Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • lfb somo 83 uku. 194-uku. 195 fu. 1
  • Yesu Anakulisha Maelfu ya Watu

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Yesu Anakulisha Maelfu ya Watu
  • Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Anatumia Mikate Tano na Samaki Wawili ili Kukulisha Maelfu ya Watu
    Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
  • Muujiza wa Mikate Wenye Yesu Alifanya
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2024
  • Chakula cha Mangaribi cha Mwisho cha Yesu
    Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
  • Yesu Anatembea Juu ya Maji
    Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
Ona Habari Zaidi
Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
lfb somo 83 uku. 194-uku. 195 fu. 1
Mitume wanapatia watu mingi chakula

83

Yesu Anakulisha Maelfu ya Watu

Mbele tu ya Pasaka ya mwaka wa 32, mitume walirudia kutoka mu kazi ya kuhubiri. Kwa sababu walikuwa wamechoka, Yesu na mitume wake walipanda mu mashua (bateau) ya kuenda Betsaida ili wapumuzike. Lakini wakati mashua ilikaribia kufika pembeni ya bahari, Yesu aliona kama watu mingi walikuwa wamewafuata. Hata kama alipenda yeye na mitume wake wakuwe peke yao, alitendea muzuri wale watu. Aliponyesha wagonjwa wao, na alianza kuwafundisha. Ile siku yote, aliwafundisha juu ya Ufalme wa Mungu. Wakati ilikuwa mangaribi, mitume walimuambia: ‘Watu wanasikia njaa. Uwaambie waende kujitafutia chakula.’

Kijana anapatia Yesu kitunga cha mikate na samaki

Yesu akawajibu: ‘Haiko lazima waende. Munaweza kuwapatia chakula hapa.’ Kisha, Mitume wakamuuliza: ‘Unataka tuende kuwauzia mikate?’ Filipo, mumoja wa mitume, akasema: ‘Hata tukuwe na feza mingi hatutaweza kuuza mikate yenye itawashibisha.’

Yesu akauliza: ‘Tuko na chakula gani?’ Andrea akamujibu: ‘Tuko tu na mikate tano na samaki mbili za kidogo-kidogo. Ile chakula haitaenea watu wote wenye kuwa hapa. Yesu akasema: ‘Muniletee ile mikate na samaki.’ Kisha, akaambia watu wakae juu ya majani, wajipange mu vikundi-vikundi vya watu 50 na 100. Yesu akakamata mikate na samaki, akaangalia juu mbinguni, na kusali. Kisha akapatia mitume, mitume nao wakapatia watu. Wanaume 5000, wanamuke, na watoto wakakula na kushiba. Kisha, mitume wakakusanya chakula chenye kilibakia, ili kusikuwe chakula chenye kingetupwa. Chakula chenye kilibakia kilijaa vitunga 12. Ule ni muujiza wenye kushangaza sana, hauone vile?

Watu walifurahi sana na walitaka kumufanya Yesu akuwe mufalme wao. Lakini Yesu alijua kama wakati wenye Yehova alimuwekea ili akuwe mufalme ulikuwa haujafika. Kwa hiyo, aliambia watu warudie na akaambia mitume waende ngambo ingine ya Bahari ya Galilaya. Mitume walipanda mu mashua, lakini Yesu alienda ku mulima peke yake. Juu ya nini? Kwa sababu alipenda asali kwa Baba yake. Hata wakati alikuwa na mambo mingi ya kufanya, Yesu alitafuta wakati wa kusali.

“Musifanye kazi kwa ajili ya chakula chenye kinaharibikaka, lakini mufanye kazi kwa ajili ya chakula chenye kinadumu kwa ajili ya uzima wa milele, chenye Mwana wa binadamu atawapatia.”​—Yohana 6:27

Maulizo: Yesu alifanya nini ili kuonyesha kama alihangaikia watu? Ile inatufundisha nini juu ya Yehova?

Matayo 14:14-22; Luka 9:10-17; Yohana 6:1-15

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine