Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • g 3/14 uku. 14-15
  • Wakati Unavunjika Moyo kwa Sababu ya Ndoa Yako

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Wakati Unavunjika Moyo kwa Sababu ya Ndoa Yako
  • Amuka!—2014
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • TATIZO
  • Wakati Urafiki Unakuwa wa Nguvu Sana
    Amuka!—2013
  • Namna ya Kusamehe
    Amuka!—2013
  • “Ndoa na Iheshimiwe”
    Mubaki “Katika Upendo wa Mungu”
  • Wakati Mawazo Inapingana
    Musaada kwa Familia
Ona Habari Zaidi
Amuka!—2014
g 3/14 uku. 14-15
Mwanamuke anayesikia kuvunjika moyo kwa sababu ya ndoa yake

MUSAADA KWA FAMILIA | NDOA

Wakati Unavunjika Moyo kwa Sababu ya Ndoa Yako

TATIZO

Bibi na bwana wenye kufungwa munyororo kwenye miguu

Wewe na bibi ao bwana yako mulionekana kuwa mulipatana katika mambo mengi mbele mufunge ndoa. Sasa, kuvunjika moyo kunafanya uhusiano wenu uwe zaifu na unajisikia kuwa unafungwa na bibi ao bwana yako, kuliko kufurahia kuwa pamoja naye.

Unaweza kufanya uhusiano wenu uwe muzuri. Kwanza, fikiria sababu gani unaweza kujisikia kuwa unavunjika moyo.

SABABU GANI JAMBO HILO LINATOKEA?

Mahangaiko ya maisha. Kutumika kila siku, kulea watoto, na kuhangaikia wakwe, mambo hayo yote yanaweza kuharibu polepole furaha ya ndoa. Tena, magumu yasiyotazamiwa yanaweza kuleta mahangaiko katika ndoa, pengine matatizo ya feza ao kumuhangaikia mutu fulani wa familia aliye na ugonjwa usioweza kupona.

Inaonekana kuwa tabia zenu hazipatane kabisa. Wakati wa uchumba, mwanaume na mwanamuke hawajali tabia zilizo tofauti kati yao. Lakini wakati wanaoana, wanatambua kuwa tabia zao hazipatane katika mambo mengi, kama vile, namna ya kuzungumuza, namna ya kutumia feza, na namna ya kutatua matatizo. Tabia ambazo mbele zilikuuzi kidogo tu zinaweza sasa kuonekana kuwa hauwezi kuzivumilia.

Kila mumoja wenu hahangaikie namna mwenzake anajisikia moyoni. Baada ya muda, kuweka katika akili maneno yasiyofaa ambayo bibi ao bwana yako alikuambia ao mambo mabaya aliyokufanyia, na kuweka matatizo mengi bila kuyatatua kunaweza kumufanya bibi ao bwana ajizuie kueleza namna anavyojisikia moyoni. Na jambo mbaya zaidi, anaweza kuanza kuwa na uhusiano wa kimapenzi na mutu mwengine.

Mambo uliyotazamia hayakutimizwa. Watu fulani wanafunga ndoa wakiamini kwamba wamepata mutu aliyetayarishwa kabisa kwa ajili yao. Hata ikiwa wazo hilo linaweza kuonekana kuwa ni la kimapenzi, linaweza kuleta tatizo. Wakati magumu yanatokea katika ndoa, wazo la uongo la kwamba mutu alipata “bibi ao bwana mukamilifu” linavunja moyo, na kumufanya bibi na bwana wote wawili wajisikie kuwa walichagua vibaya.

MAMBO UNAYOWEZA KUFANYA

Kazia akili sifa nzuri za bibi ao bwana yako. Jaribu kufanya hivi: Andika sifa tatu nzuri za bibi ao bwana yako. Pengine unaweza kuziandika nyuma ya picha ndogo ya ndoa, katika telefone ao ordinatere yako ya mukononi na uwe na nafasi uliandika sifa hizo mahali pote unapopatikana. Usome sifa hizo mara kwa mara ili ukumbuke sababu gani ulioa ao kuolewa na bibi ao bwana yako. Kukazia akili sifa nzuri za bibi ao bwana yako kunasaidia kuleta amani na kutakusaidia uvumilie tabia zake zilizo tofauti na zako.​—Kanuni ya Biblia: Waroma 14:19.

Mupange wakati wa kupitisha pamoja. Mbele muoane, pengine mulikuwa munapanga wakati wa kufanya mambo pamoja. Wakati wa uchumba ulikuwa wakati muzuri na wenye kufurahisha, kwa sababu mulizoea kupanga wakati wa kupitisha pamoja. Munaweza kufanya hivyo leo pia. Mupange mambo ambayo yatafanya mupitishe wakati wa pekee pamoja, kama mulivyokuwa munafanya wakati wa uchumba. Kufanya hivyo kunaweza kuwasaidia muwe na uhusiano wa karibu na kunaweza kuwawezesha mupambane vizuri na matatizo yanayoweza kutokea katika maisha bila kutazamia.​—Kanuni ya Biblia: Methali 5:18.

Muzungumuzie namna munavyojisikia moyoni. Ikiwa maneno ao matendo ya bibi ao bwana yako yalikuumiza, je, unaweza kusahau jambo hilo? Ikiwa hauwezi kusahau, tenda kama mutu muzima kwa kuepuka kumunyamazia bibi ao bwana yako. Zungumuzia matatizo yako kwa upole na bibi ao bwana yako bila kukawia, siku hiyohiyo ikiwa inawezekana.​—Kanuni ya Biblia: Waefeso 4:26.

Ikiwa maneno ao matendo ya bibi ao bwana yako yalikuumiza, je, unaweza kusahau jambo hilo?

Ujue kwamba bibi ao bwana yako hakukusudia kukuumiza. Inaelekea kwamba hakuna mumoja wenu anayekusudia kumuumiza mwengine hata siku moja. Umuhakikishie bibi ao bwana yako jambo hilo kwa kumuomba musamaha wa kweli kwa sababu ya jambo lolote ulilofanya ambalo lilimuumiza. Kisha muzungumuzie mambo munayoweza kufanya ninyi wawili ili kuepuka kuumizana bila kukusudia. Mufuate shauri hili la Biblia: ‘Iweni wenye fazili ninyi kwa ninyi, wenye huruma nyororo, mukisameheana kwa hiari.’​—Waefeso 4:32.

Usitazamie mambo mengi kupita kiasi. Biblia inakubali kwamba wale wanaooa ao kuolewa ‘watakuwa na ziki.’ (1 Wakorintho 7:28) Wakati unapata ziki ao magumu kama hayo, usiseme haraka kwamba ulichagua vibaya. Lakini, ujikaze kutatua matatizo wewe na bibi ao bwana yako na ‘muendelee kuvumiliana na kusameheana kwa hiari.’​—Wakolosai 3:13.

MAANDIKO YA MAANA

  • “Tufuatilie mambo yanayofanya kuwe na amani.”—Waroma 14:19.

  • ‘Ushangilie pamoja na muke wa ujana wako.’—Methali 5:18.

  • ‘Jua lisitue mukiwa katika hali ya kuchokozeka.’—Waefeso 4:26.

UISHI KUPATANA NA KIAPO CHAKO CHA NDOA

Unakumbuka maneno uliyosema katika kiapo chako cha ndoa? Unaweza kuyarudilia na kujiuliza hivi, ‘Ninafanya nini ili kuishi kupatana na mambo niliyoahidi?’ Epuka kishawishi cha kukazia akili mambo ambayo bibi ao bwana yako anafanya kuhusiana na jambo hilo. Kiapo chako kina maneno ambayo wewe mwenyewe ulisema juu ya mambo ambayo wewe utafanya. Ikiwa kila mumoja wenu anajikaza kuishi kupatana na kiapo chake, inaelekea kwamba ninyi wote wawili mutafurahia matokeo mazuri.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine