Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • rq somo 7 uku. 14-15
  • Kumukaribia Mungu Karibu Katika Sala

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Kumukaribia Mungu Karibu Katika Sala
  • Mungu Anataka Nini Kwetu?
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Sala Ni Zawadi Kutoka kwa Mungu
    Biblia Inatufundisha Nini?
  • Go Rapela Modimo go Nyoko go Šutetsa Thina Naye
    Furahia Maisha Milele!—Ujifunze Biblia kwa Njia ya Mazungumuzo
  • Namna ya Kumukaribia Mungu Katika Sala
    Biblia Inafundisha Kabisa Nini?
  • Sehemu ya 11
    Umusikilize Mungu
Ona Habari Zaidi
Mungu Anataka Nini Kwetu?
rq somo 7 uku. 14-15

Somo 7

Kumukaribia Mungu Karibu Katika Sala

Kwa nini ni lazima kusali kwa ukawaida? (1)

Tunapaswa kusali kwa nani, na namna gani? (2, 3)

Mambo gani yanayofaa kutiwa katika sala? (4)

Unapaswa kusali wakati gani? (5, 6)

Je! Mungu anasikiliza sala zote? (7)

1. Sala ni kuzungumuzia Mungu kwa unyenyekevu. Unapaswa kusali kwa Mungu kwa ukawaida. Kwa kufanya hivyo utaweza kujisikia kuwa karibu naye kama kuwa karibu ya rafiki unayemupenda sana. Yehova ni mukuu zaidi na mwenye nguvu sana, hata hivyo yeye anasikiliza sala zetu! Je! wewe unasali kwa Mungu kwa ukawaida?​—⁠Zaburi 65:2; 1 Watesalonika 5:⁠17.

2. Sala ni sehemu ya ibada yetu. Kwa hiyo, tunapaswa kusali kwa Mungu pekee, Yehova. Yesu alipokuwa duniani, siku zote alisali kwa Baba yake, na si kwa mutu mwingine yeyote. Tunapaswa kufanya hivyo hivyo. (Matayo 4:10; 6:⁠9) Lakini, sala zetu zote zinapaswa kusemwa katika jina la Yesu. Jambo hilo linaonyesha kwamba tunaheshimu cheo cha Yesu na kwamba sisi tuna imani katika zabihu yake ya ukombozi.​—⁠Yoane 14:6; 1 Yoane 2:​1, 2.

3. Tunaposali tunapaswa kusema kwa Mungu yale yanayotoka moyoni. Sala tunazosema zisiwe zile zinazopangwa katika ufahamu au kuzisoma katika kitabu cha sala. (Matayo 6:​7, 8) Tunaweza kusali tukiwa katika kikao chochote chenye heshima, haizuru wakati gani, na mahali popote. Mungu anaweza kusikia hata sala zinazosemwa kimya kimya katika moyo wetu. (1 Samweli 1:​12, 13) Ni vizuri kutafuta mahali pa kimya mbali na watu wengine ili kusema sala zetu za kipekee.​—⁠Marko 1:⁠35.

4. Unaweza kusali kwa ajili ya mambo gani? Jambo lolote linaloweza kugusia urafiki wako naye. (Wafilipi 4:​6, 7) Ile sala ya kielelezo inaonyesha kwamba tunapaswa kusali kwa ajili ya jina la Yehova na kusudi lake. Tunaweza pia kuomba ili tupewe mahitaji yetu ya kimwili, ili zambi zetu zisamehewe, pia ili tupewe musaada kushindana na jaribu. (Matayo 6:​9-13) Sala zetu hazipaswi kuwa za ubinafsi (uchoyo). Tunapaswa tu kusali juu ya mambo yanayopatana na mapenzi ya Mungu.​—⁠1 Yoane 5:⁠14.

5. Unaweza kusali wakati wowote ule moyo wako unakusukuma kusema asante au kumusifu Mungu. (1 Mambo ya Siku 29:​10-13) Unapaswa kusali wakati una magumu na wakati imani yako inakuwa yenye kujaribiwa. (Zaburi 55:22; 120:⁠1) Ni jambo lenye kufaa kusali mbele ya kula chakula chako. (Matayo 14:19) Yehova anatualika sisi kusali “kwa kila wakati.”​—⁠Waefeso 6:⁠18.

6. Tuna lazima ya kusali hasa ikiwa tumefanya zambi nzito. Kwa wakati kama huo tunapaswa kumulilia Yehova kwa kuomba rehema yake na musamaha wake. Tukiungama zambi zetu kwake na kufanya kabisa kadiri tuwezavyo ili tusizirudilie, Mungu ni “tayari kusamehe.”​—⁠Zaburi 86:5; Mezali 28:⁠13.

7. Yehova anasikiliza tu sala za watu wenye haki. Ili sala zako zisikilizwe na Mungu, unapaswa kujaribu kuishi kulingana na sheria zake kadiri unavyoweza. (Mezali 15:29; 28:⁠9) Unapaswa kuwa munyenyekevu unaposali. (Luka 18:​9-14) Una lazima ya kufanya nguvu ili utende kulingana na yale unayosema katika sala. Kwa kufanya hivyo utaonyesha kwamba una imani na kwamba wewe ni mwenye kukusudia yale unayosema. Ni kwa kufanya hivyo peke yake kwamba Yehova atajibu sala zako.​—⁠Waebrania 11:⁠6.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine