Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • g21 na. 3 uku. 8-9
  • Mambo Yenye Wanasayansi Hawawezi Kutuambia

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Mambo Yenye Wanasayansi Hawawezi Kutuambia
  • Amuka!—2021
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Mwanasayansi wa Kiini-Tete Anaeleza Imani Yake
    Amuka!—2016
  • Sayansi na Maisha Yako
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Vitu Vyenye Uzima Vilianza Namna Gani?
    Furahia Maisha Milele!—Ujifunze Biblia kwa Njia ya Mazungumuzo
  • Uwasaidie Watoto Wako Wakuwe na Imani Yenye Nguvu Katika Muumbaji
    Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2017
Ona Habari Zaidi
Amuka!—2021
g21 na. 3 uku. 8-9
Mwalimu wa sayansi iko anazungumuza na wanafunzi wake fulani.

Mambo Yenye Wanasayansi Hawawezi Kutuambia

Inaonekanaka sawa vile wanasayansi walishakajifunza kila kitu juu ya ulimwengu. Lakini, kusema kweli, kuko maulizo mingi yenye hawawezi kujibia.

Wanasayansi walishakaonyesha namna ulimwengu na vitu vyenye uzima vilianzaka? Kwa kifupi jibu ni hapana. Watu fulani wanasema kama elimu fulani yenye kuitwa kosmolojia inaweza kutufasiria namna ulimwengu ulianzaka. Lakini, ona mambo yenye Marcelo Gleiser alisema. Yeye ni profesa wa mambo ya anga ku masomo ya Dartmouth, na anaamini kama haiwezekane kujua ikiwa Mungu anakuwaka ao hapana. Alisema hivi: “Hatuyawezaka hata kidogo kufasiria namna ulimwengu ulianzaka.”

Vilevile, habari moja mu gazeti Science News inasema hivi kuhusu namna vitu vyenye uzima vilianzaka: “Inaweza kuwa nguvu kujua namna vitu vyenye uzima vilianzaka ku Dunia, juu majiwe na vitu vingine vyenye tungeweza kuchunguza juu ya kutusaidia kujua namna mambo ilikuwaka wakati Dunia ilianza, vilishakapotea.” Ile maneno inaonyesha kama sayansi haiyawezaka kuonyesha namna ulimwengu na vitu vyenye uzima vilianzaka.

Lakini unaweza kujiuliza, ‘Kama vitu vyenye uzima vyenye kuwa mu dunia vilifanywa, nani njo alivifanya?’ Pengine pia ulishakajiuliza hii maulizo: ‘Kama kuko Muumbaji mwenye hekima na mwenye upendo, juu ya nini anaacha watu wenye aliumba wateseke? Juu ya nini anaacha watu wamuabudu mu njia mbalimbali zenye kutofautiana? Juu ya nini anaacha watu wenye kumuabudu wafanye mambo mingi ya mubaya?’

Sayansi peke yake haiwezi kujibia ile maulizo. Lakini ile haimaanishe kama hauwezi kupata majibu yenye kufaa. Kusema kweli, watu wengi walishakapata majibu yenye kufaa mu Biblia.

Ukipenda kujua juu ya nini wanasayansi fulani wenye walishakajifunza Biblia wanasema kuwa wanaamini kama kuko Muumbaji, fungua jw.org. Kwenye sehemu ya kutafutia, tafuta mavideo yenye kichwa: “Maoni Mbalimbali Kuhusu Mwanzo wa Uzima.”

Sayansi na Biblia Viliwasadikisha

Georgiy N. Koidan, mwanakemia

“Mara mingi, mu kazi yangu inaombaka ‘nichange’ vitu mbalimbali juu ya kufanya mamolekile. Na inaombaka nipange mbele ya wakati mambo yenye nitafanya juu ya kutengeneza ile mamolekile. Kama nakosa kufanya hata jambo moja tu, molekile yenye niko nafanya inaweza kuharibika. Ni kweli kazi yangu iko nguvu, lakini naionaka kuwa mwepesi wakati nailinganisha na mambo mingi sana na ya ajabu yenye inafanyikaka ndani ya chembe juu ya kutokeza molekile za ajabu. Ile inafanya niamini kama kunapaswa kuwa Mwanakemia (Chimiste) Mukubwa Sana, ni kusema, Muumbaji.

“Wakati nilijifunza Biblia, nilielewa kama haiko sawa vitabu vingine. Kazi ya kuandika Biblia ilimalizika kumepita miaka 2 000 hivi, lakini nawaza kama mashauri yenye kuwa mu Biblia ni yenye faida hata leo. Mambo yenye Biblia inasema juu ya kumaliza hali ya kukosa kuelewana kati ya watu wa familia, majirani, na kati ya watu wenye wanatumika pamoja, inaletaka tu matokeo ya muzuri. Nimefikia kutambua kama ni mutu mwenye iko na akili yenye inapita ya wanadamu njo mwenye anaweza kuleta ile mashauri yenye kutegemeka.”

Yan-Der Hsuuw, mutu mwenye kujifunzia kiini-tete

“Wakati kiini-tete iko nakomala, chembe zote zinapaswa kutumika pamoja juu chembe zingine zifanywe kuwa mishipa, mifupa, damu, na mambo ingine ya lazima ku mwili ya mwanadamu. Ni nguvu sana kuelewa namna kiini-tete inakomalaka. Vile ninaonaka, vitu vyenye uzima vinapaswa kuwa vilitoka kwa mutu fulani mwenye kuwa na akili.

“Namna Biblia inafasiria mu Zaburi 139:15, 16 vile kiini-tete inakomalaka mu tumbo ya mama, inafanana na mambo yenye wanasayansi wamevumbula mu miaka kidogo yenye imepita. Namna gani mwandikaji wa ile zaburi angeweza kusema tangu zamani na bila kukosea, namna kiini-tete inakomalaka mu tumbo ya mama, kama haiko Muumbaji njo alimuambiaka aandike vile?”

Angalia video Rocío Picado Herrero: Mwalimu wa Kemia Anafasiria Imani Yake. Utafute ile video ku jw.org.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine