Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • ll sehemu 5 uku. 12-13
  • Garika Kubwa—Ni Nani Walimusikiliza Mungu? Ni Nani Hawakumusikiliza?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Garika Kubwa—Ni Nani Walimusikiliza Mungu? Ni Nani Hawakumusikiliza?
  • Umusikilize Mungu ili Uishi Milele
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Safina ya Noa
    Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
  • Sehemu ya 5
    Umusikilize Mungu
  • “Alitembea Pamoja na Mungu wa Kweli”
    Tuige Imani Yao
  • Noa “Alitembea Pamoja na Mungu wa Kweli”
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
Ona Habari Zaidi
Umusikilize Mungu ili Uishi Milele
ll sehemu 5 uku. 12-13

SEHEMU YA 5

Garika Kubwa—Ni Nani Walimusikiliza Mungu? Ni Nani Hawakumusikiliza?

Watu wengi wenye waliishi wakati wa Noa walikuwa wanafanya mambo ya mubaya. Mwanzo 6:5

Malaika wabaya wenye kuvaa miili ya watu wako pamoja na wanamuke

Adamu na Eva walizaa watoto, na watu wakakuwa wengi ku dunia. Kisha wakati fulani, malaika fulani walijitia ngambo ya Shetani, ili kumupinga Mungu.

Walikuja ku dunia, wakavaa miili ya watu ili waweze kuoa wanamuke. Wale wanamuke walizaa watoto wenye walikuwa na nguvu mingi kupita watu wengine na walikuwa wabaya sana.

Mwanamuke mumoja anakamata mutoto mudogo wakati mutoto mwanaume anamupiga; Wanefili, watoto wanaume wenye malaika wabaya walizaa, wanafanya mambo ya mubaya

Ku dunia kulijaa watu wenye walikuwa wanafanya mambo ya mubaya. Biblia inasema hivi: “Uovu wa mwanadamu ulikuwa mwingi juu ya dunia na kila muelekeo wa mawazo ya moyo wake ulikuwa tu mubaya wakati wote.”

Noa alimusikiliza Mungu na akajenga safina. Mwanzo 6:​13, 14, 18, 19, 22

Noa anamusikiliza Mungu

Noa alikuwa mutu muzuri. Yehova alimuambia kama ataua watu wabaya kwa kutumia garika kubwa (mvua ya mingi sana).

Noa na familia yake wanajenga safina

Tena Mungu alimuambia Noa ajenge mashua kubwa sana; mashua hiyo iliitwa safina. Na alimuambia aingize ndani ya mashua hiyo, familia yake na kila namna ya munyama.

Noa anatolea watu angalisho juu ya Garika yenye kuwa karibu, lakini watu wanamuchekelea

Noa alitolea watu angalisho juu ya Garika yenye ilikuwa karibu kuja, lakini hawakumusikiliza. Watu fulani walimuchekelea Noa na wengine walimuchukia.

Noa na familia yake wanakusanya wanyama ili kuwaingiza ndani ya safina

Wakati Noa alimaliza kujenga safina, aliingiza wanyama ndani.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine