Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • g20 na. 2 uku. 6-7
  • 1. Mungu Njo Anatuleteaka Mateso?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • 1. Mungu Njo Anatuleteaka Mateso?
  • Amuka!—2020
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Juu ya Nini ni Muzuri Kujiuliza Vile?
  • Jambo la Kufikiria
  • Mambo Yenye Biblia Inasema
  • Habari Zenye Kuwa Ndani
    Amuka!—2020
  • Biblia Inasema Nini?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2017
  • Ulizo la 3: Sababu Gani Mungu Anaacha Niteseke?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Sababu Gani Mungu Anawaacha Watu Wateseke?
    Biblia Inafundisha Kabisa Nini?
Ona Habari Zaidi
Amuka!—2020
g20 na. 2 uku. 6-7
Padiri iko na Biblia mu kanisa wakati iko anazungumuza na wale wenye walifiwa.

1. Mungu Njo Anatuleteaka Mateso?

Juu ya Nini ni Muzuri Kujiuliza Vile?

Juu watu wengi wanamukataa Mungu sababu wanawaza kama yeye njo analeteaka watu mateso.

Jambo la Kufikiria

Viongozi wengi wa dini wanafundisha moja kwa moja ao kwa njia yenye haiko ya moja kwa moja kama Mungu njo anatuleteaka mateso. Kwa mufano, wamoja wanasema:

  • Misiba ya asili ni malipizi kutoka kwa Mungu.

  • Watoto wanakufa kwa sababu Mungu iko na lazima ya malaika wengine mbinguni.

  • Mungu anaunga mukono vita, yenye ni sababu kubwa ya mateso.

Inawezekana mambo yenye viongozi wa dini wanasema kumuhusu Mungu ikuwe ya uongo? Kama Mungu amekwisha kuwakataa, tunaweza kuamini mambo yenye wanasema?

IKIWA UNAPENDA KUJUA MINGI ZAIDI

Ona video Sababu Gani Ujifunze Biblia? yenye kuwa ku jw.org.

Mambo Yenye Biblia Inasema

Mungu hatuleteake mateso.

Kusema kama Mungu njo anatuleteaka mateso, kunapingana na mambo yenye Biblia inasema kuhusu sifa zake. Kwa mufano:

“Njia . . . zote [za Mungu] ni haki. . . . Yeye ni mwenye haki na munyoofu.”​—KUMBUKUMBU LA TORATI 32:4.

“Ni jambo lenye haliwezi kuwaziwa kwamba Mungu wa kweli atende uovu, na Mweza-Yote afanye makosa!”​—YOBU 34:10.

“Mweza-Yote hawezi kupotosha haki.”​—YOBU 34:12.

Mungu anakataa dini zenye kumusemea uongo.

Anakataa pia wale wenye wanafundisha kama yeye njo anatuleteaka mateso, na dini zenye kujiingiza katika vita na mambo ya jeuri.

“Manabii wanatoa unabii wa uongo katika jina langu [jina la Mungu]. Sikuwatuma wala kuwaamuru wala kusema nao. Maono ya uongo na . . . udanganyifu wa moyo wao wenyewe ndio unabii wenye wanawatolea ninyi.”​—YEREMIA 14:14.

Yesu alilaumu unafiki wa dini.

“Haiko kila mutu mwenye kuniambia, ‘Bwana, Bwana,’ ndiye ataingia katika Ufalme wenye kuwa mbinguni, lakini ni ule tu mwenye kufanya mapenzi ya Baba yangu mwenye kuwa mbinguni ndiye ataingia. Wengi wataniambia siku hiyo: ‘Bwana, Bwana, je, hatukutoa unabii katika jina lako, na kufukuza pepo wachafu katika jina lako, na kufanya matendo mengi yenye nguvu katika jina lako?’ Halafu nitawaambia: ‘Sikuwajua ninyi hata kidogo! Mutoke mbele yangu, ninyi wenye matendo ya kuvunja sheria!’”​—MATAYO 7:21-23.

Mungu njo anatuleteaka mateso?

Tufikirie baba mwenye anakomalisha watoto wake na anawatimizia mahitaji yao kulingana na uwezo wake. Kisha, mutoto mumoja mwanaume anaasi, anatoka kwao, na anachagua kuishi maisha ya upotovu ao ya raha. Tunaweza kusema kama ni baba njo alifanya mutoto wake achague maisha ya upotovu? Mutoto anaweza kusema kama ni baba njo anafanya apatwe na mambo ya mubaya yenye inamufikia? Vilevile, hatuwezi kusema kama Mungu njo anatuleteaka mateso.

Sasa, ile inamaanisha kama sisi njo tunajileteaka mateso?

Pata jibu kwenye ulizo la 2.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine