Maulizo ya kujikumbusha ya sehemu ya 3
Uzungumuzie hii maulizo na mwalimu wako:
- Musome Mezali 27:11. - Juu ya nini unapenda kuwa mushikamanifu kwa Yehova? - (Ona Somo ya 34.) 
 
- Nini njo inaweza kukusaidia kukamata maamuzi ya muzuri wakati Biblia haionyeshe waziwazi jambo ya kufanya? - (Ona Somo ya 35.) 
- Unaweza kufanya nini juu uonyeshe kama uko munyoofu mu mambo yote? - (Ona Somo ya 36.) 
- Musome Matayo 6:33. - Unaweza kufanya nini juu ya kuonyesha kama ‘kuendelea kutafuta kwanza Ufalme’ njo jambo ya maana zaidi kuliko kazi na makuta? - (Ona Somo ya 37.) 
 
- Unaweza kufanya nini juu ya kuonyesha kama unaona uzima sawa vile Yehova anauona? - (Ona Somo ya 38.) 
- Musome Matendo 15:29. - Unaweza kufanya nini juu ya kuonyesha kama unatii sheria ya Mungu kuhusu damu? 
- Unawaza kama mambo yenye Mungu anatuomba tufanye inafaa? - (Ona Somo ya 39.) 
 
- Musome 2 Wakorinto 7:1. - Tunaweza kufanya nini juu mwili yetu, vitu vyetu, na mwenendo wetu uendelee kuwa safi? - (Ona Somo ya 40.) 
 
- Musome 1 Wakorinto 6:9, 10. - Biblia inasema nini juu ya ngono? Unakubali mambo yenye Biblia inasema? 
- Biblia inasema nini juu ya pombe? - (Ona Somo ya 41 na 43.) 
 
- Musome Matayo 19:4-6, 9. - Mungu anatoa kanuni gani juu ya ndoa? 
- Juu ya nini kuandikisha ndoa na kuvunja ndoa inapaswa tu kufanywa ku serikali? - (Ona Somo ya 42.) 
 
- Ni sikukuu gani zenye Yehova hakubali, na juu ya nini? - (Ona Somo ya 44.) 
- Musome Yohana 17:16 na Matendo 5:29. - Nini njo inaweza kuonyesha kama hauunge mukono upande wowote? 
- Kama sheria ya serikali inapingana na sheria ya Mungu, utafanya nini? - (Ona Somo ya 45.) 
 
- Musome Marko 12:30. - Unaweza kufanya nini juu ya kuonyesha kama unamupenda Yehova? - (Ona Somo ya 46 na 47.)