MAISHA YA MUKRISTO
Njia Tatu za Kumutegemea Yehova
Daudi alishinda Goliati juu alimutegemea Yehova. (1Sa 17:45) Yehova anapenda kuonyesha nguvu zake kwa ajili ya watumishi wake wote. (2Ny 16:9) Namna gani tunaweza kutegemea musaada wenye Yehova anatupatia kuliko kutegemea uzoefu na uwezo wetu? Tuone njia tatu:
Sali kila mara. Usisali tu juu ya kuomba musamaha wakati ulifanya kosa fulani, lakini usali pia juu ya kuomba nguvu ya kupambana na jaribu. (Mt 6:12, 13) Usisali tu juu ya kuomba Yehova abariki maamuzi yenye ulishakamata, lakini umuombe pia akupatie muongozo na hekima mbele ya kukamata maamuzi.—Yak 1:5
Ukuwe na kawaida ya kusoma na kujifunza Biblia. Soma Biblia kila siku. (Zb 1:2) Fikiri sana juu ya mifano yenye kuwa mu Biblia na utumikishe mambo yenye unajifunza. (Yak 1:23-25) Ujitayarishe kwa ajili ya mahubiri kuliko tu kutegemea mambo yenye umezoea kufanya. Ukuwe natayarisha mikutano mbele ya wakati ili ufaidike nayo
Fuata muongozo wa tengenezo ya Yehova. Ujikaze kukuwa najua muongozo wa sasa wa tengenezo na kuufuata palepale. (Hes 9:17) Sikiliza wazee wakati wanatoa mashauri na maagizo.—Ebr 13:17
MUANGALIE VIDEO HAKUNA SABABU YA KUOGOPA UPINZANI, KISHA MUJIBIE HII MAULIZO:
• Ni mambo gani yenye ndugu na dada waliogopa?
• Nini njo iliwasaidia wapiganishe ile woga?