Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • lfb somo 35 uku. 86-uku. 87 fu. 1
  • Hana Anasali Apate Mutoto Mwanaume

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Hana Anasali Apate Mutoto Mwanaume
  • Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Alimufungulia Mungu Moyo Katika Sala
    Tuige Imani Yao
  • Acha Yehova Akutulize
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2020
  • Fungulia Yehova Moyo Wako Katika Sala
    Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2022
  • Yehova Anaona Machozi Yako
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2024
Ona Habari Zaidi
Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
lfb somo 35 uku. 86-uku. 87 fu. 1
Hana anapatia Eli Samweli ku tabenakulo

35

Hana Anasali Apate Mutoto Mwanaume

Mwanaume Mwisraeli mwenye aliitwa Elkana alikuwa na bibi wawili: Hana na Penina. Lakini Elkana alipenda sana Hana. Kila wakati, Penina alimucheka Hana juu yeye alikuwa na watoto wengi, lakini Hana hakukuwa na mutoto. Kila mwaka, Elkana na familia yake walienda kuabudu ku tabenakulo kule Shilo. Siku moja, wakati walikuwa kule, alitambua kama bibi yake mupendwa Hana alikuwa na huzuni sana. Akamuambia: ‘Hana, tafazali usilie. Niko pale juu yako. Ninakupenda.’

Kisha, Hana alienda kusali. Aliendelea kumulilia Yehova amusaidie. Akamutolea hii ahadi: ‘Yehova, ukinipatia mutoto mwanaume, nitakupatia ule mutoto ili akutumikie maisha yake yote.’

Kuhani Mukubwa Eli anaona Hana iko analia wakati iko anasali

Wakati kuhani Mukubwa Eli aliona Hana iko analia, aliwaza kama Hana analewa. Hana akamujibu: ‘Hapana, Bwana wangu, siko mulevi. Niko na shida kubwa yenye iko inanisumbua sana na njo yenye niko ninaelezea Yehova.’ Eli alitambua kama alikuwa amewazia Hana mubaya, kwa hiyo akamuambia: ‘Mungu akupatie jambo lenye unamuomba.’ Hana akajisikia muzuri zaidi, kisha akaenda. Mbele mwaka moja ienee, akazaa mutoto mwanaume na akamupatia jina Samweli. Wazia namna Hana alifurahi sana kupata mutoto!

Hana hakusahau ahadi yenye alimutolea Yehova. Kisha Samweli kuacha kunyonya, alimupeleka ku tabenakulo juu atumikie kule. Hana aliambia Eli: ‘Huyu njo mutoto mwenye niliombaka Yehova anipatie. Ninamutoa kwa Yehova juu amutumikie maisha yake yote.’ Kila mwaka, Elkana na Hana walikuwa wanaenda kuona Samweli na walikuwa wanamupelekea koti yenye haina mikono. Yehova alibariki Hana na akazaa watoto wengine, wanaume tatu na wanamuke wawili.

“Muendelee kuomba, na mutapewa; muendelee kutafuta, na mutapata.”​—Matayo 7:7

Maulizo: Juu ya nini Hana alikuwa na huzuni? Namna gani Yehova alibariki Hana?

1 Samweli 1:1–2:11, 18-21

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine