Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w25 Mwezi wa 8 uku. 31
  • Maulizo ya Wasomaji Wetu

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Maulizo ya Wasomaji Wetu
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2025
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Ufalme wa Mungu Unaondoa Maadui Wake
    Ufalme wa Mungu Unatawala!
  • Tunajua Nini Juu ya Namna Yehova Atahukumu Watu?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2024
  • Armagedoni Ni Habari Njema!
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2019
  • Endelea Kuwa Muaminifu Wakati wa “Taabu Kubwa”
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2019
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2025
w25 Mwezi wa 8 uku. 31

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Kazi ya kuhubiri itaisha wakati gani?

Yesu alisema hivi: “Hii habari njema ya Ufalme itahubiriwa katika dunia yote yenye kuikaliwa na watu ili kuwa ushahidi kwa mataifa yote, na kisha ule mwisho utakuja.” (Mt. 24:14) Neno ya Kigiriki yenye inatafsiriwa “mwisho” mu hii mustari na mu mustari wa 6 na wa 13, ni teʹlos. Ile neno inamaanisha mwisho kabisa wa ulimwengu wa Shetani ku vita ya Armagedoni. (Ufu. 16:14, 16) Kwa hiyo, kazi ya kuhubiri itaisha mbele tu ile mwisho ifike. Ile inarekebisha namna tulielewa zamani.

Zamani tulielewa kama tutaacha kuhubiri habari njema wakati taabu kubwa itaanza, ni kusema wakati Babiloni Mukubwa itaharibiwa. (Ufu. 17:3, 5, 15, 16) Tuliwaza kama wakati taabu kubwa itaanza, ile njo itakuwa mwisho wa “mwaka [wa mufano] wa nia njema ya Yehova,” ni kusema tuliwaza kama kisha pale Yehova hatapatia tena batu nafasi ya kukubali habari njema. (Isa. 61:2) Pia tuliwaza kama benye bataokoka taabu kubwa ni benye batakuwa bameonyesha kama ni baaminifu mbele taabu kubwa ianze. Tulibafananisha na Bayahudi benye baliokoka uharibifu wa Yerusalemu mu mwaka wa 607 mbele ya kuzaliwa kwa Yesu. Bale Bayahudi balikuwa bametiwa alama mbele, juu balimuabudu Yehova na balichukia mambo ya mubaya. (Eze. 5:11; 9:4) Lakini kulinganisha benye bataokoka taabu kubwa na benye baliokoka uharibifu wa Yerusalemu, haipatane na maneno ya Yesu yenye iko mu Matayo 24:14, yenye inaonyesha kama batu batakuwa na nafasi ya kukubali habari njema hata mbele tu mwisho ifike, mbele ya Armagedoni.

Namna yetu ya mupya ya kuelewa Matayo 24:14 inafanya turekebishe namna yetu ya kuelewa Ufunuo 16:21 yenye inazungumuzia mvua kubwa ya majiwe. Kisha kuchunguza ile maandiko mbili tumeona kama inazungumuzia jambo moya; andiko moya inaongezea ingine. Kitu yenye inatusaidia kujua ile ni namna Biblia inazungumuzia vile batu banaitikia wakati banasikia ujumbe wa Ufalme. Mutume Paulo aliandika kama kwa “wale wenye kuokolewa,” ujumbe wa Ufalme ni habari njema, “harufu ya uzima.” Lakini kwa maadui wa Mungu ni habari ya mubaya, “harufu ya kifo.” (2 Ko. 2:15, 16) Banachukia ujumbe wa Ufalme juu unaonyesha kama ulimwengu wabo wenye banapenda, ni mubaya, unatawaliwa na Shetani, na utaharibiwa.—Yoh. 7:7; 1 Yo. 2:17; 5:19.

Ufunuo 16:21 inaonyesha pia kama ile mvua kubwa ya majiwe itakuwa “kubwa ajabu.” Ile inaweza kumaanisha kama wakati wa taabu kubwa, kazi yetu ya kuhubiri itatikisa batu na itafikia batu mingi sana kupita wakati wowote. Kwa hiyo, batu mingi batajua jina ya Yehova. (Eze. 39:7) Je, mu ile wakati, ni kusema kisha uharibifu wa Babiloni mukubwa, kutakuwa batu benye batakubali ujumbe wetu, sawa vile harufu ya muzuri? Inawezekana. Pengine batakumbuka ao batajua kama kwa miaka mingi Mashahidi wa Yehova walihubiri kama dini za uongo zitaharibiwa.

Ile itafanana na mambo yenye ilitokea mu Misri ya zamani kisha mapigo kumi. Kisha Yehova “[kuleta] hukumu juu ya miungu yote ya Misri, . . . kikundi kikubwa cha watu wenye kuchangamana” wenye hawakukuwa Waisraeli, walijiunga na watu wake. (Kut. 12:12, 37, 38) Pengine bale batu benye habakukuwa Baisraeli baliamua kuenda na Baisraeli wakati baliona kama mambo yote yenye Musa alisema juu ya zile pigo kumi ilitimia.

Kila mutu mwenye ataamua kuwa ngambo ya Yehova kisha Babiloni Mukubwa kuharibiwa, atakuwa na nafasi ya kutegemeza ndugu za Kristo wenye watakuwa wangali ku dunia. (Mt. 25:34-36, 40) Hata vile, nafasi ya kuhukumiwa kuwa kondoo itaisha muda kidogo tu mbele Armagedoni ianze, wakati batiwa-mafuta benye batakuwa bangali ku dunia batapanda mbinguni.

Hii Mafasirio ya mupya inaonyesha kabisa kama Yehova iko na upendo sana na rehema ya mingi. “Hataki mutu yeyote aharibiwe lakini anataka wote wafikie kutubu.”—2 Pe. 3:9.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2026)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine