Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • g 4/14 uku. 4-5
  • Namna ya Kukubali Marekebisho

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Namna ya Kukubali Marekebisho
  • Amuka!—2014
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • TATIZO
  • Nizamu—Inaonyesha Upendo wa Yehova
    Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2019
  • Namna ya Kupambana na Magumu
    Amuka!—2019
  • 6 Nizamu
    Amuka!—2018
  • Kufundisha Watoto Unyenyekevu
    Amuka!—2017
Ona Habari Zaidi
Amuka!—2014
g 4/14 uku. 4-5

MUSAADA KWA FAMILIA | VIJANA

Namna ya Kukubali Marekebisho

TATIZO

“Wakati mutu fulani anakurekebisha, kwa kweli mutu huyo anakuambia kwamba unafanya jambo fulani mbaya. Na sijue mutu yeyote anayeweza kusema, ‘Ninapenda mutu aniambie kwamba ninafanya jambo fulani mbaya!’”​—Amy, aliye na miaka 17.a

Watumishi katika munara wa kuongozea ndege wanaoongoza ndege mbili ili zisigongane

Mutu anayekataa marekebisho anafanana na mutu wa kuendesha ndege anayezarau uongozi kutoka kwenye munara wa kuongozea ndege. Matokeo yanaweza kuwa mabaya sana.

Unaona kuwa vigumu kukubali marekebisho kutoka kwa wazazi, walimu wako, na watu wengine wenye kukomaa? Ikiwa ni vile, habari hii itakusaidia.

MAMBO UNAYOPASWA KUJUA

Kila mutu ana lazima ya kurekebishwa.

‘Sisi wote tunajikwaa mara nyingi.’​—Yakobo 3:2.

“Hakuna sababu ya kusikia haya unapokuwa na lazima ya kurekebishwa wakati unafanya jambo fulani mbaya.”​—Jessica.

Kurekebishwa hakumaanishe kwamba wewe ni mutu mubaya.

‘Yeye ambaye Yehovab anamupenda, anamukaripia, kama vile baba anavyomukaripia mwana anayemufurahia.’​—Methali 3:12.

“Wakati watu wananirekebisha, ninajaribu kukazia akili namna ni vigumu kwao kufanya hivyo na namna wananionyesha upendo kwa kunipatia shauri.”​—Tamara.

Marekebisho yanaweza kukusaidia uwe mutu muzuri.

‘Sikiliza nizamu upate kuwa na hekima.’​—Methali 8:33.

“Marekebisho ni ya lazima ili kukomaa. Yanamusaidia mutu ajue namna wengine wanamuona na kuacha tabia mbaya ambazo labda hajue kama amekuwa nazo.”​—Deanne.

MAMBO UNAYOWEZA KUFANYA

Uone marekebisho kwa njia inayofaa. Marekebisho yanaweza kukufanya ukasirike. Lakini ujikaze kuzuia hasira yako. Ili uweze kufanya hivyo, ujitoshe kwa muda fulani katika hali hiyo na uwazie kuwa ni wewe unayemurekebisha mutu mwengine, kwa mufano ndugu yako mudogo. Je, sasa unaona mambo fulani mazuri katika shauri hilo? Kisha ujirudishe katika hali hiyo na ujaribu kuona mambo kwa njia ileile.​—Kanuni ya Biblia: Mhubiri 7:9.

“Wakati mwengine unaweza kukasirika mutu fulani anapokuonyesha makosa yako na hivyo unasahau kwamba mutu huyo alijaribu kukusaidia ili ukuwe mutu muzuri, lakini hakutaka kukuumiza moyoni.”​—Theresa.

Endelea kuwa munyenyekevu. Usiache kiburi kikufanye ukatae marekebisho. Kwa upande mwengine, usijiache uvunjike moyo sana kwa sababu tu una jambo fulani la kurekebisha. Unyenyekevu utakusaidia kuepuka mambo hayo mawili, ni kusema kiburi na kuvunjika moyo. Kumbuka: Marekebisho yanayoumiza sana moyoni yanaweza kuwa ndiyo marekebisho uliyo nayo lazima kabisa. Ikiwa, kwa sababu fulani, unakataa marekebisho, unapoteza nafasi nzuri ya kukomaa.​—Kanuni ya Biblia: Methali 16:18.

Marekebisho yanayoumiza sana moyoni yanaweza kuwa ndiyo marekebisho uliyo nayo lazima kabisa

“Kukubali marekebisho ni moja kati ya mambo ya maana yanayofanya mutu akomae. Ikiwa hatujifunze kuyakubali na kukomaa kutokana nayo, tunaweza hata kufikia kujiumiza wenyewe.”​—Lena.

Onyesha shukrani. Hata ikiwa unaona kuwa ni vigumu kukubali marekebisho, ni vizuri kumuonyesha shukrani mutu aliyekurekebisha. Bila shaka, mutu huyo anakutakia mema, na anataka kabisa upate matokeo mazuri.​—Kanuni ya Biblia: Zaburi 141:5.

“Hakuna ubaya kusema aksanti, zaidi sana ikiwa tulikuwa na lazima ya shauri. Hata ikiwa haukuwa na lazima ya shauri, unaweza kuonyesha adabu na shukrani kwa bidii ambayo mutu huyo alifanya ili kukufikia.”​—Carla.

a Majina fulani yamebadilishwa katika habari hii.

b Yehova ni jina la Mungu kama inavyoonyeshwa katika Biblia.

MAANDIKO YA MAANA

  • ‘Usikuwe na haraka kuuzika katika roho yako.’​—Mhubiri 7:9.

  • ‘Kiburi kinatangulia kuanguka.’​—Methali 16:18.

  • ‘Muadilifu akinipiga [kwa karipio], zingekuwa fazili zenye upendo.’​—Zaburi 141:5.

“Kuonyeshwa makosa kunaweza kuumiza moyoni, lakini ninajikaza kukumbuka kwamba mutu anayenionyesha makosa yangu anapenda nikuwe mutu muzuri zaidi kama ninavyopaswa kuwa. Ninajaribu kumuona kuwa rafiki anayenisaidia nipate matokeo mazuri katika maisha.”​—JUSTIN

“Ninajua kwamba nitakosea, kwa hiyo, ninashukuru wakati watu wananiambia kuwa nimekosea. Hilo linanisaidia nijue jambo ninalopaswa kurekebisha.”​—CHARLETTE

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine