Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • ypq ulizo 5 uku. 15-17
  • Nifanye Nini Kama Ninachokozwa Kwenye Masomo?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Nifanye Nini Kama Ninachokozwa Kwenye Masomo?
  • Majibu ya Maulizo 10 Yenye Vijana Wanajiulizaka
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Umutegemee Yehova Wakati Wengine Wanakuonea
    Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2023
  • Yaliyomo
    Amuka!—2013
  • Tuseme Nini Kuhusu Magazeti
    Huduma Yetu ya Ufalme—2003
Majibu ya Maulizo 10 Yenye Vijana Wanajiulizaka
ypq ulizo 5 uku. 15-17
Kijana mwanaume anachokozwa na mwengine mbele ya wanafunzi wenzake

Ulizo LA 5

Nifanye Nini Kama Ninachokozwa Kwenye Masomo?

SABABU GANI ULIZO HILO NI LA MAANA?

Namna utajiendesha wakati unachokozwa inaweza kufanya mambo yakuwe muzuri zaidi ao mubaya zaidi.

UNGEFANYA NINI?

Wazia jambo hili: Thomas hapendi kuenda kwenye masomo leo, wala kesho, wala siku ingine. Mambo yote yalianzia kwenye masomo kumepita miezi tatu. Wakati huo wanafunzi wenzake walieneza habari za mubaya juu yake. Kisha walianza kumupatia majina mengi ya kumukasirisha. Wakati fulani mwanafunzi mwenzake anaweza kuangusha mabuku (cahiers) zenye kuwa katika mikono ya Thomas na kufanya kama vile ilikuwa aksida, ao mumoja kati ya wanafunzi wenye kuwa katika kikundi anaweza kumusukuma, na wakati Thomas anageuka ili kuangalia mutu mwenye alimusukuma, hatambue kama ni nani. Na jambo la mubaya zaidi ni kwamba, jana Thomas alipata barua kupitia Internete yenye kumuambia afanye angalisho . . .

Kama ungekuwa Thomas, ungefanya nini?

WAZA KIDOGO!

Haiko kusema kwamba hauna nguvu kabisa! Kwa kweli, unaweza kumushinda mutu mwenye anakuchokoza bila kumupiga. Namna gani?

  • UKUWE MWENYE KUTULIA. Biblia inasema hivi: ‘Mutu mujinga anaiachilia roho yake yote, lakini mwenye hekima anaituliza mupaka mwisho. (Methali 29:11) Kama unajikaza kuonyesha kwamba unatulia kabisa, inawezekana wale wenye kukuchokoza hawatafurahia tena kuendelea kukuchokoza.

  • USIRUDISHE UBAYA KWA UBAYA. Biblia inasema hivi: ‘Musimulipe yeyote uovu kwa uovu.’ (Waroma 12:17) Kama unatafuta kurudisha ubaya kwa ubaya, mambo yatakuwa mubaya zaidi.

  • USIJIINGIZE KATIKA MAGUMU. Biblia inasema hivi: ‘Mutu mwerevu ni yule ambaye ameona musiba [ao, hatari] na kujificha.’ (Methali 22:3) Ujikaze kabisa kuepuka watu wenye wanaweza kukuchokoza ao hali zenye zinaweza kufanya watu wakuchokoze.

  • UWAJIBIE KWA NJIA YENYE HAWAWAZIE. Biblia inasema hivi: ‘Jibu, linapokuwa la upole, linageuza gazabu [ao, hasira].’ (Methali 15:1) Unaweza hata kuchekesha kidogo. Kwa mufano, kama mutu mwenye anakuchokoza anasema kwamba unanenepa sana, unaweza kumujibia, “Ninaona kuwa ni muzuri kupunguza kilo fulani!”

  • UNYAMAZE. Nora mwenye kuwa na miaka 19 anasema hivi: “Kunyamaza kunaonyesha kwamba uko mutu mwenye kukomaa na kwamba uko na nguvu kuliko mutu mwenye anakuchokoza. Kufanya hivyo, kunaonyesha kwamba unajua kujizuia. Lakini, mutu mwenye anakuchokoza hajue kufanya jambo hilo.”—2 Timotheo 2:24.

  • UFANYE NGUVU ILI KUONYESHA KWAMBA UNAJITUMAINIA. Mara nyingi, watu wenye kuchokoza wengine wanaweza kutambua watu wenye hawajitumainie na wenye hawana nguvu ya kupigana kama wanachokozwa. Lakini, watu wengi wenye wanachokoza wengine hawatakuchokoza kama wanaona kwamba hauwapatie nafasi ya kufanya hivyo.

  • UMUAMBIE MUTU MWENGINE. Mutu mumoja mwenye alikuwa mwalimu wa masomo anasema hivi: “Ningeshauri mutu mwenye anachokozwa amuambie mutu mwengine jambo hilo. Hilo ni jambo la muzuri la kufanya ili kuzuia mutu mwengine asichokozwe.”

    Kujitumania kutakupatia nguvu yenye mutu mwenye anakuchokoza hana

Kijana mwanaume anapambana na mutu mwenye anamuchokoza kwa kujitumainia

Kujitumania kutakupatia nguvu yenye mutu mwenye anakuchokoza hana

ULIJUA?

Kuchokozwa haiko tu kutendewa mubaya kimwili, lakini inaweza kuwa pia:

  • Maneno yenye kuwa kama moto yanatoka katika kinywa cha mutu mwenye kuchokoza mwengine

    Kuchokozwa kupitia maneno. “Siwezi kusahau majina yenye walinipatia ao mambo yenye walisema. Walifanya nijisikie kuwa mutu mwenye hana maana, mwenye hapendwi, na wa bure kabisa. Ningependa hata wanipige kuliko kuniambia maneno hayo.”—Celine, mwenye kuwa na miaka 20.

  • Kijana mwanaume anakaa peke yake kisha kutengwa na wenzake

    Wengine kukuepuka. “Wanafunzi wenzangu walianza kuniepuka. Walifanya kama vile hakuna nafasi kwenye meza ili nisikae nao. Kwa muda wa mwaka muzima, nililia na kula peke yangu.”​—⁠Haley, mwenye kuwa na miaka 18.

  • Kijana mwanamuke anarudia nyuma kisha kuchokozwa kwenye Internete

    Kuchokozwa kupitia Internete. “Kwa kuandika maneno kidogo tu kwenye Internete, unaweza kuharibisha sifa ya mutu na hata maisha yake. Inaonekana kama vile ni kutia chumvi, lakini jambo hilo linaweza kutokea!”—Daniel, mwenye kuwa na miaka 14.

MAULIZO KUHUSU TABIA YA KUWACHOKOZA WENGINE

KWELI AO UONGO

MAJIBU

1 Tabia ya kuchokoza wengine ilianza tangu zamani sana.

1 Kweli. Kwa mufano, Biblia inazungumuzia Wanefili wenye jina lao linamaanisha “Wale Wenye Kuangusha Wengine.”—Mwanzo 6:4.

2 Kuwachokoza wengine haiko mubaya sana. Ni muzaha tu.

2 Uongo. Tabia ya kuchokoza wengine ni kati ya mambo yenye kusukuma vijana wengi wajiue.

3 Njia ya muzuri ya kufanya mutu mwenye anakuchokoza akuache ni kumurudishia tu.

3 Uongo. Mara nyingi, watu wenye wanazoea kuchokoza wengine wako na nguvu zaidi kuliko wale wenye wanachokozwa. Kwa hiyo, ni bure kujaribu kuwarudishia.

4 Kama unaona mutu mwenye anachokozwa, ni muzuri sana kufanya kama vile hauone.

4 Uongo. Wakati unaangalia tu mutu fulani anachokozwa na haufanye kitu, unaweza kuwa kati ya watu wenye kuleta magumu kuliko kuwa kati ya wale wenye kusaidia kuyamaliza.

5 Hata kama watu wenye kuchokoza wengine wanasema kwa kujivuna, mara nyingi wanaogopa.

5 Kweli. Hata kama watu wenye wanazoea kuchokoza wengine wanajivuna sana, wengi kati yao wanaogopa. Kwa hiyo, wanachokoza wengine ili wajisikie muzuri zaidi.

6 Kama wanapata musaada, Watu wenye wanachokoza wengine wanaweza kubadilisha mawazo na matendo yao.

MAMBO NINAPANGA KUFANYA

  • Kama mutu fulani ananichokoza, nitasema ao nitafanya nini?

ILI KUPATA HABARI ZAIDI!

Umushinde Mwenye Kukuchokoza Bila Kumupiga

Angalia picha kwenye ubao Umushinde Mwenye Kukuchokoza Bila Kumupiga kwenye www.pr2711.com/swc ((Fungua kichwa MAFUNDISHO YA BIBLIA > VIJANA)

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine