Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w13 1/3 uku. 16
  • Maulizo juu ya habari za Biblia yanajibiwa

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Maulizo juu ya habari za Biblia yanajibiwa
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Juu ya Nini Yesu Anaitwa Mwana wa Mungu?
    Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
  • Sababu Gani Mungu Alimutuma Yesu Duniani?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Yesu Kristo Ni Nani?
    Biblia Inafundisha Kabisa Nini?
  • Yesu Kristo Ni Nani?
    Biblia Inatufundisha Nini?
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
w13 1/3 uku. 16
[Picha katika ukurasa wa 16]

MAULIZO JUU YA HABARI ZA BIBLIA YANAJIBIWA

Sababu Gani Yesu Anaitwa Mwana wa Mungu?

Mungu hana bibi ao muke halisi ambaye alizaa naye watoto. Yeye ni Muumbaji wa viumbe vyote vyenye uzima. Wanadamu waliumbwa wakiwa na uwezo wa kuiga sifa za Mungu. Ndiyo sababu Adamu, mutu wa kwanza ambaye Mungu aliumba, anaitwa “mwana wa Mungu.” Vivyo hivyo, Yesu anaitwa “Mwana wa Mungu” kwa sababu aliumbwa akiwa na sifa kama zile za Baba yake.​—Soma Luka 3:38; Yohana 1:14, 49.

Yesu aliumbwa wakati gani?

Mungu alimuumba Yesu mbele ya kumuumba Adamu. Kwa kweli, Mungu alimuumba Yesu na kisha akamutumia ili kuumba vitu vingine vyote, kutia ndani malaika. Ndiyo sababu Biblia inamuita Yesu ‘muzaliwa wa kwanza wa viumbe vyote’ vya Mungu.​—Soma Wakolosai 1:15, 16.

Yesu aliishi mbinguni akiwa kiumbe wa roho mbele ya kuzaliwa huko Bethlehemu. Wakati ulipofika ili Yesu azaliwe kama mwanadamu, Mungu alihamisha uzima wa Yesu kutoka mbinguni na kuuweka ndani ya tumbo la uzazi la Maria.​—Soma Luka 1:30-32; Yohana 6:38; 8:23.

Sababu gani Mungu aliruhusu Yesu azaliwe kama mwanadamu duniani? Yesu alitimiza daraka gani la pekee? Unaweza kupata majibu kwa maulizo hayo katika Biblia, na majibu hayo yatakusaidia sana kuongeza ujuzi wako na shukurani yako juu ya mambo ambayo Mungu na Yesu wamefanya kwa ajili yako.

Ili kupata habari zingine, soma sura ya 4 ya kitabu hiki: Biblia Inafundisha Kabisa Nini?, kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine