Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • lfb somo 74 uku. 176-uku. 177 fu. 4
  • Yesu Anakuwa Masiya

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Yesu Anakuwa Masiya
  • Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Yesu Anabatizwa
    Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
  • Yohana Anatayarisha Kuja kwa Masiya
    Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
  • Yesu Kristo Ni Nani?
    Biblia Inatufundisha Nini?
  • Yesu Anaongezeka na Yohana Anapunguka
    Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
Ona Habari Zaidi
Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
lfb somo 74 uku. 176-uku. 177 fu. 4
Kisha Yohana kubatiza Yesu, roho ya Mungu inashuka juu ya Yesu kama njiwa

74

Yesu Anakuwa Masiya

Yohana alikuwa anahubiri hivi: ‘Mutu fulani mukubwa kuliko mimi anakuja.’ Wakati Yesu alikuwa na miaka 30 hivi, alitoka Galilaya na kuenda ku Muto Yordani, kwenye Yohana alikuwa anabatiza watu. Alipenda Yohana amubatize. Lakini Yohana alimuambia: ‘Haiko mimi njo ninapaswa kukubatiza. Wewe njo unapaswa kunibatiza.’ Yesu akamuambia: ‘Yehova anapenda wewe unibatize.’ Kwa hiyo, wakaingia katika Muto Yordani, na Yohana akazamisha Yesu ndani ya maji.

Kisha Yesu kutoka ndani ya maji, alisali. Palepale, mbingu zikafunguliwa, na roho ya Mungu ikashuka juu yake kama njiwa. Kisha sauti ya Yehova ikatoka mbinguni na kusema: “Wewe ni Mwana wangu, mupendwa; nimekukubali.”

Wakati roho ya Yehova ilishuka juu ya Yesu njo sasa akakuwa Kristo, ao Masiya. Sasa angeweza kuanza kazi yenye Yehova alimutuma afanye ku dunia.

Kisha tu kubatizwa, Yesu alienda mu jangwa. Alifanya kule siku 40. Wakati alitoka mu jangwa, akaenda kuona Yohana. Wakati Yesu alifika karibu na Yohana, Yohana akasema: ‘Huyu njo Mwana-Kondoo wa Mungu mwenye ataondoa zambi ya ulimwengu.’ Wakati Yohana alisema vile, alisaidia watu wajue kama Yesu njo Masiya. Je, unajua mambo yenye ilimufikiaka Yesu wakati alikuwa mu jangwa? Ile njo tutaona mu sura yenye kufuata.

“Sauti ikatokea mbinguni: ‘Wewe ni Mwana wangu, mupendwa; nimekukubali.’”​—Marko 1:11

Maulizo: Juu ya nini Yesu alibatizwa? Juu ya nini Yohana alisema kama Yesu alikuwa Mwana-Kondoo wa Mungu?

Matayo 3:13-17; Marko 1:9-11; Luka 3:21-23; Yohana 1:29-34; Isaya 42:1; Waebrania 10:7-9

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine