Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • lfb somo 70 uku. 166-uku. 167 fu. 2
  • Malaika Wanatangaza Kama Yesu Amezaliwa

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Malaika Wanatangaza Kama Yesu Amezaliwa
  • Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Yesu Alizaliwa Wapi na Wakati Gani?
    Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
  • Yesu Kristo—Tumukumbuke Kama Mutoto Muchanga ao Kama Mufalme?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Alifikiri na Kuamua Katika Moyo Wake
    Tuige Imani Yao
  • Maulizo ya Wasomaji Wetu
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2023
Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
lfb somo 70 uku. 166-uku. 167 fu. 2
Malaika wanatangazia wachungaji kama Yesu amezaliwa

70

Malaika Wanatangaza Kama Yesu Amezaliwa

Mutawala wa Roma, Kaisari Augusto, alitoa amri kama Wayahudi wote waende kujiandikisha mu miji yao. Kwa hiyo, Yosefu na Maria walirudia Betlehemu, kwenye familia ya Yosefu ilitokaka. Wakati huo, Maria alikuwa karibu kuzaa.

Wakati walifika Betlehemu, walikosa fasi ya muzuri ya kubakia. Kwa hiyo, walienda kukaa fasi ya kulalishia wanyama. Mule njo Maria alizalia mutoto wake, Yesu. Alimufunga na vitambaa laini na kumulalisha mu chombo cha kukulishia wanyama.

Karibu na Betlehemu, kulikuwa wachungaji fulani wenye walikuwa inje usiku. Walikuwa wanachunga makundi yao ya wanyama. Palepale, malaika akasimama pembeni yao na mwangaza wa utukufu wa Yehova ukaangaza pande zote. Wachungaji wakaogopa, lakini malaika akawaambia: ‘Musiogope, niko na habari ya muzuri sana ya kuwaambia. Leo, Masiya amezaliwa Betlehemu.’ Mara moja, malaika wengi wakajiunga na ule malaika, na kusema: ‘Utukufu kwa Mungu kule juu, na amani ku dunia.’ Kisha wale malaika hawakuonekana tena. Sasa, wachungaji walifanya nini?

Wachungaji wakaambiana hivi: ‘Tuende mara moja Betlehemu.’ Wakaenda haraka na wakakuta Yosefu na Maria na mutoto wao mudogo fasi ya kulalishia wanyama.

Wote wenye walisikia mambo yenye malaika aliambia wachungaji walishangaa sana. Maria alifikiri sana kuhusu maneno ya ule malaika na hakuisahau hata kidogo. Basi wachungaji wakarudia kuchunga makundi yao ya wanyama na wakamushukuru Yehova juu ya mambo yote yenye waliona na kusikia.

“Nilitoka kwa Mungu na niko hapa. Sikukuja kwa uamuzi wangu mwenyewe, lakini Yeye ndiye alinituma.”​—Yohana 8:42

Maulizo: Namna gani malaika walitangaza kama Yesu amezaliwa? Wachungaji walikuta nani kule Betlehemu?

Luka 2:1-20; Isaya 9:6

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine