Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • lfb somo 48 uku. 116-uku. 117 fu. 1
  • Mutoto wa Mujane Anafufuliwa

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Mutoto wa Mujane Anafufuliwa
  • Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Mujane wa Sarefathi Alibarikiwa kwa Sababu ya Imani Yake
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Mungu Wake Alimufariji
    Tuige Imani Yao
  • Alifarijiwa na Mungu Wake
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Unajisikia Kuwa Peke Yako na Mwenye Kuogopa?
    Uwafundishe Watoto Wako
Ona Habari Zaidi
Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
lfb somo 48 uku. 116-uku. 117 fu. 1
Eliya anaita mujane mwenye kukusanya kuni

48

Mutoto wa Mujane Anafufuka

Mutungi wa unga na wa mafuta

Wakati mvua haikukuwa inanyesha, Yehova aliambia Eliya: ‘Uende Sarefati. Kule, mujane fulani atakupatia chakula.’ Wakati alifika kwenye milango mikubwa ya muji, Eliya alikutana na mujane maskini mwenye alikuwa anakusanya kuni. Akamuomba maji ya kunywa. Wakati alienda kuleta maji, Eliya akamuita na kumuambia: ‘Tafazali, uniletee kipande cha mukate.’ Lakini ule mujane akamuambia: ‘Sina mukate wa kukupatia. Niko tu na unga na mafuta kidogo ya kupika nayo chakula yangu na ya mutoto wangu.’ Eliya akamuambia: ‘Yehova amesema kama ukinitayarishia mukate, unga wako na mafuta yako havitaisha mupaka wakati mvua itaanza tena kunyesha.’

Basi, ule mujane akaenda kwake na kupikia nabii wa Yehova mukate. Sawa vile tu Yehova alisema, ule mujane na mutoto wake walikuwa na chakula wakati wote wenye mvua haikunyesha. Mitungi yake ya unga na mafuta haikupunguka.

Kisha jambo fulani la mubaya likatokea. Mutoto wa ule mujane akagonjwa sana na akakufa. Ule mujane akamulilia Eliya amusaidie. Eliya akakamata ule mutoto mwanaume na kumupeleka mu chumba cha juu cha ile nyumba ya ule mujane. Akamulalisha ku kitanda na kusali hivi: ‘Yehova, tafazali fufua huyu mutoto.’ Aliomba Yehova afanye jambo la kushangaza sana. Unajua juu ya nini? Ni juu, kama vile tunajua, mbele ya pale hakuna mutu mwenye alikufaka kisha akafufuka. Na ule mujane na mutoto wake hawakukuwa hata Waisraeli.

Lakini ule mutoto akaanza kupumua, na akakuwa tena muzima! Eliya akaambia ule mujane: ‘Ona! Mutoto wako iko muzima.’ Ule mujane akafurahi sana na kuambia Eliya: ‘Uko mutu wa Mungu kabisa. Ninajua vile juu unasemaka tu mambo yenye Yehova anakuambia useme.’

Eliya anapatia mujane mutoto wake mwenye amefufuliwa

“Muangalie kunguru: Hawapande mbegu wala hawavune; hawana chumba cha kuwekea chakula wala depo; lakini Mungu anawalisha. Je, ninyi hamuko wa maana kuliko ndege?”—Luka 12:24

Maulizo: Mujane wa Sarefati alifanya nini ili kuonyesha kama anamutumainia Yehova? Nini njo inaonyesha kama Eliya alikuwa nabii wa kweli wa Mungu?

1 Wafalme 17:8-24; Luka 4:25, 26

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine