Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • rr uku. 10
  • 1A Ibada Ni Nini?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • 1A Ibada Ni Nini?
  • Ibada Safi ya Yehova Inarudishwa Tena!
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Ibada ya Kweli Itaongeza Furaha Yako
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2022
  • “Yehova Mungu Wako Ndiye Unapaswa Kuabudu”
    Ibada Safi ya Yehova Inarudishwa Tena!
  • Njia ya Muzuri ya Kumuabudu Mungu
    Biblia Inatufundisha Nini?
  • “Abudu Mungu”
    Ibada Safi ya Yehova Inarudishwa Tena!
Ona Habari Zaidi
Ibada Safi ya Yehova Inarudishwa Tena!
rr uku. 10
Wanajifunza pamoja kitabu Ibada Safi

KISANDUKU CHA KUFUNDISHIA 1A

Ibada Ni Nini?

Ibada inaweza kufasiriwa kuwa “tendo la kuonyesha heshima na upendo kwa mungu fulani.” Mu Biblia, maneno ya luga ya kwanza yenye kutafsiriwa “ibada” inatoa wazo la kuonyesha heshima kubwa, ao kujitiisha, kwa viumbe. (Mt. 28:9) Ile maneno inaweza pia kumaanisha tendo la kidini lenye mutu anafanyia Mungu wa kweli ao mungu fulani wa uongo. (Yoh. 4:23, 24) Habari yenye kuzungumuziwa inasaidia kuelewa ni mu maana gani ile maneno inatumiwa.

Yehova peke yake, Muumbaji na Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi wa Ulimwengu Wote, njo tunapaswa kuabudu. (Ufu. 4:10, 11) Tunamuabudu Yehova kwa kuheshimia mamlaka yake makubwa zaidi na kwa kuheshimia jina lake. (Zb. 86:9; Mt. 6:9, 10) Ile mambo mbili​—mamlaka makubwa zaidi ya Yehova na jina lake—​inazungumuziwa sana mu kitabu cha Ezekieli. Maneno “Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova” inatumiwa mara 217 mu kitabu cha Ezekieli peke yake, na maneno “kujua kwamba mimi ni Yehova,” na maneno mengine yenye kufanana nayo inapatikana mara 55.​—Eze. 2:4; 6:7.

Ibada yetu haiko hisia tu; lakini ibada ya kweli inaonyeshwa kwa matendo. (Yak. 2:26) Wakati tunatoa maisha yetu kwa Yehova, tunaahidi kama mu kila sehemu ya maisha yetu, tutamutii yeye akiwa Mutawala wetu Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi na pia tutaheshimia sana jina lake. Kumbuka kwamba mu jibu lenye alitoa wakati alijaribiwa mara ya tatu, Yesu alionyesha kama kuko uhusiano kati ya ibada na “utumishi mutakatifu.” (Mt. 4:10) Sisi waabudu wa Yehova, tuko na tamaa kubwa ya kumutumikia.a (Kum. 10:12) Tunamutolea Mungu wetu utumishi mutakatifu wakati tunafanya mambo mbalimbali yenye kuhusiana moja kwa moja na ibada yetu na yenye inaomba kuonyesha roho ya kujitoa. Mambo gani?

Anatoa jibu mu mukutano; kusafisha fasi ya mukusanyiko

Utumishi mutakatifu unaweza kufanywa mu njia mingi, na zote ni za maana sana mu macho ya Yehova. Tunafanya utumishi mutakatifu wakati tunahubiria wengine, wakati tunatoa majibu mu mikutano ku Jumba letu la Ufalme, na wakati tunatunza na kujenga fasi yetu ya kufanyia mikutano. Zaidi ya ile, tunatoa utumishi mutakatifu wakati tunashiriki mu ibada ya familia, wakati tunatoa michango juu ya kusaidia waamini wenzetu wenye kuwa na lazima ya musaada, wakati tunajitolea kufanya kazi ku mikusanyiko, ao wakati tunatumika ku Beteli. (Ebr. 13:16; Yak. 1:27) Kama ibada safi inakamata nafasi ya kwanza mu akili na moyo wetu, tutatoa “utumishi mutakatifu muchana na usiku.” Tunafurahia sana kuabudu Mungu wetu, Yehova!​—Ufu. 7:15.

Rudia ku sura ya 1, fungu la 9

a Moja kati ya maneno ya Kiebrania yenye inatoa wazo la ibada inaweza pia kumaanisha ‘kutumikia.’ Kwa hiyo, kutolea mutu ibada kunaweza pia kumaanisha kumutumikia.​—Kut. 3:12, maelezo ya chini.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine