Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • g17 na. 5 uku. 10-11
  • Vita

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Vita
  • Amuka!—2017
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Sababu gani Waisraeli wa zamani walienda kwenye vita?
  • Leo, Mungu anaunga mukono upande fulani katika vita?
  • Vita itaisha siku moja?
  • Mungu Anaona Vita Namna Gani?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Namna Mungu Anaona Vita Leo
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Waisraeli wa Zamani Walipigana Vita​—Juu ya Nini Siye Hapana?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2022
  • Namna Mungu Aliona Vita Wakati wa Zamani
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
Ona Habari Zaidi
Amuka!—2017
g17 na. 5 uku. 10-11
Bunduki yenye kukatika vipande-vipande

MAWAZO YA BIBLIA

Vita

Zamani, Waisraeli walipigana vita katika jina la Mungu wao, Yehova. Hilo linamaanisha kwamba Mungu anakubali vita ya siku zetu?

Sababu gani Waisraeli wa zamani walienda kwenye vita?

MAMBO WATU FULANI WANASEMA

Waisraeli waliabudu mungu wa vita mwenye kuwa na kiu ya damu.

MAMBO BIBLIA INASEMA

Mataifa yenye Israeli ilipiga yalichafuka na matendo mabaya sana ya jeuri na mwenendo mubaya​—kutia ndani kulala na wanyama, kufanya ngono na mutu wa familia, na zabihu ya watoto. Kisha kuwaachia mamia ya miaka ili kubadilisha mwenendo wao, Mungu alisema hivi: “Kwa sababu kwa mambo yote hayo mataifa ninayoyafukuza kutoka mbele yenu yamejifanya yenyewe kuwa si safi.”​—Mambo ya Walawi 18:21-25; Yeremia 7:31.

“Yehova anayafukuzia mbali mataifa haya kutoka mbele yako kwa sababu ya uovu wao.”​—Kumbukumbu la Torati 9:5.

Leo, Mungu anaunga mukono upande fulani katika vita?

PENGINE UMEKWISHA KUONA

Katika vita nyingi, viongozi wa dini wa pande zote mbili wanasema kwamba Mungu iko upande wao. Kitabu The Causes of War kinasema hivi: “Tangu zamani dini imeunga mukono upande fulani katika vita vyote vyenye vimefanywa.”

MAMBO BIBLIA INASEMA

Wakristo hawaruhusiwe kupigana na maadui wao. Mutume Paulo aliandikia Wakristo wenzake hivi: ‘Ikiwezekana, kwa kadiri inavyowategemea ninyi, iweni wenye kufanya amani na watu wote . . . Musijilipizie kisasi.’​—Waroma 12:18, 19.

Kuliko kutuma wafuasi wake kwenye vita, Yesu aliwaambia hivi: ‘Muendelee kuwapenda adui zenu na kusali kwa ajili ya wale wanaowatesa ninyi; ili mupate kuwa wana wa Baba yenu aliye mbinguni.’ (Mathayo 5:44, 45) Hata wakati taifa ambamo wanaishi linafanya vita, Wakristo hawapaswe kuunga mukono upande wowote, wao “si sehemu ya ulimwengu.” (Yohana 15:19) Kama Mungu anapenda waabudu wake katika mataifa yote wapende maadui wao na kukataa kujiingiza katika mambo ya ulimwengu, namna gani anaweza kutegemeza upande fulani wenye kupigana leo?

“Ufalme wangu si sehemu ya ulimwengu huu. Kama ufalme wangu ungekuwa sehemu ya ulimwengu huu, watumishi wangu wangepigana ili nisitiwe mikononi mwa Wayahudi. Lakini, kama ilivyo, ufalme wangu hautoki katika chanzo hiki.”​—Yohana 18:36.

Vita itaisha siku moja?

MAMBO WATU FULANI WANASEMA

Vita haiwezi kuepukwa. Kitabu War and Power in the 21st Century kinasema hivi: “Vita itaendelea. Hakuna tumaini lolote la kuwa na amani katika kipindi chetu.”

MAMBO BIBLIA INASEMA

Vita vitakwisha wakati hakutakuwa tena mutu yeyote mwenye kuwa na tamaa ya kufanya vita. Kwa hiyo, Ufalme wa Mungu​—serikali ya kweli yenye kutawala ikiwa mbinguni​—itatenda ili kumaliza silaha katika dunia na kufundisha watu kufuatilia amani. Biblia inatuhakikishia kwamba Mungu “[atanyoosha] mambo kuhusu mataifa yenye nguvu yaliyo mbali. Nao watafua panga zao ziwe majembe na mikuki yao iwe miundu. Hawatainua upanga, taifa juu ya taifa, wala hawatajifunza vita tena.”​—Mika 4:3.

Biblia inafundisha kwamba chini ya Ufalme wa Mungu, hakutakuwa serikali za mataifa zenye kufuatilia faida zao, mawazo ao mipango ya mubaya yenye kuchochea wakaaji waasi, ao kuchochea migawanyiko kati ya makabila. Matokeo ni kwamba vita itaisha. Mungu anaahidi hivi: ‘Hawatasababisha mazara yoyote wala kusababisha uharibifu wowote . . . kwa maana dunia hakika itajawa na kumujua Yehova kama vile maji yanavyoifunika bahari.’​—Isaya 11:9.

‘Anakomesha vita mupaka kwenye mwisho wa dunia. Upinde anauvunja na kuukata mukuki vipande-vipande; magari ya kukokotwa anayateketeza motoni.’ ​—Zaburi 46:9.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine