WIMBO 83
“Nyumba kwa Nyumba”
Maandishi
1. Tunahubiria wote
Neno ya Yehova,
Kila nyumba na mulango,
Mu dunia yote.
Ufalme unatawala,
Ni habari njema.
Wazee pia vijana
Wanaihubiri.
2. Tunaenda fasi yote,
Hata mu mashamba,
Ili kufundisha watu
Kumuhusu Mungu.
Na wakimuheshimia
Wataokolewa.
Basi tuwahubirie
Ku kila mulango.
3. Tuende nyumba kwa nyumba
Ili kuhubiri;
Watu wajichagulie
Kuipenda kweli.
Na hata wakikatala,
Tutaendelea
Kuwatafuta kondoo
wa Yehova Mungu.
(Ona pia Mdo. 2:21; Ro. 10:14.)