Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • rq somo 16 uku. 31
  • Uamuzi Wako Kumutumikia Mungu

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Uamuzi Wako Kumutumikia Mungu
  • Mungu Anataka Nini Kwetu?
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Uko Tayari Kubatizwa?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2020
  • Ubatizo Ni Hatua Inayomuongoza Mutu Kwenye Uhusiano Muzuri Pamoja na Mungu
    Biblia Inafundisha Kabisa Nini?
  • Ninapaswa Kutoa Maisha Yangu kwa Mungu na Kubatizwa?
    Biblia Inatufundisha Nini?
  • Vijana—Muko Tayari kwa Ajili ya Ubatizo?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2016
Ona Habari Zaidi
Mungu Anataka Nini Kwetu?
rq somo 16 uku. 31

Somo 16

Uamuzi Wako Kumutumikia Mungu

Unapaswa kufanya nini ili uwe rafiki ya Mungu? (1, 2)

Namna gani unaweza kujiweka wakfu kwa Mungu? (1)

Ungepaswa kubatizwa wakati gani? (2)

Namna gani unaweza kupata nguvu ya kubaki mwaminifu kwa Mungu? (3)

1. Ili uwe rafiki ya Mungu, unapaswa kupata ujuzi muzuri wa kweli ya Biblia (1 Timoteo 2:​3, 4), kutia imani katika mambo umejifunza (Waebrania 11:⁠6), kutubu zambi zako (Matendo 17:​30, 31), na kugeuka katika mwendo wa maisha yako. (Matendo 3:19) Ndipo upendo wako kwa Mungu ungepaswa kukusukuma kujiweka wakfu mwenyewe kwake. Hilo lamaanisha kwamba katika sala yako mwenyewe, peke yako unamwelezea kwamba unajitoa mwenyewe kwake ili kufanya mapenzi yake.​—⁠Matayo 16:24; 22:⁠37.

2. Baada ya kuwa umefanya wakfu wako kwa Mungu, yakupasa ubatizwe. (Matayo 28:​19, 20) Ubatizo unamufanya kila mutu ajue kwamba umejiweka wakfu mwenyewe kwa Yehova. Hivyo ubatizo ni kwa ajili ya wale watu wazima vya kutosha ambao wanaweza kufanya uamuzi wa kumutumikia Mungu. Wakati mutu anapobatizwa, mwili wake wote unapaswa kuingizwa ndani ya maji kwa muda.a​—⁠Marko 1:​9, 10; Matendo 8:⁠36.

3. Kisha kujiweka wakfu, Yehova atakutazamia uishi kulingana na ahadi yako. (Zaburi 50:14; Muhubiri 5:​4, 5) Ibilisi atajaribu kukuzuia usimutumikie Yehova. (1 Petro 5:⁠8) Basi umukaribie Mungu karibu katika sala. (Wafilipi 4:​6, 7) Jifunze Neno lake kila siku. (Zaburi 1:​1-3) Shikamana sana na kutaniko. (Waebrania 13:17) Kwa kufanya hayo yote, utapata nguvu ya kubaki mwaminifu kwa Mungu. Kwa umilele wote unaweza hivyo kufanya mambo ambayo Mungu anataka kwako!

[Maelezo ya Chini]

a Funzo la kitabu Biblia Inafundisha Nini Hasa?, au kitabu kingine kama hicho kilichotolewa na Mashahidi wa Yehova, kinapendekezwa katika kujitayarisha kuhusu ubatizo.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine