Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • lfb somo 94 uku. 220-uku. 221 fu. 1
  • Wanafunzi Wanapokea Roho Takatifu

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Wanafunzi Wanapokea Roho Takatifu
  • Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Mamia Wanamuona Mbele ya Pentekoste
    Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
  • Walijiacha Waongozwe na Roho ya Mungu: Wakati wa Mitume na Katika Siku Zetu
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • “Wakajazwa Roho Takatifu”
    “Kutoa Ushahidi Kamili” juu ya Ufalme wa Mungu
Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
lfb somo 94 uku. 220-uku. 221 fu. 1
Watu mu Yerusalemu wanashangaa kusikia wanafunzi wa Yesu wanazungumuza nao mu luga zao

94

Wanafunzi Wanapokea Roho Takatifu

Siku kumi kisha Yesu kurudia mbinguni, wanafunzi wake walipokea roho takatifu. Ilikuwa Sikukuu ya Pentekoste ya mwaka wa 33. Watu wa sehemu mbalimbali walikuwa wamekuja Yerusalemu kwa ajili ya ile Sikukuu. Wanafunzi wa Yesu 120 hivi walikuwa wamekusanyika mu chumba cha juu cha nyumba fulani. Mara moja, jambo la kushangaza likatokea. Kitu fulani kama moto kikaonekana juu ya kichwa cha kila mwanafunzi, na wakaanza kusema luga mbalimbali. Makelele sawa vile makelele ya upepo wenye nguvu ikajaa mu ile nyumba.

Wageni wenye walitoka sehemu mbalimbali na kuja Yerusalemu walisikia ile makelele na kuenda mbio ku ile nyumba ili waone kama kulitokea nini. Walishangaa wakati walisikia wanafunzi wanazungumuza zile luga mbalimbali. Wakasema: ‘Hawa watu ni Wagalilaya, mbona wako wanasema luga zetu?’

Kisha Petro na mitume wengine wakasimama mbele ya watu mingi. Petro akawaelezea namna Yesu aliuawa na kama Yehova alimufufua. Petro akasema: ‘Sasa Yesu iko mbinguni ku mukono wa kuume wa Mungu, naye ametupatia roho takatifu kama vile alituambiaka. Njo maana mumeona na kusikia hii miujiza.’

Maneno yenye Petro alisema iligusa watu moyo. Kwa hiyo, wakauliza: “Inaomba tufanye nini?” Petro akawaambia: ‘Mutubu zambi zenu na mubatizwe katika jina la Yesu. Na ninyi pia, mutapokea zawadi ya roho takatifu.’ Ile siku, watu karibu 3000 wakabatizwa. Kuanzia ile wakati, hesabu ya wanafunzi ikaongezeka haraka katika Yerusalemu. Kwa musaada wa roho takatifu, mitume wakaanzisha makutaniko mingi ili waweze kufundisha wanafunzi mambo yote yenye Yesu alikuwa amewaagiza.

“Kama unatangaza mbele ya watu wote kwa kinywa chako kwamba Yesu ni Bwana, na unaonyesha imani katika moyo wako kwamba Mungu alimufufua kutoka kwa wafu, utaokolewa.”​—Waroma 10:9

Maulizo: Ni nini ilitokea siku ya Pentekoste ya mwaka 33? Juu ya nini watu mingi sana walibatizwa?

Matendo 1:15; 2:1-42; 4:4; Yohana 15:26

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine