Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • g18 na. 1 uku. 10-11
  • Kusamehe

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Kusamehe
  • Amuka!—2018
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • KANUNI ZA BIBLIA ZINASAIDIA KABISA!
  • Ukuwe Tayari Kusamehe
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Namna ya Kusamehe
    Amuka!—2013
  • Tuwe Tayari Kusameheana
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • 4 Kusameheana
    Amuka!—2018
Ona Habari Zaidi
Amuka!—2018
g18 na. 1 uku. 10-11
Mwanamuke mumoja anamusamehe rafiki yake

NJIA YA MAISHA YENYE FURAHA

Kusamehe

“WAKATI NILIKUWA MUTOTO, NILIZOEA KUSIKIA MATUKANO NA KULALAMIKIANA KATIKA FAMILIA YETU.” Ni vile mwanamuke mumoja mwenye kuitwa Patricia alisema. Anaongeza hivi, “Sikujifunza kusamehe. Hata wakati nilikuwa mutu muzima, ningeendelea kufikiria mambo ya mubaya yenye nilitendewa, na kukosa usingizi.” Kwa kweli, maisha yenye kujaa kasirani na kinyongo ni maisha yenye haina furaha na haiko muzuri kwa afya. Uchunguzi mbalimbali unaonyesha kwamba mutu mwenye hapendake kusamehe anaweza . . .

  • Kuacha kasirani ao uchungu viharibishe urafiki, jambo lenye linaweza kufanya ajitenge na wengine na ajisikie kuwa peke yake

  • Kukasirika haraka, kuwa na mahangaiko, ao hata kushuka moyo sana

  • Kukaza sana akili juu ya makosa mupaka anashindwa kufurahia maisha

  • Kujisikia kwamba hafuate kanuni za Mungu

  • Kuwa na mahangaiko mengi na kuwa katika uwezekano mukubwa wa kuwa na magonjwa hatari, kutia ndani damu kutembea haraka sana, magonjwa ya moyo, na maumivu mbalimbali, kama vile rhumatisme na maumivu ya kichwaa

KUSAMEHE NI NINI? Kusamehe ni tendo la kuhurumia mutu mwenye alikukosea, kuacha kasirani, kinyongo na mawazo ya kulipiza kisasi. Hilo halimaanishe kuachilia tu kosa, kupunguza uzito wa kosa, ao kufanya kama vile kosa hilo halikufanyika. Lakini, kusamehe ni uamuzi wenye mutu anafikiria muzuri, na wenye anaona kuwa ndilo jambo la maana ili kufanya amani na kujenga ao kukomalisha urafiki wa muzuri pamoja na mutu mwenye alimukosea.

Kusamehe kunaonyesha kwamba mutu iko na utambuzi. Mutu mwenye kusamehe anatambua kwamba sisi wote tunakosea, ao kufanya zambi katika maneno na matendo. (Waroma 3:23) Biblia inakazia jambo hilo kwa kusema: ‘Muendelee kuvumiliana na kusameheana kwa hiari [ao, kwa kupenda] ikiwa yeyote ana sababu ya kulalamika juu ya mwingine.’​—Wakolosai 3:13.

Kwa hiyo, ni wazi kwamba kusamehe ni sehemu ya maana ya upendo, wenye ni “kifungo kikamilifu cha muungano.” (Wakolosai 3:14) Kwa kweli, kulingana na adresi ya Internete ya Mayo Clinic, kusamehe kunafanya mutu . . .

  • Akuwe na urafiki wa muzuri pamoja na wengine, kutia ndani kusikia huruma, kuwa na utambuzi, na kujitia pa nafasi ya mutu mwenye alimukosea

  • Akuwe na afya ya muzuri ya akili na urafiki wa muzuri pamoja na Mungu

  • Apunguze mahangaiko na wasiwasi, na asikuwe na chuki

  • Akuwe na alama kidogo ya kushuka moyo

UJISAMEHE WEWE MWENYEWE. Kulingana na gazeti Disability & Rehabilitation, kujisamehe mwenyewe kunaweza kuwa “jambo lenye kuwa nguvu kabisa kufanya,” lakini “lenye kuwa la lazima zaidi ili kuwa na afya ya muzuri ya akili na ya kimwili.” Ni nini inaweza kukusaidia ujisamehe wewe mwenyewe?

  • Usitafute kuwa mukamilifu, lakini ukiwa na mawazo yenye kufaa, ukubali kuwa wewe​—kama vile tu watu wengine wote​—utafanya makosa.​—Mhubiri 7:20

  • Ujifunze kupitia makosa yako, hilo litasaidia usifanye tena makosa yaleyale

  • Ujivumilie wewe mwenyewe; makosa na tabia fulani za mubaya vinaweza kuchukua wakati ili kuisha.​—Waefeso 4:23, 24

  • Upitishe wakati pamoja na marafiki wenye kutiana moyo, wenye kuwa na mawazo yenye kufaa, na wenye kuwa wema lakini wenye watakuambia mambo waziwazi.​—Methali 13:20

  • Ikiwa unakosea mutu fulani, kubali kosa lako na ukuwe tayari kumuomba huruma. Ikiwa munafanya amani, utapata amani ya akili.​—Mathayo 5:23, 24

KANUNI ZA BIBLIA ZINASAIDIA KABISA!

Kisha kujifunza Biblia, Patricia, mwenye tulizungumuzia mwanzoni mwa habari hii, alijifunza kusamehe. Aliandika hivi: “Nimeachana na kasirani yenye iliharibisha maisha yangu. Siteseke tena, na sifanye watu wengine wateseke. Kanuni za Biblia zinaonyesha wazi kabisa kwamba Mungu anatupenda na anatutakia maisha ya muzuri.”

Mwanamume mumoja mwenye kuitwa Ron alisema: “Singeweza kuzuia mawazo na matendo ya watu wengine. Lakini ningeweza kuzuia mawazo na matendo yangu. Ikiwa nilipenda amani, nilipaswa kuachana na kinyongo. Nilianza kuona amani na kinyongo kama vile usiku na muchana. Singeweza kufanya mambo hayo mbili mara moja. Sasa niko na zamiri safi.”

a Chanzo cha habari: Adresi ya internete ya Mayo Clinic na ya Johns Hopkins Medecine na gazeti The Social Psychiatry and Psychiatric Epidemiology.

MAMBO YA MAANA

‘Muendelee kuvumiliana na kusameheana kwa hiari.’​—Wakolosai 3:13.

Kusamehe kunafanya mutu . . .

  • Akuwe na urafiki wa muzuri pamoja na wengine na akuwe na amani ya akili

  • Apunguze mahangaiko na wasiwasi, na asikuwe na chuki

  • Akuwe na afya ya muzuri ya kimwili, ya akili, na ya kiroho

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine