Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • g20 na. 2 uku. 8-9
  • 2. Sisi Njo Tunajileteaka Mateso?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • 2. Sisi Njo Tunajileteaka Mateso?
  • Amuka!—2020
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Juu ya Nini ni Muzuri Kujiuliza Vile?
  • Jambo la Kufikiria
  • Mambo Yenye Biblia Inasema
  • Biblia Inasema Nini?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2017
  • Habari Zenye Kuwa Ndani
    Amuka!—2020
  • Ulizo la 3: Sababu Gani Mungu Anaacha Niteseke?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • 4. Mungu Alituumba Juu Tuteseke?
    Amuka!—2020
Ona Habari Zaidi
Amuka!—2020
g20 na. 2 uku. 8-9
Mwanaume iko mu nyumba yake, iko na tumbako mu mukono moja na chupa ya pombe yenye kufunguliwa mu mukono ingine.

2 Sisi Njo Tunajileteaka Mateso?

Juu ya Nini ni Muzuri Kujiuliza Vile?

Juu kama jibu ni ndiyo, maana yake tunaweza kupunguza mateso yetu.

Jambo la Kufikiria

Ni kwa kiasi gani wanadamu wamefanya mambo yenye kuwa hapa chini iletee watu mateso?

  • Alama ya ngumi, yenye kuonyesha kutendewa mubaya.

    Kutendewa Mubaya.

    Shirika la Afya Ulimwenguni (OMS) linakadiria kama mutu muzima mumoja kati ya watu wazima ine alitendewa mubaya kimwili wakati alikuwa mutoto na kama mwanamuke mumoja kati ya wanamuke tatu amekwisha kutendewa mubaya kimwili ao kingono (ao hali zote mbili) katika maisha.

  • Alama ya majiwe ya makaburi.

    Kufiwa.

    Ripoti ya uchunguzi wa afya ya 2018 (World Health Statistics 2018), yenye ilitolewa na Shirika la Afya Ulimwenguni inasema: “Mauaji karibu 477000 ilitokea katika mwaka wa 2016.” Zaidi ya ile, inakadiriwa kuwa watu 180000 waliuawa katika vita na mapambano katika ule mwaka.

  • Alama ya moyo wenye kuwa na mistari ya kadiogramu, yenye kuonyesha matatizo ya afya.

    Matatizo ya Afya.

    Katika gazeti moja (The National Geographic magazine), muandikaji Fran Smith anasema: “Zaidi ya miliare moja ya watu wanavuta tumbako, na tumbako iko kati ya mambo yenye kufanya watu wapatwe na magonjwa tano yenye kuua sana: ugonjwa wa moyo, ugonjwa wa ubongo wenye kufanya sehemu fulani ya mwili ipooze, magonjwa yenye kushambulia njia ya kupumua, ugonjwa wenye kukawia wenye kufanya mutu apumue kwa shida, na kansere ya mapafu.”

  • Alama ya kilo chenye kuegemea upande mumoja, yenye kuonyesha ukosefu wa haki.

    Ukosefu wa haki.

    Mutu mumoja mwenye elimu ya mambo ya akili, Jay Watts, anasema: “Umaskini, watu kutendewa bila haki juu ya hali yao ya maisha, kubaguliwa, mutu kuzarauliwa juu tu iko mwanamuke, roho ya kushindana na kuwa mukimbizi, ile yote inafanya mahangaiko ya akili iongezeke.”

    IKIWA UNAPENDA KUJUA MINGI ZAIDI

    Angalia video Sababu Gani Mungu Aliumba Dunia? yenye kuwa ku jw.org.

Mambo Yenye Biblia Inasema

Mwanaume mwenye amekwisha kuonyeshwa analala ku kitanda cha hospitali. Bibi yake anageuka wakati munganga anatoa habari ya mubaya kuhusu afya ya bwana yake.

Mateso mingi yenye inapata wanadamu, inaletwa na wanadamu wao wenyewe.

Mingi kati ya ile mateso inaletwa na serikali zenye kutesa watu, ni kusema, serikali zenye kuliko kusaidia watu, zimefanya maisha yao ikuwe nguvu.

“Mwanadamu ametawala mwanadamu mwenzake ili kumuumiza.”​—MUHUBIRI 8:9.

Inawezekana kupunguza mateso.

Kanuni za Biblia zinasaidia watu wakuwe na afya ya muzuri na waishi na wengine kwa amani.

“Moyo mutulivu unapatia mwili uzima,lakini wivu unaozesha mifupa.”​—MEZALI 14:30.

“Muondoe kutoka kwenu kila namna ya uchungu wenye uovu, hasira, kasirani kali, kufoka, matukano, na kila jambo lenye kuumiza.”​—WAEFESO 4:31.

Sisi njo tunajileteaka mateso?

Biblia inasema: “Kitu chochote chenye mutu anapanda, ni kile atavuna pia.” (Wagalatia 6:7) Mateso fulani inaletwa na maamuzi yetu wenyewe. Njo maana wanganga wengi wanatia watu moyo kutumia chakula chenye kujenga, kufanya mazoezi, na kuepuka tabia za mubaya kama vile kuvuta tumbako. Lakini, hatuwezi kusema kama mateso yote inaletwa na wanadamu. Watu wengi wenye hawana kosa wanateseka kwa sababu ya aksidenti, misiba, na mambo ingine.

Juu ya nini watu wazuri wanateseka?

Pata jibu kwenye ulizo la 3.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine