SURA YA 3
Mungu Anapenda Wanadamu Wakuwe na Maisha ya Namna Gani?
1. Mungu iko na kusudi gani juu ya wanadamu?
MUNGU iko na kusudi la muzuri sana juu ya wanadamu. Aliumba Adamu na Eva, mwanaume na mwanamuke, ili waishi mu bustani ao shamba lenye kupendeza sana. Alipenda wazae watoto, wafanye dunia yote ikuwe paradiso, na kuhangaikia wanyama.—Mwanzo 1:28; 2:8, 9, 15; ona Mafasirio Ingine ya 6.
2. (a) Ni nini inaonyesha kama Mungu atatimiza mambo yenye alikusudia? (b) Biblia inasema kama ni nani wataishi milele mu dunia?
2 Unawaza kama siku moja tutaishi mu paradiso? Yehova anatuambia hivi: “Nimekusudia, na pia nitalitimiza.” (Isaya 46:9-11; 55:11) Kwa kweli, atafanya mambo yenye alikusudia, na hakuna kitu chenye kitamuzuia. Yehova anasema kama aliumba dunia kwa kusudi fulani. “Hakuiumba tu bila sababu.” (Isaya 45:18) Anapenda watu waishi mu dunia yote. Mungu anapenda watu wa namna gani waishi mu dunia, na kwa muda gani? Biblia inasema hivi: “Wenye haki [ao, wenye kumutii Mungu] watariti dunia na wataishi milele juu yake.”—Zaburi 37:29; Ufunuo 21:3, 4.
3. Wakati unaona wanadamu wanagonjwa na kufa, unaweza kujiuliza ulizo gani?
3 Lakini, leo watu wanagonjwa na wanakufa. Mu maeneo ya mingi, watu wanapigana na kuuana. Kwa kweli, Mungu hakupenda mambo yakuwe vile. Kwa hiyo, ni nini ilitokea, na juu ya nini? Biblia tu njo inaweza kutuambia.
ADUI YA MUNGU
4, 5. (a) Ni nani alizungumuza na Eva kupitia nyoka? (b) Namna gani mutu muzuri anaweza kugeuka na kuwa mwizi?
4 Biblia inasema kama Mungu iko na adui mwenye “kuitwa Ibilisi na Shetani.” Shetani alitumia nyoka ili kuzungumuza na Eva mu bustani ya Edeni. (Ufunuo 12:9; Mwanzo 3:1) Alifanya ionekane kama vile nyoka alikuwa anasema.—Ona Mafasirio Ingine ya 7.
5 Sasa, Mungu aliumba Shetani Ibilisi? Hapana! Wakati Mungu alikuwa anaumba dunia kwa ajili ya Adamu na Eva, kulikuwa malaika wengi mbinguni. Mumoja kati yao aligeuka na kuwa Ibilisi. (Yobu 38:4, 7) Jambo hilo liliwezekana namna gani? Wazia mufano huu: Namna gani mutu muzuri anaweza kugeuka na kuwa mwizi? Hakukuwa mwizi wakati alizaliwa. Lakini, anatamani kitu chenye hakiko chake. Anaendelea kuwaza juu ya kitu hicho, na tamaa yake ya mubaya inakuwa yenye nguvu sana. Kisha, wakati anapata nafasi anaiba kitu hicho. Amejifanya yeye mwenyewe kuwa mwizi.—Soma Yakobo 1:13-15; ona Mafasirio Ingine ya 8.
6. Namna gani malaika mumoja aligeuka na kuwa adui ya Mungu?
6 Mambo yalikuwa vile juu ya ule malaika. Kisha Yehova kuumba Adamu na Eva, aliwaambia wazae watoto na ‘kujaza dunia.’ (Mwanzo 1:27, 28) Pengine ule malaika aliwaza hivi: ‘Watu hao wote wanaweza kuniabudu mimi kuliko kumuabudu Yehova!’ Kadiri aliendelea kuwaza juu ya jambo hilo, alitamani sana jambo lenye lilikuwa la Yehova. Ule malaika alipenda watu wamuabudu. Kwa hiyo, alimuambia Eva mambo ya uongo, na akamudanganya. (Soma Mwanzo 3:1-5.) Wakati alifanya vile, aligeuka na kuwa Shetani Ibilisi, adui ya Mungu.
7. (a) Juu ya nini Adamu na Eva walikufa? (b) Juu ya nini tunazeeka na kufa?
7 Adamu na Eva hawakumutii ao kumusikia Mungu na wakakula lile tunda. (Mwanzo 2:17; 3:6) Walimutendea Yehova zambi, na kisha wakafikia kufa, kama vile tu Yehova alikuwa amesema. (Mwanzo 3:17-19) Watoto wa Adamu na Eva walikuwa pia watenda-zambi; kwa hiyo, walikufa. (Soma Waroma 5:12.) Ili uelewe sababu gani watoto wa Adamu na Eva walikuwa pia watenda-zambi, wazia mufano huu: Unapikia mikate mu chombo chenye kuwa na alama fulani. Mikate hiyo itakuwa pia na alama hiyo. Wakati Adamu alikosa kumutii Mungu, akakuwa mutenda-zambi. Kwa sababu tuko watoto wa Adamu, sisi wote ni watenda-zambi, ao tuko na “alama” ileile yenye alikuwa nayo. Na kwa sababu sisi wote tuko watenda-zambi, tunazeeka na kufa.—Waroma 3:23; ona Mafasirio Ingine ya 9.
8, 9. (a) Shetani alipenda Adamu na Eva waamini nini? (b) Juu ya nini Yehova hakuua wapinzani hao palepale?
8 Shetani alianzisha upinzani juu ya Yehova wakati alichochea Adamu na Eva wakose kumutii Mungu. Alipenda Adamu na Eva waamini kama Yehova ni musema-uongo na ni mutawala mubaya mwenye hakuwatakia mambo ya muzuri. Shetani alisema kama wanadamu hawakukuwa na lazima ya kuongozwa na Mungu. Tena, alisema kama Adamu na Eva wanapaswa kuamua wao wenyewe mambo ya muzuri na ya mubaya. Kwa hiyo, Yehova angefanya nini? Angeweza kuua wapinzani hao na kumaliza uasi huo. Lakini, kufanya vile kungeonyesha kama Shetani ni musema-uongo? Hapana.
9 Kwa hiyo, Yehova hakuua wapinzani hao palepale. Lakini, aliachia wanadamu wakati ili wajitawale wao wenyewe. Hilo lingeonyesha wazi kama Shetani ni musema-uongo na kama Yehova anajua mambo yenye kuwa ya muzuri kwa wanadamu. Tutajifunza mambo mingi juu ya jambo hilo mu Sura ya 11. Lakini, uko na mawazo gani juu ya uamuzi wa Adamu na Eva? Je, walifanya muzuri wakati walimusikiliza Shetani na kukosa kumutii Mungu? Yehova njo alikuwa amepatia Adamu na Eva kila kitu chenye walikuwa nacho. Aliwapatia uzima mukamilifu, makao yenye kupendeza, na kazi yenye walifurahia. Lakini Shetani hakukuwa amewafanyia hata jambo moja la muzuri. Kama ulikuwa pale, wewe ungefanya nini?
10. Kila mumoja wetu anapaswa kukamata uamuzi gani wa maana?
10 Leo, kila mumoja wetu anapaswa pia kukamata uamuzi, na uzima wetu unategemea uamuzi huo. Tunaweza kumuchagua Yehova kuwa Mutawala wetu na kumutii, na kusaidia kuonyesha kama Shetani ni musema-uongo. Ao tunaweza kuchagua Shetani kuwa mutawala wetu. (Zaburi 73:28; soma Mezali 27:11.) Mu dunia hii, ni watu kidogo sana njo wanamutii Mungu. Kwa kweli, Mungu haiko mutawala wa dunia. Sasa kama haiko Mungu njo anatawala ulimwengu, mutawala wa ulimwengu ni nani?
NI NANI ANATAWALA ULIMWENGU?
Kama falme zote za ulimwengu hazikukuwa za Shetani, angeahidi Yesu kama atamupatia falme hizo?
11, 12. (a) Shetani alimutolea Yesu nini? Na hilo linatufundisha nini? (b) Ni maandiko gani yenye kuonyesha kama Shetani njo mutawala wa ulimwengu?
11 Yesu alijua kabisa mutawala wa ulimwengu ao dunia ni nani. Wakati fulani, Shetani ‘alimuonyesha falme zote za ulimwengu na utukufu wa falme hizo.’ Kisha Shetani akamuambia Yesu hivi: “Nitakupatia vitu hivi vyote ukianguka chini [ao, ukiinama] na kunifanyia tendo la ibada.” (Matayo 4:8, 9; Luka 4:5, 6) Ujiulize hivi: ‘Kama falme hizo hazikukuwa za Shetani, angeahidi Yesu kama atamupatia falme hizo?’ Hapana. Serikali ao guvernema zote ni za Shetani.
12 Unaweza kujiuliza hivi: ‘Namna gani Shetani anaweza kuwa mutawala wa ulimwengu? Je, haiko Yehova Mungu Mweza-Yote njo aliumba ulimwengu wote?’ (Ufunuo 4:11) Ndiyo ni yeye, lakini Yesu aliita Shetani waziwazi kuwa “mutawala wa ulimwengu huu.” (Yohana 12:31; 14:30; 16:11) Mutume Paulo aliita Shetani Ibilisi “mungu wa mupangilio huu wa mambo.” (2 Wakorinto 4:3, 4) Na mutume Yohana aliandika kama “ulimwengu muzima unakaa katika nguvu za ule muovu.”—1 Yohana 5:19.
ULIMWENGU WA SHETANI UTAHARIBIWA NAMNA GANI?
13. Juu ya nini tuko na lazima ya ulimwengu mupya?
13 Ulimwengu huu unaendelea kuwa hatari zaidi. Tunaona kila mahali vita, rushwa (ao kata-midomo), unafiki, na jeuri. Wanadamu hawawezi kumaliza magumu hayo yote, hata kama wanajikaza sana. Lakini, karibuni Mungu ataharibu ulimwengu huu muovu kwenye vita yake ya Armagedoni. Na kisha ataleta ulimwengu mupya wenye haki.—Ufunuo 16:14-16; ona Mafasirio Ingine ya 10.
14. Mungu amechagua nani ili akuwe Mufalme wa Ufalme wake? Biblia ilitabiri nini juu ya Yesu?
14 Yehova alichagua Yesu Kristo ili akuwe Mufalme wa serikali ao Ufalme wake wa mbinguni. Maelfu ya miaka yenye imepita, Biblia ilitabiri kama Yesu angetawala akiwa “Mukubwa wa Amani” na kama ufalme wake haungekuwa na mwisho. (Isaya 9:6, 7) Yesu alifundisha wanafunzi wake wasali kwa ajili ya serikali hiyo. Aliwaambia wasali hivi: “Ufalme wako ukuje. Mapenzi yako yafanyike duniani kama mbinguni.” (Matayo 6:10) Mu Sura ya 8, tutajifunza namna Ufalme wa Mungu utakamata nafasi ya serikali za ulimwengu. (Soma Danieli 2:44.) Kisha, Ufalme wa Mungu utafanya dunia ikuwe paradiso yenye kupendeza.—Ona Mafasirio Ingine ya 11.
ULIMWENGU MUPYA UKO KARIBU!
15. “Dunia mupya” ni nini?
15 Biblia inatoa ahadi (malako) hii: “Tunangojea mbingu mupya na dunia mupya,” na “mule haki itakaa.” (2 Petro 3:13; Isaya 65:17) Wakati fulani, Biblia inatumia neno “dunia,” ili kuzungumuzia watu wenye kuishi mu dunia. (Mwanzo 11:1) Kwa hiyo, “dunia mupya” yenye haki ni watu wote wenye wanamutii Mungu na wenye anabariki.
16. Wale wenye wataishi mu ulimwengu mupya, Mungu atawapatia zawadi gani ya muzuri? Tunapaswa kufanya nini ili kupata zawadi hiyo?
16 Yesu aliahidi kama wale wenye wataishi mu ulimwengu mupya wa Mungu watapata “uzima wa milele.” (Marko 10:30) Tunapaswa kufanya nini ili tupate zawadi hiyo? Ili kupata jibu, unaweza kusoma Yohana 3:16 na Yohana 17:3. Tuone sasa mambo yenye Biblia inasema juu ya namna maisha yatakuwa mu dunia Paradiso.
17, 18. Ni nini inaonyesha kama kutakuwa amani na usalama mu dunia yote?
17 Hakutakuwa tena mambo ya mubaya, vita, kuvunja sheria, na kuumizana ao kuuana. Hakutakuwa tena watu wabaya mu dunia. (Zaburi 37:10, 11) Mungu ‘atamaliza vita katika dunia yote.’ (Zaburi 46:9; Isaya 2:4) Dunia itajaa watu wenye kumupenda Mungu na wenye kumutii. Kutakuwa amani milele.—Zaburi 72:7.
18 Watu wa Yehova wataishi katika usalama. Zamani, wakati Waisraeli walimutii Mungu, waliishi katika usalama kwa sababu Mungu aliwalinda. (Mambo ya Walawi 25:18, 19) Mu Paradiso, hatutaogopa kitu fulani ao mutu fulani. Tutakuwa na usalama sikuzote!—Soma Isaya 32:18; Mika 4:4.
19. Juu ya nini tunaweza kuamini kabisa kama kutakuwa chakula mingi mu dunia mupya?
19 Kutakuwa chakula mingi. “Kutakuwa nafaka nyingi juu ya dunia; itajaa sana kwenye kichwa cha milima [ao juu ya milima].” (Zaburi 72:16) Yehova, “Mungu wetu, atatubariki,” na “dunia itatoa mazao yake.”—Zaburi 67:6.
20. Ni nini inaonyesha kama dunia itakuwa paradiso?
20 Dunia yote itakuwa paradiso. Watu watakuwa na nyumba na bustani zenye kupendeza. (Soma Isaya 65:21-24; Ufunuo 11:18.) Dunia yote itakuwa yenye kupendeza kama vile bustani ya Edeni ilikuwa. Yehova atatupatia sikuzote mambo yenye tuko nayo lazima. Biblia inasema hivi juu yake: “Unafungua mukono wako na kutimiza tamaa ya kila kitu chenye uzima.”—Zaburi 145:16.
21. Ni nini inaonyesha kama kutakuwa amani kati ya watu na wanyama?
21 Kutakuwa amani kati ya watu na wanyama. Wanyama hawataumiza watu tena. Watoto watajisikia salama, hata wakati wako pamoja na wanyama wenye kuwa hatari leo.—Soma Isaya 11:6-9; 65:25.
22. Yesu atafanyia nini wale wenye kuwa wagonjwa?
22 Hakuna mutu mwenye atagonjwa. Wakati Yesu alikuwa mu dunia, aliponyesha watu wengi. (Matayo 9:35; Marko 1:40-42; Yohana 5:5-9) Lakini kwa sababu yeye ni Mufalme wa Ufalme wa Mungu, Yesu ataponyesha watu wote. Hakuna mutu mwenye atasema hivi: “Niko mugonjwa.”—Isaya 33:24; 35:5, 6.
23. Mungu atafanyia nini watu wenye wamekufa?
23 Watu wenye wamekufa wataishi tena. Mungu anaahidi kama atafufua watu wengi sana wenye wamekufa. “Kutakuwa ufufuo wa wenye haki na wenye hawako wenye haki.”—Soma Yohana 5:28, 29; Matendo 24:15.
24. Unapenda kuishi mu Paradiso? Juu ya nini?
24 Sisi wote tunapaswa kuchagua. Tunaweza kuchagua kujifunza juu ya Yehova na kumutumikia. Ao tunaweza tu kufanya mambo yenye tunapenda. Kama tunachagua kumutumikia Yehova, tutapata mambo ya muzuri wakati wenye kuja. Wakati mwanaume mumoja aliomba Yesu amukumbuke kisha kifo chake, Yesu alimuahidi hivi: “Utakuwa pamoja na mimi katika Paradiso.” (Luka 23:43) Mu sura zenye kufuata, tutajifunza mambo mengi zaidi juu ya Kristo na tutaona namna atatimiza ahadi za muzuri sana za Mungu.