Maulizo ya Wasomaji Wetu
Ni “wazo” gani yenye Yehova atatia mu mioyo ya mataifa hivi karibuni?
Kuhusu mwanzo wa taabu kubwa, Ufunuo 17:16, 17 inasema hivi: “Zile pembe kumi (10) zenye uliona, na ule munyama wa pori, hawa watamuchukia ule kahaba na kumuacha bila kitu na uchi, na watakula nyama yake na kumuteketeza kabisa kwa moto. Kwa maana Mungu alitia jambo hilo ndani ya mioyo yao ili kutimiza wazo lake, ndiyo, kutimiza lile wazo lao moja kwa kumupatia ule munyama wa pori ufalme wao.” Zamani bichapo yetu ilisema kama ile wazo ni “wazo” ya kuharibu dini za uongo.
Lakini inaomba tubadilishe namna tulielewa zamani. “Wazo” yenye Yehova atatia mu mioyo ya ile mataifa ni wazo ya kupatia “ule munyama wa pori ufalme wao.” Juu ya kuelewa vile ile unabii itatimia, tutajibia maulizo yenye kufuata.
Ni nani njo anazungumuziwa mu hii unabii? Hii unabii inazungumuzia “ule kahaba” mwenye anaitwa pia “Babiloni Mukubwa”; ule kahaba anafananisha dini zote za uongo. Inazungumuzia pia “munyama wa pori mwenye rangi nyekundu yenye kungaa” mwenye anafananisha Umoja wa Mataifa. Umoja wa Mataifa ilianzishwa mu 1919 juu isaidie kuleta amani mu ulimwengu, ile wakati iliitwa Muungano wa Mataifa. (Ufu. 17:3-5) Tena hii unabii inazungumuzia “zile pembe kumi (10)” zenye zinafananisha serikali zote zenye zinaunga mukono ule munyama wa pori.
Ule kahaba na ule munyama wa pori mwenye rangi nyekundu yenye kungaa biko na uhusiano gani? Kwa miaka mingi, ule kahaba “amekaa juu ya” ule munyama wa pori. Ni kusema anajaribu kumuongoza na hata kumutawala.
Ni nini njo itapata ule kahaba? Ule munyama wa pori na zile pembe kumi zenye kumuunga mukono, “watamuchukia ule kahaba.” Juu ya ile chuki, batamunyanganya kila kitu yenye iko nayo na kuonyesha batu yote bubaya yake. Kisha batatimiza hukumu ya Yehova juu yake, ni kusema batamuharibu kabisa. (Ufu. 17:1; 18:8) Lakini mbele ile itokee, Yehova atachochea mataifa ifanye jambo fulani yenye haiyafanyikaka mu historia ya banadamu.
Yehova atachochea mataifa ifanye nini? Atatia mu mioyo ya zile pembe kumi “wazo lake,” wazo la ‘kupatia ule munyama wa pori [mwenye rangi nyekundu yenye kungaa ]’ ni kusema Umoja wa Mataifa, “nguvu na mamlaka yao.” (Ufu. 17:13) Ile inaonyesha nini? Inaonyesha kama haiko serikali za banadamu zenyewe njo zitaamua kupatia ule munyama wa pori mamlaka na nguvu. Lakini sawa vile hii unabii inaonyesha, ni Mungu mwenyewe njo atazichochea zifanye vile. (Mez. 21:1; linganisha na Isaya 44:28.) Na ile yote haitatokea pole kwa pole, itakuwa jambo ya kushitukia na ya haraka. Kisha ule munyama wa pori mwenye atakuwa sasa amepewa nguvu, ataharibu kabisa-kabisa dini zote za uongo.
Tunaweza kutazamia nini? Tusitazamie kupata habari zenye zinaonyesha kama pole kwa pole serikali zimeanza kuunga mukono zaidi Umoja wa Mataifa. Jambo yenye tunaweza kutazamia ni hii: Kwa kushitukia Yehova atatia mu mioyo ya mataifa wazo ya kupatia Umoja wa Mataifa mamlaka yao. Wakati ile itatokea, tutajua kama taabu kubwa iko karibu kuanza. Lakini mbele ile mambo yote ifike, “tukae macho na kulinda akili zetu” juu hivi karibu mambo itabadilika haraka sana!—1 Te. 5:6.