WIMBO 78
‘Kufundisha Neno ya Mungu’
Maandishi
1. Wakati tunafundisha
Neno ya Yehova,
Anatubariki sana.
Tuko na furaha.
Tunajikaza kuiga
Upendo wa Kristo,
Wakati tunafundisha
Watu kuhusu Mungu.
2. Siye wenye kufundisha
Tunatii Mungu,
Ili kwa matendo yetu
Watu wamusifu.
Tunaipenda Biblia
na tunaisoma,
Ili tuielewe
Na kufundisha wengine.
3. Wakati tunafundisha,
Tumuombe Mungu
Atupatie hekima
Na atuongoze.
Tunapenda watu wote
Na kuwafundisha,
Ili nao pia
Wafundishe watu wengine.
(Ona pia Zb. 119:97; 2 Ti. 4:2; Tit. 2:7; 1 Yo. 5:14.)