Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • lfb somo 6 uku. 20-uku. 21 fu. 5
  • Watu Munane Waliokoka Garika

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Watu Munane Waliokoka Garika
  • Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Safina ya Noa
    Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
  • Alilindwa “Akiwa Salama Pamoja na Wengine Saba”
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Noa “Alitembea Pamoja na Mungu wa Kweli”
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Kila Mmoja Anaweza Kujifunza Kutokana na Vidio Noé : il marchait avec Dieu
    Huduma Yetu ya Ufalme—2002
Ona Habari Zaidi
Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
lfb somo 6 uku. 20-uku. 21 fu. 5
Safina inaenda juu ya maji wakati mvua inanyesha

6

Watu Munane Waliokoka Garika

Noa, familia yake, na wanyama wanatoka mu safina

Noa, familia yake, na wanyama waliingia mu safina. Kisha, Yehova alifunga mulango na mvua ikaanza kunyesha. Ile mvua ilikuwa ya mingi sana na safina ilianza kuenda juu ya maji. Kisha, dunia yote ikajaa maji. Watu wote wabaya wenye walikuwa inje ya safina walikufa. Lakini Noa na familia yake walikuwa salama mu safina. Hauone kama walifurahi kwa sababu walimutii Yehova?

Mvua ilinyesha kwa siku 40 muchana na usiku, kisha ikaisha. Maji ikaanza kupunguka polepole. Ku mwisho, safina ikasimama ku mulima. Lakini, kulikuwa kungali maji ya mingi fasi yote, kwa hiyo Noa na familia yake hawakuweza kutoka mu safina palepale.

Maji iliendelea kukauka polepole. Noa na familia yake walibakia ndani ya safina zaidi ya mwaka moja. Kisha, Yehova aliwaambia watoke mu safina. Walifurahi sana kwa sababu Yehova aliwaokoa. Na ili kumushukuru, walimutolea zabihu.

Upinde wa mvua

Yehova alifurahia ile zabihu. Na alisema kama hataharibishaka tena vitu vyote mu dunia kupitia garika ao mvua kubwa. Ili kuonyesha kama hataharibishaka tena dunia kupitia garika, alifanya upinde wa mvua (arc-en-ciel) uonekane mu mawingu kwa mara ya kwanza. Ulishakaona upinde wa mvua?

Kisha pale, Yehova aliambia Noa na familia yake wazae watoto na kujaza dunia.

“Noa aliingia ndani ya safina; na [watu] hawakuhangaika mupaka Garika ikakuja na kuwaharibu wote.”​—Matayo 24:38, 39

Maulizo: Kisha Yehova kufunga mulango wa safina, kulitokea nini? Upinde wa mvua unatukumbusha nini?

Mwanzo 7:1–9:17

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine