WIMBO 51
Ninajitoa kwa Mungu!
Maandishi
1. Mungu njo aliniongoza kwa Yesu,
Ili nijifunze Biblia.
Niliamini mambo
Yenye nilijifunza.
Sasa ninaamua
Kutumikia Mungu.
(REFREE)
Miye peke najitoa kwa Yehova.
Kweli niko na furaha sana.
2. Mu sala nilimuambia Yehova
Kama nitamutumikia.
Ninafurahi sana
Kubeba jina yake,
Na kuhubiri sana
Habari ya Ufalme.
(REFREE)
Miye peke najitoa kwa Yehova.
Kweli niko na furaha sana.