SOMO YA 14
Tufanye Nini Juu Mungu Afurahie Ibada Yetu?
Sawa vile tuliona mu somo ya 13, haiko dini zote njo Mungu anakubali. Hata vile, tunaweza kumuabudu Mungu mu namna yenye anafurahia. Ni “ibada [ao, dini]” ya namna gani njo Mungu anafurahia? (Yakobo 1:27, maelezo ya chini) Ona mambo yenye Biblia inafundisha.
1. Nini njo itatusaidia kujua namna ya muzuri ya kumuabudu Mungu?
Biblia njo itatusaidia. Yesu aliambia hivi Mungu: “Neno lako ni kweli.” (Yohana 17:17) Dini za mingi hazifundishake kweli yenye iko mu Neno ya Mungu, Biblia. Zinafundishaka njo mafundisho na desturi za wanadamu. Lakini, Yehova hafurahiake wale wenye ‘wanazarau amri’ yake. (Soma Marko 7:9.) Yehova anafurahi wakati tunamuabudu mu namna yenye Biblia inaonyesha na wakati tunafuata mashauri ya Biblia.
2. Tunapaswa kumuabudu Yehova namna gani?
Tunapaswa kumuabudu Yehova tu juu yeye njo alituumbaka. (Ufunuo 4:11) Ni kusema, yeye tu njo tunapaswa kupenda na kuabudu. Hatupaswe kutumia sanamu wakati tuko namuabudu.—Soma Isaya 42:8.
Ibada yetu inapaswa kuwa “takatifu, na yenye kukubalika” kwa Yehova. (Waroma 12:1) Ni kusema, tunapaswa kutii sheria zake. Kwa mufano, wale wenye kumupenda Yehova wanapenda sheria zake juu ya ndoa na wanazitii. Wanaepuka tabia za mubaya, sawa vile kuvuta tumbako ao kutumia mubaya dawa za kulewesha ao pombe.a
3. Juu ya nini tunapaswa kumuabudu Yehova pamoja na Wakristo wengine?
Mikutano yetu ya kila juma inatupatiaka nafasi ya ‘kumusifu Yehova . . . katika kutaniko.’ (Zaburi 111:1, 2) Kwa mufano, tunafanyaka vile wakati tunamuimbia Mungu sifa. (Soma Zaburi 104:33.) Yehova anatuomba tukuwe tunaenda ku mikutano juu anatupenda, na anajua kama ile mikutano itatusaidia tufurahie maisha milele. Ku mikutano, tunatianaka moyo.
TUJIFUNZE MAMBO MINGI ZAIDI
Tuone juu ya nini Yehova hapendake tukuwe natumia sanamu wakati tuko namuabudu. Na tuone namna tunaweza kumusifu Mungu.
4. Tusitumie sanamu wakati tuko tunaabudu Mungu
Nini njo inaonyesha kama Mungu anachukiaka sana wakati tunafanya vile? Muangalie VIDEO, na kisha muzungumuzie ulizo yenye kufuata.
Mambo ilikuwa namna gani wakati watu wa Mungu walipima kutumia sanamu mu ibada yao?
Watu fulani wanaonaka kama kutumia sanamu kunawafanyaka wajisikie kuwa karibu na Mungu. Lakini hauone kama kufanya vile kunaweza njo kuwatenganisha na Mungu? Musome Kutoka 20:4-6 na Zaburi 106:35, 36, na kisha muzungumuzie hii maulizo:
Watu wanatumiaka vitu gani ao sanamu gani mu ibada yao?
Yehova iko na mawazo gani juu ya kutumia sanamu?
Na weye uko na mawazo gani juu ya kutumia sanamu?
5. Kuabudu Yehova tu kunatusaidia tuachane na mawazo ya uongo
Tuone namna kumuabudu Yehova mu namna yenye anapenda kunaweza kutusaidia tuachane na mawazo ya uongo. Muangalie VIDEO.
Musome Zaburi 91:14, na kisha muzungumuzie hii ulizo:
Yehova anasema atatufanyia nini kama tunaonyesha kuwa tunamupenda kwa kumuabudu yeye tu?
6. Tunamuabudu Yehova ku mikutano ya kutaniko
Tunamusifu Yehova na tunatiana moyo wakati tunaimba na kutoa majibu ku mikutano. Musome Zaburi 22:22, na kisha muzungumuzie hii maulizo:
Unafurahiaka kusikia majibu ya watu ku mikutano?
Hauone kama ni muzuri na weye ukuwe najitayarisha juu ukuwe najibia ku mikutano?
7. Yehova anafurahiaka wakati tunaambia wengine mambo yenye tuko najifunza
Kuko mambo mingi yenye tunaweza kufanya juu tuelezee wengine mambo yenye tuko najifunza. Musome Zaburi 9:1 na 34:1, na kisha muzungumuzie hii ulizo:
Ni jambo gani yenye umejifunza mu Biblia yenye ungependa kuambia mutu mwingine?
WATU FULANI WANASEMAKA: “Haiwezekane kumufurahisha Mungu.”
Na weye unawazaka nini?
KWA KIFUPI
Tunamufurahisha Mungu wakati tunamuabudu yeye tu, wakati tunamusifu ku mikutano, na wakati tunaelezea wengine mambo yenye tumejifunza.
Maulizo ya kujikumbusha
Nini njo inaweza kutusaidia kujua namna ya muzuri ya kumuabudu Mungu?
Juu ya nini Yehova tu njo mwenye tunapaswa kuabudu?
Juu ya nini tunapaswa kumuabudu Mungu pamoja na watu wengine wenye nao wanapenda kumufurahisha?
HABARI ZINGINE
Mu habari “Nilishakaacha Kuabudu Sanamu,” soma namna mwanamuke mumoja aliacha kuabudu sanamu.
“Biblia Inabadilisha Maisha ya Watu” (Munara wa Mulinzi, 1 Mwezi wa 7, 2011)
Ona mambo yenye inaweza kukusaidia ukuwe unajibia ku mikutano.
“Umusifu Yehova Katika Kutaniko” (Munara wa Mulinzi, Mwezi wa 1, 2019)
Ona namna mikutano ilisaidia kijana fulani mwanaume hata kama alikuwa na magumu ya kufika ku mikutano.
Watu wengi wanawazaka kama musalaba ni alama ya Ukristo. Lakini tunapaswa kuitumia mu ibada yetu?
“Juu ya Nini Mashahidi wa Yehova Hawatumiake Musalaba mu Ibada?” (Inapatikana ku Enternete)
a Ile mambo itazungumuziwa mu somo zingine.