Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • g 8/15 uku. 8-9
  • Kufundisha Watoto Sifa ya Kujizuia

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Kufundisha Watoto Sifa ya Kujizuia
  • Amuka!—2015
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • MAGUMU
  • Faida za Kuwa Mwenye Kujizuia
    Amuka!—2019
  • Komalisha Sifa ya Kujizuia
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2017
  • Kujizuia Ni Sifa ya Maana Sana ili Kukubaliwa na Yehova
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2020
Amuka!—2015
g 8/15 uku. 8-9
Mutoto mudogo mwanamuke anamulalamikia kwa hasira mama yake na anamushota kidole ndugu yake mwanaume

MUSAADA KWA FAMILIA | KULEA WATOTO

Kufundisha Watoto Sifa ya Kujizuia

MAGUMU

Mutoto wako wa miaka sita anaonekana kuwa hajue kabisa kujizuia. Kama anaona kitu fulani chenye anataka, anapenda kukipata palepale! Kama anakasirika, wakati fulani anafoka kwa hasira kubwa. Unajiuliza, ‘Hii ni tabia ya kawaida kwa mutoto? Tabia hii itaisha kisha wakati fulani, ao huu ndio wakati wa kumufundisha sifa ya kujizuia?’

MAMBO UNAPASWA KUJUA

Desturi za leo hazikazie sifa ya kujizuia. Musomi David Walsh anasema hivi: “Katika desturi yetu yenye kuachilia mambo, mara nyingi watu wazima na watoto wanasikia habari zenye kuonyesha kuwa tunapaswa kufanya kila kitu tunapenda. Kuanzia watu wenye kushauria wengine mupaka watu wenye kutumia ujanja ili kuiba feza za wengine, mara kwa mara tunasikia kuwa tunapaswa kutimiza tamaa zetu.”a

Ni jambo la lazima kufundisha mutoto sifa ya kujizuia tangu utoto. Katika uchunguzi mumoja wenye ulifanywa kwa miaka mingi, wachunguzi walipatia watoto wa miaka ine bombo moja moja. Waliwaambia kama wanaweza kula bombo hiyo palepale ao kungojea kwa muda kidogo ili wapewe zawadi ya bombo ingine kwa sababu ya uvumilivu wao. Kisha miaka mingi, wakati watoto hao walikuwa wamemaliza masomo, wale wenye walijizuia wakati walikuwa na miaka ine ndio walikuwa na afya ya muzuri ya moyoni, ya akili, na walikuwa wanaishi muzuri na wengine.

Kukosa kufundisha mutoto sifa ya kujizuia kunaweza kuleta matokeo mabaya. Wachunguzi wanaamini kuwa namna ubongo wa mutoto unafanya kazi inaweza kubadilika kupitia mambo yenye anaona katika maisha. Kulingana na Musomi Dan Kindlon, hilo linamaanisha kama “Ikiwa tunadekesha watoto (ao kuwabembeleza sana), hatuwafundishe namna ya kungoja wakati wao ufike, kuzuia tamaa zao, na namna ya kupinga vishawishi, pengine hilo linaweza kufanya wasikuwe na tabia za muzuri.”b

MAMBO UNAWEZA KUFANYA

Uonyeshe mufano. Wewe mwenyewe unaonyesha sifa ya kujizuia? Mutoto wako anaona kama unakosa kujizuia wakati motokari zinafungana sana katika barabara, unatambuka wengine kwenye mustari katika duka, ao unakatikiza wengine wakati wanazungumuza? Kindlon aliandika hivi: “Njia ya muzuri zaidi ya kusaidia watoto wetu wakuwe na sifa ya kujizuia ni kuonyesha sifa hiyo sisi wenyewe.”—Kanuni ya Biblia: Waroma 12:9.

Ufundishe mutoto wako matokeo ya kukosa kujizuia. Kwa njia inayofaa miaka ya mutoto, umufundishe kuona kama anaweza kupata faida ikiwa anazuia tamaa zake na kama anaweza kupata matokeo mabaya ikiwa anashindwa kuzizuia. Kwa mufano, ikiwa mutoto wako anakasirika kwa sababu mutu fulani alimutendea mubaya, umusaidie afikiri kidogo na kujiuliza hivi: ‘Kulipiza kisasi kutanisaidia ao kutaniumiza? Kunaweza kuwa njia ya muzuri ya kupambana na hali hiyo, pengine kwa kuhesabu moja mupaka kumi ili hasira itulie? Inaweza kuwa muzuri sana kuondoka?’—Kanuni ya Biblia: Wagalatia 6:7.

Umutie moyo mutoto wako. Umusifu mutoto wako wakati anaonyesha sifa ya kujizuia. Umujulishe kama wakati fulani haiko vyepesi kuzuia tamaa zake lakini wakati anafanya hivyo, anaonyesha kama iko na nguvu! Biblia inasema hivi: ‘Mutu asiyezuia roho yake ni kama jiji lililobomolewa, lisilo na ukuta.’ (Methali 25:28) Lakini, ‘asiye mwepesi wa hasira ni bora [muzuri] kuliko mwanaume mwenye nguvu.’—Methali 16:32.

Mufanye mazoezi. Mufanye muchezo wenye utaita “Unaweza Kufanya Nini?” ao “Maamuzi Mazuri na Maamuzi Mabaya” ao muchezo mwengine wa namna hiyo. Muzungumuzie hali zenye zinaweza kutokea na namna mbalimbali mutu anaweza kutenda, unaweza kuziita, “namna za muzuri” na “namna za mubaya.” Utumie vitu mbalimbali: Ikiwa unapenda, utumie popi, michoro (dessins), ao ufundi mwengine ambao utafanya muchezo huo ukuwe wenye kufurahisha na wenye kufundisha. Kusudi lako ni kusaidia mutoto wako aone kama kuwa na sifa ya kujizuia ni muzuri kuliko kutimiza tamaa zake palepale.—Kanuni ya Biblia: Methali 29:11.

Ukuwe muvumilivu. Biblia inasema kama ‘ujinga umefungwa pamoja na moyo wa muvulana [kijana mwanaume].’ (Methali 22:15) Kwa hiyo, usiwazie kuwa mutoto wako atakuwa na sifa ya kujizuia mara moja. Kitabu kimoja kinasema hivi: “Hiyo ni hatua ya siku nyingi, ya polepole na yenye kuleta maendeleo kisha, inaweza kuwa vigumu wakati fulani, lakini kunakuwa maendeleo zaidi.” (Teach Your Children Well) Hata hivyo, bidii yako haiko ya bure. Kitabu hicho kinasema tena hivi: “Mutoto mwenye kujizuia anaweza kukataa dawa za kulewesha wakati atakuwa na miaka 12 na kukataa kufanya kitendo cha ndoa wakati atakuwa na miaka 14.”

a Maneno yenye kutoka katika kitabu No: Why Kids—of All Ages—Need to Hear It and Ways Parents Can Say It.

b Maneno yenye kutoka katika kitabu Too Much of a Good Thing—Raising Children of Character in an Indulgent Age.

MAANDIKO YA MAANA

  • “Upendo wenu na uwe bila unafiki.”—Waroma 12:9.

  • ‘Lolote lile analopanda mutu, atavuna hilo pia.’—Wagalatia 6:7.

  • ‘Mutu mujinga anaachilia roho yake yote, lakini mwenye hekima anaituliza mupaka mwisho.’—Methali 29:11.

UPATIE MUTOTO ZAWADI KWA AJILI YA TABIA YA MUZURI

Hata watoto wenye kujifunza kutembea wanaweza kufundishwa sifa ya kujizuia. Kitabu kimoja kinasema hivi: “Ikiwa mutoto analia sana ili umupatie bombo kwenye duka na unamupatia, umemufundisha kama kulia ndiyo njia ya muzuri ya kupata kitu chenye anataka. Wakati mwengine akitaka kitu fulani, atalia sana ili kupata kitu hicho kwa sababu wakati uliopita alilia na akapata kitu chenye alikuwa anataka. Lakini, upatie mutoto zawadi kwa ajili tu ya tabia ya muzuri. Wazazi wengi wanaitika kupatia mutoto kitu analilia kwa sababu hilo linaonekana kuwa jambo jepesi, ao kwa sababu hawawezi kukatalia mutoto kitu fulani chenye anataka. Lakini, ikiwa unapatia mutoto kila kitu chenye anataka, unamunyima mambo mengi. Kupatia mutoto zawadi kwa sababu aliomba kwa njia ya muzuri kunamufundisha kuwa na sifa ya kujizuia na kusikilizana na watu wengine.” (Generation Me)

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine