Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • lmd somo 6
  • Ujasiri

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Ujasiri
  • Penda Watu—Juu Ufanye Wanafunzi
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Mambo Yenye Yesu Alifanya
  • Mufano wa Yesu Unatufundisha Nini?
  • Umuige Yesu
  • Je, wewe unahubiri kwa uhodari?
    Huduma Yetu ya Ufalme—2000
  • Endelea Kusema Neno la Mungu kwa Ujasiri
    Huduma Yetu ya Ufalme—2005
  • Andika Majibu ya Maulizo Haya
    Programu ya Mukusanyiko wa Muzunguko wa 2018-2019—Pamoja na Mwangalizi wa Muzunguko
  • Utusaidie Tusiogope
    ‘Tumuimbie Yehova kwa Furaha’
Ona Habari Zaidi
Penda Watu—Juu Ufanye Wanafunzi
lmd somo 6

KUANZISHA MAZUNGUMUZO

Yesu anamuambia Zakayo ashuke ku muti, na watu fulani wenye wako naangalia wanashangaa.

Lu. 19:1-7

SOMO YA 6

Ujasiri

Kanuni: “Mungu wetu alitufanya tusikuwe na woga ili tuwatangazie ninyi habari njema.”​—1 Tes. 2:2.

Mambo Yenye Yesu Alifanya

Yesu anamuambia Zakayo ashuke ku muti, na watu fulani wenye wako naangalia wanashangaa.

VIDEO: Yesu Anamuhubiria Zakayo

1. Angalia VIDEO, ao usome Luka 19:1-7. Kisha ufikirie maulizo yenye kufuata:

  1. Ni mambo gani yenye ingefanya watu waogope kumukaribia Zakayo?

  2. Hata vile, nini njo ilifanya Yesu aende kumuhubiria?

Mufano wa Yesu Unatufundisha Nini?

2. Tuko na lazima ya ujasiri juu tuhubirie watu bila kuwabagua.

Umuige Yesu

3. Umutumainie Yehova. Vile tu roho ya Mungu ilimupatia Yesu nguvu ya kuhubiri, inaweza pia kukupatia na weye nguvu. (Mt. 10:19, 20; Lu. 4:18) Umuombe Yehova akusaidie ukuwe na ujasiri juu uhubirie watu wenye wanaweza kukuogopesha​—Mdo. 4:29.

4. Usikuwe haraka kuhukumu mutu. Unaweza kuogopa kuhubiria mutu pengine juu ya namna anaonekana kwa inje, juu iko tajiri, juu ya tabia yake, ao juu ya mambo yenye anaamini. Lakini kumbuka hii mambo:

  1. Yehova na Yesu njo wako na uwezo wa kusoma mioyo ya watu; siye hatuna ile uwezo.

  2. Yehova anaweza kusaidia mutu yeyote mwenye anapenda.

5. Ukuwe na ujasiri, lakini pia ukuwe na heshima na ukuwe muangalifu. (Mt. 10:16) Usibishane. Wakati unaona kama uko mu hatari ao mutu hapendi kusikiliza habari njema, kwa heshima unaweza kusimamisha mazungumuzo.​—Mez. 17:14.

ONA PIA

Mdo. 4:31; Efe. 6:19, 20; 2 Ti. 1:7

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine