyo wetu katika sala? (Zab. 55:22) [Juma la tarehe 30 Mwezi wa 11, w10 1/12 uku. 11 fu. 7]
Sababu gani Mufalme Asa alisali ili ashinde askari wengi sana, na tunapaswa kuwa hakika na jambo gani katika vita yetu ya kiroho? (2 Nya. 14:11) [Juma la tarehe 7 Mwezi wa 12, w12 15/8 uku. 8 fu. 6–uku. 9 fu. 1]
Namna Yehova alimutendea Mufalme Yehoshafati wakati alimukosea inatufundisha nini juu ya upendo wa Mungu, na jambo hilo linaweza kutusaidia tuone wengine namna gani? (2 Nya. 19:3) [Juma la tarehe 14 Mwezi wa 12, w03 1/7 uku. 17 fu. 13; cl uku. 245 fu. 12]
Sababu gani tunapaswa kubakia ‘mahali petu’ na ‘kusimama tuli [bila kutikisika]’ katika siku zetu, na namna gani tunaweza kufanya hivyo? (2 Nya. 20:17) [Juma la tarehe 21 Mwezi wa 12, w05 1/12 uku. 21 fu. 2; w03 1/6 uku. 21 fu. 15-16]]
Ni jambo gani la kufikiria kwa uzito tunapata katika andiko la 2 Mambo ya Nyakati 21:20 kuhusu kifo cha Yehoramu? [Juma la tarehe 21 Mwezi wa 12, w98 15/11 uku. 32 fu. 4]]
Kulingana na andiko la 2 Mambo ya Nyakati 26:5, ni nani alichochea kijana Uzia kufanya mambo mazuri, na namna gani vijana wa leo wanaweza kuchochewa na Wakristo wenye kukomaa kiroho katika kutaniko? [Juma la tarehe 28 Mwezi wa 12, w07 15/12 uku. 10 fu. 2, 4]]