Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • od sura 6 uku. 53-58
  • Watumishi wa Huduma Wanafanya Kazi ya Maana

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Watumishi wa Huduma Wanafanya Kazi ya Maana
  • Tengenezo Yenye Kufanya Mapenzi ya Yehova
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • SIFA ZENYE KUWA MU MAANDIKO ILI KUWA MUTUMISHI WA HUDUMA
  • NAMNA WANATUMIKIA KUTANIKO
  • Watumishi wa Huduma Wanafanyaka Kazi Gani?
    Ni Nani Wanafanya Mapenzi ya Yehova Leo?
  • Watumishi wa Huduma Hutoa Utumishi Wenye Thamani
    Huduma Yetu ya Ufalme—1999
  • Ndugu​—⁠Muko Najikaza juu Mufikie Kuwa Watumishi wa Huduma?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2024
  • Onyesha Shukrani Juu ya “Zawadi Katika Wanadamu”
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2024
Ona Habari Zaidi
Tengenezo Yenye Kufanya Mapenzi ya Yehova
od sura 6 uku. 53-58

SURA YA 6

Watumishi wa Huduma Wanafanya Kazi ya Maana

MUTUME Paulo aliandika hivi mu barua yenye aliandikia kutaniko ya Filipi: “Paulo na Timoteo, watumwa wa Kristo Yesu, kwa watakatifu wote katika umoja na Kristo Yesu wenye kuwa katika Filipi, pamoja na waangalizi na watumishi wa huduma.” (Flp. 1:1) Andiko inaonyesha kama Paulo alisalimia pia watumishi wa huduma. Ni wazi kama wale wanaume walitimiza daraka ya maana ili kusaidia wazee wa kutaniko ile wakati. Na leo pia ni vile. Watumishi wa huduma, wanafanya kazi mbalimbali ili kusaidia waangalizi; na ile inasaidia kukuwe utaratibu mu kutaniko.

2 Unajua watumishi wa huduma wa mu kutaniko yako? Unajua kazi zenye wanafanyaka kwa faida yako na kwa faida ya kutaniko yote? Bila shaka, Yehova anapendezwa na kazi ya bidii yenye wale wanaume wanafanyaka. Paulo aliandika hivi: “Wanaume wenye kutumikia muzuri wanajipatia wenyewe sifa ya muzuri na uhuru mwingi wa kusema katika imani yenye kuwa katika Kristo Yesu.”​—1 Ti. 3:13.

SIFA ZENYE KUWA MU MAANDIKO ILI KUWA MUTUMISHI WA HUDUMA

3 Watumishi wa huduma wanapaswa kuwa na mwenendo wa muzuri mu maisha yao ya Kikristo, wanapaswa kuwa wanaume wenye kutumainika, na wenye kutimiza muzuri kazi zao mu kutaniko. Ile inaonekana wazi wakati tunafikiria maneno ya Paulo yenye aliandikia Timoteo kuhusu sifa za watumishi wa huduma. Alisema hivi: “Vilevile watumishi wa huduma wanapaswa kuchukua mambo kwa uzito, wasikuwe na ndimi mbili, wasikuwe wenye kunywa divai nyingi, wasikuwe na pupa ya faida yenye haiko ya haki, wakuwe wenye kushika siri takatifu ya imani kwa zamiri safi. Pia, wanapaswa kujaribiwa kwanza ili kujua kama wanafaa; kisha watumike wakiwa watumishi, kwa kuwa hawana shitaka. Mutumishi wa huduma anapaswa kuwa bwana wa bibi mumoja, na mwenye kusimamia muzuri watoto wake na nyumba yake mwenyewe.” (1 Ti. 3:8-10, 12) Wakati watumishi wa huduma wanatimiza zile sifa za juu zenye kuombwa na Maandiko, ile inalinda kutaniko isishitakiwe kama imepatia madaraka ya pekee wanaume wenye hawastahili.

4 Watumishi wa huduma wote, ikuwe vijana ao wazee, wanahubiri kwa bidii kila mwezi. Wanamuiga Yesu kwa kuwa na bidii mu kazi ya kuhubiri. Ile bidii inaonyesha kama wanamuiga Yehova mwenye anapenda watu wote waokolewe.​—Isa. 9:7.

5 Watumishi wa huduma ni mifano ya muzuri mu kuvala, kujipamba, kusema, mu mwenendo, na mu roho yenye wanaonyesha. Wako na akili ya muzuri, na ile inafanya wengine wawaheshimie. Zaidi ya ile, wanakamata kwa uzito uhusiano wao pamoya na Yehova na mapendeleo ya utumishi yenye wako nayo mu kutaniko.​—Tit. 2:2, 6-8.

6 Wale wanaume ‘wamejaribiwa kwanza ili kujua kama wanafaa.’ Hata mbele wawekwe kuwa watumishi wa huduma, walionyesha kabisa kama ni wanaume wenye walijitoa kwa Yehova. Wameonyesha kama wanatia faida za Ufalme pa nafasi ya kwanza mu maisha yao, na wako najikaza kufikia pendeleo yoyote ya utumishi yenye wanaweza kupewa. Kwa kweli, wale wanaume ni mifano ya muzuri yenye wengine wanaweza kuiga mu kutaniko.​—1 Ti. 3:10.

NAMNA WANATUMIKIA KUTANIKO

7 Watumishi wa huduma, wanafanya kazi mbalimbali kwa faida ya ndugu na dada zao. Ile inasaidia waangalizi wakuwe na wakati mingi ya kufanya kazi ya kufundisha na kazi ya uchungaji. Baraza ya wazee inapatia kila mutumishi wa huduma kazi ya kufanya kulingana na uwezo wake na kulingana na mahitaji ya kutaniko.

Watumishi wa huduma wanafanya kazi mbalimbali, ile inasaidia waangalizi wakuwe na wakati mingi ya kufanya kazi ya kufundisha na kazi ya uchungaji

8 Tuone sasa kazi mbalimbali za watumishi wa huduma: Mutumishi wa huduma anaweza kupewa kazi ya kushugulikia vichapo ili tupate vichapo vya kujifunza na vya kutumia mu mahubiri. Wengine wanaweza kupewa kazi ya kushugulikia konte ya kutaniko ao kuchunga fishe za eneo. Watumishi wa huduma fulani, wanapewa kazi ya kupitisha mikro, kutumika ku audio-video, na wengine wanafanya kazi ya kukaribisha watu ku mikutano na kusaidia wazee mu mambo ingine. Juu kuko kazi mingi zenye zinapaswa kufanywa ili kutunza Jumba ya Ufalme na kuifanya iendelee kuwa safi, mara mingi watumishi wa huduma wanaombwa kusaidia mu zile kazi.

9 Mu makutaniko fulani, inawezekana kila mutumishi wa huduma apewe kazi yake. Mu makutaniko ingine, mutumishi wa huduma anaweza kupewa zaidi ya kazi moya. Mu hali fulani, kazi moya inaweza kufanywa na watumishi wa huduma wengi. Kama hakuna watumishi wa huduma wengi ili kufanya zile kazi, baraza ya wazee inaweza kukamata mipango ili ndugu wenye kubatizwa, wenye kuwa mifano ya muzuri, wasaidie kufanya zile kazi za maana. Kufanya vile, itasaidia wale ndugu wapate uzoefu wenye utawasaidia wakati watastahili kuwa watumishi wa huduma. Kama hakuna ndugu mwenye anaweza kusaidia, wazee wanaweza kuomba dada mwenye kuwa mufano muzuri, asaidie mu mambo fulani hata kama hawezi kuwekwa kuwa mutumishi wa huduma. Mutu mwenye kuwa mufano muzuri ni Mukristo mwenye wengine wanaweza kuiga mwenendo wake na namna yake ya kumuabudu Mungu. Iko mufano muzuri mu mambo kama vile kuhuzuria mikutano, kuhubiri, maisha yake ya familia, namna yake ya kujifurahisha, kuvala na kujipamba, na mu mambo ingine.

10 Mu makutaniko yenye kuwa na wazee kidogo sana, watumishi wa huduma wenye kustahili wanaweza kuombwa wachunguze na wale wenye watabatizwa, maulizo yenye inahusu mafundisho ya Biblia. Ile maulizo inapatikana mu Nyongeza, “Sehemu ya 1: Mambo Yenye Mukristo Anaamini.” Juu “Sehemu ya 2: Maisha ya Mukristo,” inazungumuzia mambo ya kipekee sana ya mutu, ni muzee njo anapaswa kuichunguza.

11 Kama wazee wanaona kuwa kuko sababu ya muzuri ya kukuwa nabadilisha kazi fulani za watumishi wa huduma, wanaweza kufanya vile. Lakini, kuko faida kubwa kuwaacha wafanye kazi ileile kwa muda fulani juu waizoee na waijue muzuri zaidi.

12 Kulingana na hali ya kutaniko, watumishi wa huduma wanaweza kupewa migawo ingine ikiwa maendeleo yao ‘inaonekana wazi kwa watu wote.’ (1 Ti. 4:15) Kama kuko wazee kidogo, mutumishi wa huduma anaweza kuwekwa kuwa musaidizi wa mwangalizi wa kikundi, ao mu hali fulani, anaweza kuwa mutumishi wa kikundi, lakini atafanya ile kazi kwa kufuata muongozo wa wazee. Watumishi wa huduma wanaweza kupewa migao fulani ku Mukutano Utumishi na Maisha, wanaweza pia kuongoza Funzo ya Biblia ya Kutaniko kama ni lazima, na wanaweza kutoa hotuba za watu wote. Watumishi wa huduma wanaweza pia kupewa mapendeleo ingine mu kutaniko kama kuko uhitaji wa pekee, na kama wanastahili kutimiza ile migawo. (1 Pe. 4:10) Wakati wanasaidia wazee, watumishi wa huduma wanapaswa kujitoa kwa kujipendea.

13 Hata kama kazi za watumishi wa huduma ziko tofauti na za wazee, zile kazi ni sehemu ya utumishi mutakatifu wenye wanamutolea Mungu na ni za lazima juu kutaniko iendelee kutumika muzuri. Kisha muda fulani, kama watumishi wa huduma wanafanya muzuri kazi zao na kama wanastahili kuwa wachungaji na walimu mu kutaniko, wanaweza kupendekezwa kuwa wazee.

14 Kama uko ndugu na ungali kijana ao umebatizwa hivi karibuni, uko najikaza kutimiza sifa zenye kuombwa ili kuwa mutumishi wa huduma? (1 Ti. 3:1) Juu watu wengi wako nakuya mu kweli kila mwaka, tengenezo iko na lazima ya wanaume wenye kustahili kiroho ili watumikie madaraka mbalimbali mu kutaniko. Unaweza kujikaza kufikia mapendeleo kwa kukomalisha tamaa ya kusaidia wengine. Njia moya ya kufanya vile ni kufikiri sana juu ya mufano muzuri wa Yesu. (Mt. 20:28; Yoh. 4:6, 7; 13:4, 5) Tamaa yako itaongezeka kadiri unapata furaha ya kutumikia wengine. (Mdo. 20:35) Kwa hiyo, ujitolee ili kusaidia wengine, usaidie mu kazi ya kutunza Jumba ya Ufalme, na unaweza pia kujitolea kufanya kipindi ya mwanafunzi mwenye hakufika ku Mukutano Utumishi na Maisha. Ndugu mwenye anajikaza kufikia mapendeleo anapaswa pia kukomalisha sifa za kiroho kwa kufanya funzo ya kipekee kwa ukawaida. (Zb. 1:1, 2; Gal. 5:22, 23) Zaidi ya ile, ndugu mwenye kujikaza kufikia mapendeleo, anaonyesha kama ni mwenye kutumainika na ni muaminifu, wakati anapewa kazi fulani mu kutaniko.​—1 Ko. 4:2.

15 Watumishi wa huduma wanawekwa na roho takatifu kwa faida ya kutaniko. Ndugu na dada wote mu kutaniko, wanaweza kuonyesha shukrani yao kwa kazi ya bidii yenye watumishi wa huduma wanafanya kwa kuwaunga mukono wakati wanatimiza kazi zao mbalimbali. Wakati wanafanya vile, wanaonyesha kama wanamushukuru Yehova juu ya mupango wake wa kufanya kutaniko iendelee kuwa na utaratibu.​—Gal. 6:10.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine